Saturday, December 12, 2015
Furaha huanza juu  na kumalizikia chini kama moto wa mshumaa,  na ikiwa chini hurejeshwa tena juu ili iangaze nafsi kama jua linavyoangaza dunia. Unakumbuka sio mara moja tumesikia furaha ikipotea.Baada ya muda inarudi?.Basi wakati ikipotea hujificha, ili simanzi itutawale , na  huzuni itufike. Tuwapo ndani ya hizi hali hujiona wapweke na hatufai kama tone la chozi mbele ya mvua . Ni upweke na uchungu huu ambao  nafsi hupitia , hatimaye mtu mmoja anadhamiria kuitafta furaha kwa gharama yeyote.Wakati mmoja akifanya haya, furaha huwa inarejeshwa juu taratibu ili uzito wa amani ukae mioyoni mwetu .Faraja na neema zije juu ya  amani. Pale furaha yote inaporudi huyo mtu atakuwa na sababu kubwa ya kuishi na kupendeza. Kwani sakafu ya moyo wake imepata kile ilichokosa kwa muda mwingi. Tabasamu la huyu mtu sasa lazima  ling’ae  Kuliko  hata nyota iwakayo saa nane za usiku.Ikiwa unataka usitengane na furaha unashauriwa kufuata njia zifuatazo

1.TUMIA FURSA.Ukitaka kuwa mtu wa furaha kila mara, usishindane na hali,usigombane na watu hata kubishana sana kwa sababu ya tukio fulani.Kwani siri ya furaha ni kuruhusu kila hali ije kama ilivyo na sio wewe unavyofikiria ni lazima iwe.Na kisha thubutu kuitumia kwa style na mbinu zako zote.


2.KUBALI UWEZO WAKO.Kwa maana ya kawaida uwezo ni ile nguvu ulionayo,kiasi cha fedha unachopata ,au idadi ya mali unayomiliki, Mitaji hii na mingine mingi  ni nyenzo kuu ya kukutoa sehemu moja  hadi nyingine.Kwani sisi husahau kuwa furaha haipatikani kwa kumiliki kila  kikubwa unachotamani, bali furaha huja kwa kuthamini kile kidogo ulichonacho toka mwanzo.

3.PENDA CHANGAMOTO.Kuna misemo ya kihindi isemayo kuwa  ''hata nyota isingeweza kun'gaa kama kusingekuwapo na giza'',''Hata mvua isingeweza kunyesha kama kusingekuwapo na joto''Ikiashiria kupata kitu kimoja ni lazima  kutambua mchango wa kitu kingine ambacho ni kibaya ama kizuri.Kwa maana  huwezi kuthamini ukimya kama hujawahi kusikia kelele na huwezi kuthamini furaha kama hujapata uchungu.Furaha ya kweli ni mbegu inayoota baada ya shina la uzuni kuanguka.mizizi ya chuki kung'auka.

4.TAFTA MAFANIKIO.Hapa usichanganye haya maneno mawili; mafanikio na ushindi.Ushindi ni dhana inayoambatana na  mapambano ama mashindano baina ya mtu mmoja na mwingine.Lakini mafanikio ni ile funguo ya furaha baada nguvu , fedha, mipango kufikia malengo ya juu.Haya malengo chanya ndio hatua kubwa unazopaswa kuzifikia ndani ya siku,wiki,mwezi n.k Kulingana na ulivyojiwekea.Mafanikio ni chakula muhimu kwa kila moyo  wa furaha.

5.CHAGUA MTAZAMO SAHIHI.Hii ni namna tunavyoangalia mambo.Ni jinsi tunavyofanana au kutofautiana na wengine.Chunguzi za masulara ya furaha zinasema.Mtu anayetizama kazi za mwenzake  kwa mtazamo chanya .Huambukiza furaha mara dufu zaidi ya mwingine atazamaye shughuri hizo kwa mtazamo hasi.Na tafiti ikaongezea kuwa kadri unavyotoa furaha kwa wingi ndivyo unavyopokea kwa wingi .

  

Popular Posts