Wednesday, January 27, 2016
2.Millard Afrael Ayo.
 Mwandishi wa habari  , aliowahi kupewa tuzo ya mtangazaji bora wa kiume anayependwa(2014), mwaka mmoja mbele, 2015, taaluma ya habari inamfanya atabasamu kwa kufanikisha ufunguzi  wa Kituo binafsi cha redio alichokiita TZA.Ndani ya mwaka huo tabasamu inaendelea kushamiri baada ya Millard Ayo. Com Kutunukiwa tuzo ya Website/blog inayopendwa Tanzania. Katika tuzo za watu zilizofanyika Hyatt Legency, Dar es salaam. Ushindi huo unakuja kwa kuziacha tovuti nyingine  kama; issamichuzi.blogspot.com,  jamii forum. Com,  dj chokamusic. Com. 2015 pia ilistawisha mbegu za tabasamu jingine pale huyu mtu wa nguvu anayesihi watu wakae karibu na speaker za redio,  kuanzisha Application(Millard Ayo app) inayopatikana Google play na play store.App Inayosaidia wapenzi wa Habari anazotoa wasipitwe na chochote kile.  Lakini tujiulize, Millard Afrael Ayo ni mtu wa namna gani?...Huyu ni miongoni mwa Watanzania wabunifu,  anaejua kutumia muda,  wazo, pesa,  na watu  kwa dhamira ya kutimiza ndoto zake. Ndani ya muda wa miaka 11 (toka 2004 alipoanza kazi ya utangazaji had 2015 mwaka wa neema) Millard katoka ngazi ya ufukara mpaka Ile ya maisha bora. Wakati miaka 11 sio muda kidogo kwa hayo mabadiliko makubwa aliofanya. Huo muda umezaa mawazo na mipango yakinifu ikiwemo; kufanya kazi na vituo bora vya matangazo Tanzania (redio one /itv, clouds fm ) .Muda umezaa fikra za kuboresha production, show na matangazo ya hewani yatakayofanyika chini ya Radio yake.TZA. Mpango ambao ni moja ya malengo  matano ya siri, anayosema" muda ukiwa tayari nitaweka wazi "  Kuhusu pesa je?, Ujue sio rahisi kila mtu kutunza sh. mia na hatimae siku moja utimize kiasi cha million moja. Uwezo wa namna hii unapatikana ndani ya kingo za nafsi chache zilizokusudia kweli  . Millard Ayo  anasemaje "kwa malimbikizo ya mshahara amepata nguvu ya kununua vifaa vyote vya TZA. "kununua camera na mic za kisasa zinazotumika na Millard Ayo TV. Matumizi ambayo sio tu yanaimarisha anachokipenda (kazi) bali pia humsogeza karibu na watu. Mpaka mwaka 2015 Millard Ayo ni kipenzi cha watu. Anayeshika namba Tatu (3)Kwa kuwa mtanzania maarufu aliyefikisha idadi  ya followers million moja na zaidi  huko mitandaoni(instagram) . Huku namba moja ikishikwa na Mwanamuziki Abdul Nasib maarufu "Diamond Plutnumz" Namba mbili inakamatwa na aliyekuwa mwandani wake Diamond na miss Tanzania 2007, Wema Abraham Sepetu. Watu ni kiungo kikuu cha mafanikio ya Millard. Bila pongezi, maoni, chuki, upendo na ushirikiano wao, zile ndoto, fedha, muda, na bidii pekee visingemfikisha hapo alipo leo. Kila lakheri millard 

0 comments:

Popular Posts