Monday, February 24, 2014

Matokeo ya kidato cha nne ya mwaka 2013 yanatoka tar 21 februari 2014 , huku mabadiliko kadhaa yakijitokeza. Mabadiliko haya ni pamoja na sura mpya ya ufaulu, masomo, mbangilio wa alama, mpangilio wa madaraja,  uwiano wa wasichana na wavulana, uwiano wa shule binafsi na shule za serikali . Katika ufaulu kiwango cha panda kwa asilimia 15.17 toka asilimia 43.08 mwaka 2012 hadi asilimia 58.25 mwaka 2013. Upande wa masomo , watahiniwa wafaulu zaidi somo la Kiswahili kwa asilimia 67.77 na wafanya vibaya katika hesabu, Basic Mathematics , ikiwa ni kwa asilimia 17.78 tu. Mpangilio wa alama umeangalia A= 1 , B+= 2, B= 3, C= 4 , D= 5 ,E= 6 na F.Matokeo ya mwaka 2013 yamekuwa na pointi (alama) nyingi tofauti na miaka mingine, ukiachilia mbali  daraja la kwanza lenye pointi (9 - 17), daraja la pili lina   pointi (18 - 24), daraja la tatu  pointi (25 - 31), daraja la nne likiwa na pointi (32 - 46)  na mwisho daraja la sifuri linalofunga madaraja yote kwa pointi (47-nakuendelea).Kwa miaka iliyopita madaraja yalikuwa  kama ifuatavyo; i (9 - 17), ii (18 - 21), iii (22- 25), iv (26 - 33) na zero (34 - nakuendelea).  Katika matokeo haya  wavulana  wanaongoza wasichana ikiwa ni kwa uwiano wa asilimia  59. 58  kwa  asilimia 56. 73 . Na Shule binafsi zikitoa wahitimu wengi waliofaulu sana zidi ya shule za serikali zinazotoa wachache. Nafasi za juu zinakamatwa na shule za binafsi huku zaidi ya shule 10 za serikali zikikamata nafasi ya mwisho. Na hizi ni shule 10 bora  matokea kidato cha nne 2013    

1. St.Francis Girls (Mbeya) st




2. Marian Boys (Pwani)
 


3. Feza Girls (Dar-es-salaam)


4. Precious Blood (Arusha)


5. Canossa (Dar-es-salaam)


6. Marian Girls (Pwani)
 





7. Anwarite Girls (Kilimanjaro)


8. Abbey (Mtwara)


9. Rosmini (Tanga)


10. DonBosco Seminary (Iringa)


Saturday, February 15, 2014
Kwa mujibu wa mtandao mashuhuri duniani unaoeleza  maada na mambo mbalimbali , Wikipedia the free encyclopedia. Kusoma  ni mchakato wa kutambua na kubaini  alama, unaopelekea mtu kujenga maana. Maana hupatikana katika mpangilio  wa alama husika.Alama hizi ni kuanzia irabu , konsonanti hadi silabi. Ambazo kwa pamoja huunda neno,   kirai, kishazi na hatimaye sentensi .Sentensi pia hujenga aya , na hizi aya  zikiungana  huunda kitu kinaitwa  habari . Wakati unagundua jinsi  mfumo mzima ujengao habari unaundwa na vipengele vidogo vidogo zaidi ya kimoja .Kusoma na kuelewa habari pia kunaundwa na mbinu kadhaa. Kutoa mwangwa zaidi juu ya huu muundo wa usomaji katika  makala, kitabu au chanzo chochote cha maarifa. Tazama hizi mbinu   nne  za usomaji .
1. Kusoma kwa kina neno baada ya neno katika habari (Usomaji dhati)'Intensive reading'

2.Kusoma habari kubwa ukipitia upesi maeneo baadhi tu, na sio kila neno (usomaji wa haraka   zaidi )'scanning reading'

3.Kusoma   ili kupata maana ya habari kwa ujumla  (usomaji kawaida)'extensive reading'

4.Kusoma kwa kulenga dhana na wazo muhimu tu katika habari,na kuacha maeneo mengine.
(usomaji haraka)'skimming reading'
 

Popular Posts