Tuesday, July 15, 2014
Kombe la dunia(2014) ilikua ni michuano ya kabumbu,ambayo ilianza tar 12 mwezi june na kuisha 13 july, huku  ilikonga mioyo ya wanamichezo na mashabiki wengi wa kandanda.Mashindano hayo hayakuisha yakigusa hisia za wadau wake tu, bali hata wasio sehemu ya michezo hiyo ,walivutiwa.Vituo kadhaa vya redio hapa nchini vimeripoti matukio mengi yalioambatana na kombe la dunia.Ikiwemo kuongezeka kwa kipato na ajira za misimu na za kudumu hasa katika televisheni,TV cable,Ving'amuzi na mabanda ya kuonyesha mpira.Sifa hizo za kombe la dunia ni njema kwa upande mmoja ,na mwiba  kwa sehemu ya pili.Huu upande  ni pale michuano hiyo ilipopelekea  kuhatarisha ndoa za watu, kuiba muda mwingi wa wanafunzi, kuvunja ratiba za kazi hasa kwa watumishi wa  usiku.Ikumbukwe kuwa kila baada ya miaka minne kombe la dunia huandaliwa, na huenda pande za faida na hasara zikatatokea tena  . Lakini mbali na yote ni mhimu mtu mmoja mmoja akajipangia utaratibu wa kuburudika na tukio hili la kihisoria huku asiwe muathirika mkubwa wa changamoto  zake. Na kitu cha mwisho ni swali,je umewahi kutambua mchango wa majina haya ;Ricky Martin,Shakira , KnaanPitbull, Jenifer Lopez,Claudia Leitte, ? Haya  ni majina ya nyota na wanamuziki walioshika ngao ya burudani kwa nyimbo zao moto moto  katika makombe yaliopata kutokea.Nyimbo hizo zilizotenda haki ya burudani ni kama La Copa de la Vida (The Cup of Life 1998),"Hips Don't Lie (Bamboo mix 2006),''Waka waka(its time for Africa 2010)'', Waving flag 2010,"We Are One (Ole Ola 2014)","La La La (Brasil 2014)"  .Miongoni mwa vibao hivyo, leo ni  viashiria  na  nembo   za vipindi   katika vituo vya redio na televisheni nyingi hapa nchini. Kutambua mchango zaidi wa hayo majina tazama nyimbo  zifuatazo. 

2.

3.

4

5.

6.

7.

8.

9.


Popular Posts