Monday, July 18, 2016

Nashindwa hata niongelee vipi neno tatizo.Sababu kila mmoja ana maana yake.Na matatizo yanatofautiana kutoka kwa mtu hadi mtu.Familia hadi familia,ukoo hadi ukoo,jamii hadi jamii.na taifa hadi taifa.Nchi za dunia ya tatu zikiwa na matatizo ya maji safi na barabara nzuri.Mataifa ya dunia ya kwanza yanapitia makosa kadhaa ili kutafta amani  ya milele na upendo wa kweli.Jamii ya wafugaji ikiwa na tatizo la ardhi kwa matumizi ya mifugo  na wanyama.Jamii ya wakulima inapitia makosa kadhaa ili kupata ardhi kwa matumizi ya mazao na mashamba.Sote kwa nyakati mbalimbali tunakumbwa na shida zisizoligana.Tunatenda makosa yasiofanana.Na muda mwingine tunakuwa hivi kulingana na athari hasi ya mafunzo tuliyopata. Tulifundishwa shule,mwenye akili ni yule asiyekuwa na matatizo  ni yule asiyefanya makosa.Mwenye vema nyingi za zoezi ni mshindi.Mwenye maksi kubwa za mtihani ni wa kwanza.Mwenye makosa mengi ni mjinga ni wa mwisho hata baada ya masahihisho picha hiyo haibadiliki kwa huyo mtu.Tuliaminishwa hivyo tukasadiki hivyo.Kumbe hata kuamini hivyo kwa asilimia 100 ni makosa bado.Kwa sababu mambo yanakawa kinyume tunapoingia mitaani.Huku anayekosea sana na kujisahihisha ndiye mshindi, ndiye anayesogelea mafanikio ndiye anayeitwa tajiri.Hakuna tajiri aliye na stori ilinyooka.Kuna mahala alishindwa ,alikatishwa tamaa,aliogopa  lakini akapiga moyo konde na kuendelea. Umewahi kumsikia.Edson Thomas aliyefanya majaribio ya taa 10,000 bila mafanikio.Taa ya 10,001 ndio ikamletea heshima na utajiri.Au umewahi kusikia stori ya Abraham Lincolin,Rais wa marekani aliyeshindwa biashara tatu wakati wa ujana, akapigwa chini  mara saba katika  kampeni wakati wa kutafta nyasifa za kisiasa?.  Mpaka baadae ndipo anakuwa rais wa awamu ya 16 ya  hilo taifa lenye nguvu duniani.Hivyo hatuna haja ya kuogopa kukosea kwani haya maisha yanaturejesha kwenye maana mpya kabisa ya neno tatizo au matatizo. kosa au makosa.

1.''Kama hujawahi kukosea hujawahi kujaribu kitu kipya'' Albert Einstain

2.''Makosa ni kiashiria cha ukomo wa maarifa yako''Robert Kiyosaki


3.''Matatizo ni kipimo cha mtu na akili''Luther king jr

4.''Kila mbele ya tatizo kubwa pana fursa njema inakusubiri''

5.kukimbia tatizo hakulitatui bali kunaongeza umbali kati ya tatizo na utatuzi
6.Mwanvuli haukati mvua ispokuwa unatupa ujasiri wa kusimama katikati ya mvua,matatizo hayakwazi maisha isipokuwa yanatupa utashi wa kujikwamua.
7.Tatizo ni sawa na mashine ya nguo katika kazi na madadiliko,tegemea  kufikichwa,kukunjwa,kusuguliwa mpaka uwapo safi zaidi ya ulivyokuwa hapo  mwanzo
8.Tatizo ni sawa na dirisha litakupa upeo wa mbali endapo utalisogelea.

9.Matatizo ni kipimo unahitaji mafanikio kiasi gani.Unavyoyatatua mengi, mafanikio yako yanaongezeka.

Sunday, July 10, 2016
Mambo!. Kila kukicha  kinazaliwa kipaji kipya Tanzania.Na kila ,mwaka kunazaliwa studio mpya mtaani.Tangu sanaa ya mziki igeuke ajira.Vijana wa kibongo wameikimbilia fursa.Hakuna anayetaka kubakia shabiki kama mimi au wewe.Vijana wanataka kuwa wasanii na maproduza. Wanatamani kulingana au kumzidi Diamond na Alikiba,Nahreel na Lamar.Ni kitu kizuri kuwa na mtazamo wa mafanikio.Lakini ni kitu kibaya kutoweka daraja thabiti la kufikia hiyo ndoto au hayo mafanikio..Sitaki uchoke ndg ila nakumbusha tu kuwa,huwezi  kuitwa msanii au kufanya sanaa  ,Kama hauna mbinu na  akili ya ziada. Bilashaka unatambua kuwa hata mvuvi hawezi kuvua samaki iwe sangara au pweza, bila ujuzi. Mfano Mvua sangara anaamini hawezi kupata sangara kwa kutumia chakula asichokipenda sangara .Halikadhalika mvuvi wa  pweza anatambua hatoweza kumpata pweza bila kuiingia kwenye maji yanayopendwa  na pweza. Wembe ni ule ule mmoja hata kwa wewe unaetaka kufanya mziki hapa nchini, bila kujali ni Hiphop, taarabu, kwaito zuku, bolingo, segere, singeli, baikoko n.k. Huwezi kujizolea wafuasi bila kujua wanachopendelea .Bila kujua tabia ya mziki.Na kuonekana mjuzi kama yule mvuvi anayejua samaki anahitaji nini ,inachukua mbinu na akili ya ziada kama nilivyotangulia kusema,Gharama na nguvu pia .Kati ya mbinu nyingi ambazo unazijua,umezisikia .Kuna  chache nakukumbushia  ambazo kwa namna moja ama nyingine naamini zitakusogeza mahala katika jitihada na harakari za kuwa msanii nyota wa mziki Tanzania.


 1.Uandishi .Joh Makin anasema''Uandishi wa nyimbo ni feeling na feeling ni kama mtu anavyopata mtoto yaani kuna uumbaji''Lady Jay Dee anaelezea zaidi kwa kusema''mara nyingi nyimbo mimi ninazoandika huwa ni vitu vya ukweli ambavyo aidha ni kwangu au kwa jamii''
.

2.Collabo(kushirikiana). Msanii Alikiba anasema''Unaweza kufanya nyimbo na mastaa isiwe nzuri,Staa kwa staa.Unaweza kufanya na underground(chipukizi) na ikawa nzuri.Sometimes feeling zina kuwa tofauti tunaamka  tofauti''

3,Manager: A.Y anaelezea kuwa''Kuna vigezo vya kunimeneji mimi cha kwanza ufanye kazi atleast mara tatu ya mimi ninavyofanya kazi, kingine ni lazima huyo manager aje na networking(mtandao)wake''.Na kuhusu wasanii chipukizi anaongezea'' mtu hana single au anayo moja hajapata nafasi ya kutengeneza atleat hit song(nyimbo nzuri pendwa) nne kujipima na wasanii wengine,hapo hapo anataka manager,huwezi kuwa na manager wakati hujaijua biashara yako hata kwa kiasi fulani''


4.Promo(utanbulisho na matangazo ya wimbo):Ommy Dimpozi anashauri''Kwenye huu mziki kuna aina ya promo inaweza kufanya mziki usikae sana,inakuwa kama unavumisha kitu vuu kweli kina kuja na ule upepo alafu  ukipotea upepo na nyimbo inapotea na watu wanataka tena nyimbo mpya.Kwa hiyo kuna zile aina za promo za vurugu zinaweza sababisha nyimbo zisikae''

5.Kujiamini.Jaji maarufu wa kipindi cha kusaka vipaji vipya,Bongo star search bwana master Jay anasema''.Msanii anatakiwa kuwa mtu ambaye anajiamini kupita kiasi,hutaki kuwekeza hela yako kwa mtu ambaye ana kipaji lakini hajiamini.Mtu mwenye kipaji nusu na kujiamini mia anaweza kufanya vizuri kuliko mwenye kipaji mia na kujiamini nusu''
,
6.Fanya research(tafiti) Profesa jay anasema''Ukitaka kufanya mziki mzuri lazima ufanye mziki wa watu,sio ufanye mziki wangu(mtu binafsi),so lazima ufanye research watu wanahitaji nini na kwa muda gani,lazima uangalie jamii yako inayokuzunguka,ambayo unataka kuiimbia ipo katika situation(hali) gani ,kama wanataka bata(anasa,furaha) waimbie nyimbo za bata,kama wapo kwenye stuation ngumu waimbie nyimbo za kuwapa moyo''

7.Mafanikio: Mambo makubwa yote  wanayomiliki wanamziki hayatokani na mziki pekee.Mwana Fa anasema''Nilichogundua ni kwamba wasanii wote matajiri,hawafanyanyi mziki pekee hawawi matajiri kwa sababu yamziki.Mifano yote hai tunayo''



8.Hitimisho;Msanii Chemical anasema''Sanaa ni kuchukua kile ulichonacho ukijumlisha na vya watu wengine vingi''

Popular Posts