Saturday, July 27, 2013
Ni miongoni mwa  maswali ya msingi sana hapa duniani ,mtu kuhoji,kudadisi na kujiuliza maisha  ni nini?Kwa kuwa maisha yanagusa kila mwanadamu bila kubagua kama  ni mwalimu au mwanafunzi,amesoma ama hakusoma .Tutangalia aina mbili za elimu.Elimu rasmi na elimu isiyorasmi( formal and non-formal education).Hapa kuna tumaini jema katika kufahamu ukweli na pengine maana juu ya maisha.Kwani kuna misemo na maana nyingi sana za maisha katika aina hizi mbili za elimu .  Kama ilivyo katika misamiati mingine mingi , msamiati wa maisha umeibuka gumzo hata kupelekea wanafalsafa ,wasanii  na waelimishaji  wengi kujaribu kuongelea  maisha.Mawazo yao katika maana ya maisha ,inatofautiana sana kutoka kwa mtu mmoja hadi mwingine.Tofauti kubwa ni katika mtazamo, uwezo wa kutafakari na kufikiri .Kutoka Tanzania tutangalia misemo na maana mbalimbali za maisha zitokanazo na wasanii watano(5)sambamba na sanaa zao za muziki.

1. "Maisha ni kama kioo ukiyachekea nayo yanacheka"Fid q



2."Maisha ni kama gwaride kuna mwisho na wa kwanza ikisikika nyuma geuka wa mwisho anakuwa wa kwanza"Stamina

3.''Maisha siyo  komborela ukasubiri kubutua jipange jitume ipo siku utafunua"Nay wa Mitego


4."Maisha ni kutenda na siyo majaribio"Mrisho Mpoto


5."Amini wewe ndiye steringi na maisha ndio sinema"Prof jay

0 comments:

Popular Posts