Monday, September 15, 2014
Kuna wakati sisi wananadamu hupoteza mwelekeo  kama boti ndogo inayopigwa na dhoruba kubwa baharini. Ni muda ambao maisha huturushia tope, mawe, miiba na kila aina ya shida, Katika wasaa huu ni kawaida mtu kubaki njia panda, aidha kuendelea ama kutoendelea na jambo fulani alilokusudia hapo mwanzo. Tunapochagua kuendelea, huwa tumecheza karata sahihi. Kwani  mafanikio ni hali inayoanzia chini na baadae kufika juu ya kilele cha maendeleo aliyojipangia mtu mmoja. Watu wengi tumewahi kufanikiwa kwa namna moja ama nyingine. Lakini kadiri tunavyopiga hatua moja mbele , vikwazo navyo hutuvuta kwa hatua mbili  nyuma. Bila shaka umewahi kuona filamu ya nchini Thailand inayoitwa Ong Bak?. Ndani ya sinema hii kadiri  starling anavyopiga maadui ndivyo wanavyozidi kuongezeka. Halikadhalika na maisha ya kawaida, hali huwa hivyo .Jinsi tunavyofanikiwa zaidi na  mambo  huwa mengi zaidi. Hata Nasib au Diamond Platnums, mwanamuziki anayefanya vizuri Afrika mashariki.Hivi sasa ana ziara nyingi za muziki, Kenya,Uganda,Rwanda,Burundi na Ulaya.Hali inayomfanya,ajifunze lugha za kigeni, aandae nyimbo nzuri, afanye mazoezi ya kutosha kuliko wakati hajaanza sanaa ya muziki. Hii inatokana na ukweli kuwa ,mafanikio ni safari moja ambayo huanzisha mambo mengine. Mbali na sanaa hata katika biashara , tajiri Bill Gates ambaye sio  mgeni  masikioni mwetu. Anakiri kuwepo kwa changamoto katika mafanikio licha ya kumiliki na kuendesha miradi mikubwa ulimwenguni. Mtu huyu aliyeanza uwekezaji   akiwa na umri wa miaka tisa  ,kapitia shida ya kimasomo hata safari yake ya elimu  ikayumba kiasi. Lakini leo hii   anatuuzia vifaa,program,computer,smartphones .Bidhaa zinazoundwa na kampuni yake iitwayo  Microsoft.Hivyo   wafanyabiashara ,wasanii na sisi tunakila sababu ya kutokata tamaa na kufanikiwa ili mwisho wa siku tutimize mahitaji  yafuatayo:

1
. 

                               

2.Usalama wa maisha

                                                                                         

3. upendo na mahusiano 

                                                              

.4.Uwezo na heshima.

                                                            

.5. Uhuru katika
















Thursday, September 11, 2014
Ibrahim na Neema huvutiwa sana na mitindo.Ndoto yao juu ya tasinia hii ilianza kwa kupenda   haiba na unadhifu.Wakiwa ni vijana wasio na ajira hawakuweza kutafta mvuto kwa namna inayohusisha gharama kubwa.Hawakuweza kuingia  gym, hawakuwrza kumudu vifaa maluum vya bei mbaya. Hali iliyopelea mmoja kati yao kutafta mwalimu  wa mazoezi ya mwili kwa njia ya mkopo. Na mwingine kujisimamia katika mazoezi ya aina hiyo bila mwalimu kabisa. Neema alipata msaada mkubwa toka kwa huyu mwalimu wa mazoezi. Ibrahim halikadhalika  alifanikiwa kutokana na bidii aliyojiwekea katika mazoezi. Wawili hawa katu hawakukata tamaa ya mazoezi hata siku moja kwa kuwa walipenda michezo kuliko kitu kingine.Walipenda  kuwa wanamitindo kuliko kazi nyingine. Walivutiwa na uzuri kuliko sifa nyingine. Baada ya miezi mitatu kupita  huku zoezi ni kama dini na kitu cha muhimu kwao, mmoja wa vijana hawa anatokea kuwa kisura aliyevutia sana na mwingine ni mtanashati aliyependeza sana. Huku siri yao kubwa kufika hapo walipo ndani ya muda  kidogo, ikitokana na  juhudi katika mazoezi yafuatayo..

1,KURUKA KAMBA. Ni zoezi rahisi lisilochukua gharama kubwa.Zoezi hili linafanyika sehemu nyingi kwa sababu vifaa vyake ni rahisi kubeba na hupatikana kwa uepesi.Kwa kuwa linahusisha mikono,miguu,mgongo na viungo vingine vya mwili,huongeza stamina,nguvu na kukaza misuri ya mrukaji. Ni moja ya zoezi zuri katika kupunguza uzito wa mwili.

2.KUKIMBIA.Ni zoezi linalofanyika uwanjani,barabarani,mbugani na sehemu nyingi za uwazi mkubwa.Zoezi hili hupendeza pasipokuwa na jua kali hasa majira ya asubuhi na majira ya jioni..Ni moja ya zoezi zuri kwa mapafu na moyo.Kwani viungo hivi hurejesha msukumo wa damu na hewa  kuwa vyema,kiasi cha mkimbiaji kupata nguvu na pumzi ya kutosha katika mwili wake.

3.PUSH UP. Ni zoezi rahisi, linalochukua gharama ndogo sana na gharama hii ni muda pekee . Mbali na muda, push up hazihitaji uwanja  mpana zaidi ya chunba chako. Kwa kupiga push up ndani ya nyumba itakusaidia kukaza mwili sehemu ya juu. Ukianza na kupanuka  kifua, ikifuatiwa na kuimarisha mabega, mikono  mgongo na  tumbo. Ni zoezi zuri kwa ukakamavu

4.KUOGELEA . Ni mchezo ambao huvutia watu wengi, watoto kwa wakubwa wenye kipato na wasionacho. Lakini wakati karibu kila mmoja anafurahai mchezo huo, kuna faida nyingi mwili hupata  Kwanza ni mara mbili ya zoezi la kukimbia, na huimarisha misuli ya mwili kutokana na ukinzani wa maji. Pili huondoa mfadhaiko na msongo wa mawazo, tatu ni zoezi linalohusisha
miguu, mikono, mabega na viungo vya mwili karibu vyote na baadae mwili hujengeka na kukaa fiti.
5.KUENDESHA BAISKEL. Kwa kuendesha tu usafiri wa baiskel ni sehemu ya zoezi muhimu sana kwa afya . Miguu inapokazana kupita mpando na ama tambarare.  Mwili unashitua misuli inayosukuma nguvu zaidi . Zoezi hili linasaidia ubongo kwa kuwa makini na kunakiri chochote kinachoendelea. Unapofikia hatua ya kutoa jasho wakati wa zoezi hili , inasaidia kupunguza taka mwili na mafuta yasiotakiwa mwilini. Hatimaye mwendeshaji mwenye uzito mkubwa atakuwa anapunguza uzito endapo tu ataendesha baiskel mara kwa mara.

Popular Posts