Sunday, October 27, 2013
Kuna vitu vingi  binadamu ni vigumu kuviepuka. Moja ya vitu hivi ni kitendo cha kusinzia, kulala au vingenevyo utavyopenda kuita. Usingizi unamahusiano ya karibu sana na maisha yetu ya kila siku. Furaha, wasiwasi  na aina nyingine za hisia huathiriwa kwa kiasi kikubwa na usingizi. Mbali na kuathiri, usingizi hutawala hali nzima ya kila siku. Kwa    kutekeleza vyema , kawaida au vibaya katika  majukumu. Majukumu haya ni pamoja na kusoma, kutibu, kufundisha n.k. Sababu ipelekeayo  aina fulani ya utekelezaji  leo, ni matokeo ya muda na masaa ya usingizi mtu aliopata kusinzia jana  . Baadhi ya tafiti na chunguzi za kisayansi zinaonyesha binadamu kwa wastani hupaswa kulala kwa masaa yasiopungua manane(8). Mafanikio haya ya kisayansi katika tafiti na uchunguzi hayakutinananga hapo tu, bali yalijikita ndani zaidi na kupata mwanya wa kutoa faida kadhaa zitokanazo na usingizi. Na hivyo zifuatazo ni faida tisa zitokanazo na usingizi.

1.Kujenga kinga ya mwili


2.Huboresha kumbukumbu

3.Huwezesha kutafakari vyema

4.Kuharakisha umetaboli''metabolism''

5.Huleta hali nzuri''good mood''

6.Hupunguza mfadhaiko''stress''

7.Hupelekea kujifunza vyema

8.Huchochea umakini''concentration''

9. Hupunguza uzito  wa mwili

Popular Posts