Saturday, February 27, 2016
Kila wakati wengi wetu katika maisha, ni watu wa kujiwekea malengo. Mara nyingi huwa tunaweka malengo haya,  kwani kwa kujiwekea  malengo hayo ndiyo hutuongeza na kutuhakikishia  kule tunakotaka kufika kimafanikio. Kwa kujua hili, karibu kila mtu msaka maendeleo, kwake malengo huwa ni kitu cha lazima sio cha kuuliza tena.
Lakini hata hivyo, pamoja na kujiwekea malengo mazuri,  kwa bahati mbaya sana tena wengi wetu huwa bado hatuyafikii malengo hayo. Hapo ndipo maswali mengi sana ya kwanini huanza kuibuka vichwani kwetu? Kama mambo ni hivyo usikate tamaa, Kwa kufatilia makala haya utajifunza juu ya mambo muhimu yatakayokusaidia kufikia malengo yako.
1. Yajue malengo yako vizuri.                                                                        
Huwezi kufanikiwa kama huyajui malengo yako vizuri. Ni lazima malengo yako yawe ya wazi kwako. Ikiwezekana yaandike vizuri kwenye karatasi nayaweke sehemu inayoonekana. Kwa mafano kama lengo lako ni kufanya biashara ya ‘stationary’ liandike lengo hilo mahali na lionekane.  Kama pia lengo lako ni kufungua duka weka wazi lengo lako kwa kuliandika.
Watu wengi mara nyingi wanashindwa kufikia malengo yao kwa sababu malengo yao yanakuwa sio wazi sana. Siku zote mawazo yetu ya ndani hutusaidia kufikia malengo yetu, kama malengo hayo yana eleweka. Kinyume cha hapo, utakaa sana kusubiri malengo yatimie lakini wapi. Hivyo siri ya kufikia mafanikio jitahidi kuweka malengo yako wazi.

HAKUNA CHA KUKUZUIA KWENYE MAFANIKIO UKIAMUA.
2. Jitoe kikamilifu.
Siri ya mafanikio ni kujitoa kikimalifu kwa kile unachokifanya. Hata malengo yako ambayo umeshajiwekea na yako wazi ili kuweza kuyafikia ni lazima ufanye juu chini kujitoa kikamilifu na wala sio nusunusu. Ikiwa utakuwa unayaendea malengo yako, huku ukiwa hujaamua kujitoa kikamilifu tambua ikatokea umeshindwa usishangae hapo kwa hilo.
Kwa kuwa unanajua malengo yako nini, kama kuna kazi unatakiwa kuifanya ifanye kweli kwa nguvu zako zote bila kuchoka. Weka juhudi na maarifa yako yote na kuhakikisha unajitoa kweli. mafanikio yako hayatakuja kirahisi eti kwa kufanya kazi kilegevu. Jitoe kwa kupiga kazi kwelikweli mpaka kieleweke.
3. Kamilisha majukumu yako kila siku.
Unaweza ukawa unayajua malengo yako na umejitoa kikamilifu, lakini huwezi kuyafikia malengo yako kama kila wakti unakuwa hukamilishi zile kazi zinazotakiwa  kukusaidi kuyafikia malengo yako. Hapa sasa ndipo unapotakiwa kujilazimisha na kuhakikisha kila jukumu ulilonalo  unalikamilisha  kwa siku husika.
Kwa mfano kama wewe ni mfnyabiashra ulitakiwa kupga mahesabu Fulani ya kukusidia, fanya hivyo bila kuacha. Halikadhalika akama wewe ni mwandishi na umejipangia kuandika kurasa mbili kwa siku, pia fanya hivyo bila kuacha wala kuahirisha. Kwa kukamilisha majukumu yako kila siku itakusaidia kufikia malengo yako kuliko ambavyo ungefanya mambo nusunusu.
4. Yagawanye malengo yako.
Malengo yoyote ulinayo yanaweza kufikika. Haijalishi malengo hayo ni makubwa kivipi lakini uwezo wa kuyafanikisha upo, ikiwa tu lakini utafuata hatua za kuyakamilisha malengo hayo. Pengine unajiuliza kivipi au nitawezaje kuyakamilisha malengo yangu makubwa? Ni rahisi tu na hata wewe unaweza.
Kulielewa hilo vizuri ngoja nikupe kisa kimoja moja ambacho kinaelezea siku moja fisi mkubwa alimkuta fisi mdogo akimla tembo. Fisi Yule alivyoona vile alicheka sana na kumuuliza utamaliza lini? Fisi Yule mdogo alimwambia nitamla kidogo kidogo mpaka ataisha. Kwa kutumia mfano huo hivyo, ndivyo unavyotakiwa na wewe kufanya kwa malengo yako makubwa. Unajiona una malengo mkubwa yagawe vipande vipande mpaka uyafikie..
5. Tafuta msaada.
Ni rahisi kuyafikia malengo yako, kama utatafuta msaada wa kukusaidia kuyafikia malengo hayo. Acha kung’ang’ania kukamilisha malengo hayo ukiwa peke yake. Yaangalie malengo yako yana husu nini kisha baada ya hapo jiulize je, ni mtu gani au watu gani  ambao wanaweza kunisaidia kukamilisha malengo haya.
Kwa kujua watu ambao watakusaidia kukamilisha malengo yako itakusaidia sana kushirikiana nao kwa ukamilifu na kwa ubora wa hali ya juu hadi kufikia mafanikio yako. Tambua na elewa sio kwa sababu malengo ni yako, hivyo unatakiwa kuyakamilisha mwenyewe, hapana. Tafuta kile unachokosa, kisha omba msaada.
6. Kuwa chanya wakati wote.
Kuna wakati tunapokuwa tunajiwekea malengo huwa tunakutana na changamoto nyingi sana ambazo zinatukatisha tamaa. Sasa hali hii inapokutokea ni vyema ukajitahidi ukawa chanya wakati wote. Acha kukataa wala kujiona hufai, endelea kusonga mbele kati kati ya changamoto hizo ulizonazo wewe.
Kuwa chanya wakati unatafuta mafanikio inalipa sana. Tuchukulie kwa mfano unafanya biashara halafu ukapata hasara, hapo unafanyaje? Utaacha au itakuaje? Jibu ni kuendelea  na safari ya mafanikio kwa kutambua kwamba hiyo nayo ni hatua ya mafanikio pia. Ndiyo maana tunasema ni muhimu na lazima kuwa chanya ili kuyafikia mafanikio yako.
 7. Kuwa tayari kuyapitia malengo yako kila wakati.
Pamoja na kwamba umejwekea malengo vizuri, umejitoa kabisa kwenye malengo hayo, lakini hutakiwi kusahau kabisa kuyapitia malengo yako. Ni muhimu kuyapitia tena na tena malengo kwa kutambua wapi ulipofikia, nini kinachokukwamisha na ufanye nini ili uweze kusogea hapo ulipo kwa kasi zaidi.
Watu wengi wenye mafanikio wanayapitia malengo yao. Wanapita malengo yao asubuhi, wanapitia malengo yao mchana, wanapitia malengo yao jioni. Picha kamili ya malengo yao inakuwa ipo kichwani mwao tayari. Hiki ndicho kitu ambacho unatakiwa ukifanye hata wewe. Pitia malengo yako kila wakati ili yaumbieke vizuri na itakusaidia kuyakamilisha.
8. Jifunze kufurahia mafanikio kila hatua unayopitia.
Pamoja na kujiwekea malengo yetu makubwa, lakini kumbuka kuna yale malengo yetu madogo madogo ambayo huwa tunayashinda. Inapotokea umefanisha jambo fulani, hata kama kwako ni dogo ni vyema ukajifunza kulifurahia. Furahia mafanikio yako siku hadi siku kwa jinsi unavyoyapata. Hiyo itakupa nguvu ya kufanikisha mambo mengine.
Kama kweli una nia njema ya kufikia mafanikio makubwa, basi hayo mambo ni ya msingi sana katika kukusaidia kufikia malengo yako makubwa uliyojiwekea. Jukumu lako kubwa ni kuhakikisha unayaweka kwenye vitendo mambo hayo.  Na kwa kufanya hivyo basi utaweza kufikia malengo yako na kutakuwa hakuna wa kukuzuia.

Nikutakie siku njema na endelea kujifunza kupitia DIRA YA MAFANIKIO kila wakati. Usikose kuwaalika wengine waweze kujifunza kupitia makala tunazozitoa hapa.

Ni wako rafiki katika kusaka mafanikio ya kweli,
Imani Ngwangwalu,
Simu; 0713 04 80 35,
Siku zote maisha ya mwanadamu yanaaongozwa na miiko au kanuni. Ni miiko hiyohiyo ambayo ilianza toka zamani lakini ambayo lengo lake kubwa lilikuwa ni kutuelekeza mambo yapi tufanye na mambo yapi tusiyafanye katika maisha ili tufanikiwe. Wale waliofuta miiko hiyo ni kweli walifanikiwa, na wale walioikiuka walishindwa katika maisha yao kwa naman fulani.

Kwa bahati mbaya au nzuri miiko au kanuni hizo zinafanya kazi katika maisha yetu mpaka sasa. Wengi huwa hawajui katika hili, lakini upo umuhimu mkubwa sana wa kuijua na kuifuata hiyo miiko au kanuni na kuamua kuachana na mambo ambayo yanawezayakawa kizuizi kwetu cha mafanikio. Katika makala hii tutaangalia mambo ambayo ni lazima tuyaache ili tufanikiwe.

Yafuatayo Ni Mambo Unayotakiwa Kuyaacha katika Maisha Yako.
1. Acha kuruhusu makosa madogo madogo, hatimaye yakawa makosa makubwa na yakakuzuia kufanikiwa .

2. Acha kukimbia changamoto zinazokukabili, pambana nazo mpaka ufanikiwe na kufikia mafanikio makubwa katika maisha yako.

3. Acha kusahau kule ulikotokea. Yapo mambo ya kujifunza kutokana na kule tulikotoka.

4. Acha siku zote kujijengea tabia ya kulalamika. Kama utaebndelea kufanya hivyo utashindwa katika mambo yako mengi sana .

5. Acha kamini kuwa utashindwa kwa kile unachokifanya. Kila mara na kila wakati amini wewe ni mshindi wa maisha yako.

6. Acha kuruhusu pesa ikakutawala. Matokeo yake itawale pesa na hiyo itakusaidia kufikia uhuru wa kipesa.

7. Acha Kurusu hofu ikakutawala maisha yako. Kwa kadri utakavyozidi kuwa na hofu ndivyo ambavyo maisha yako yatazidi kuwa mgumu. Hiyo yote ni kwa sababu utashindwa kufanya mambo yako kwa sababu ya hofu ulizonazo.

8. Acha kuanzisha biashara, huku ukiwa unategemea bahati ndiyo ufanikie. Ondoa mawazo ya bahati na fanya biashara yako kwa kujimini, utafanikiwa.

9. Acha kujijengea tabia ya kufurahia, hasa ple mambo yaw engine yaopkuwa mabaya. Badala yake wape moyo na kuwafariji.

10. Acha kuogopa kusonga mbele, hata kama kuna wakati unahisi kama vile unakwama. Wewe endelea kukazana na kusonga mbele na mwisho wa siku utafanikiwa.....

Makala kwa msaada wa mwungwanablogspot.com

Popular Posts