Thursday, November 12, 2015
Japokuwa kuna giza,mwanga,mwezi , jua , bado siku hazifanani.Kama hivyo ndivyo ni kitu gani hasa hufanana?.Siku zote wewe na mimi tumeumbiwa uhitaji.Kwa maana nyingine kila siku tunaongeza idadi ya vitu tunavyopenda,tunavyotaka. Vitu hivi vinaweza kutengwa  katika mipango na katika uchumi. Katika uchumi,mimi napenda  mshahara mkubwa.Bila shaka hupendi kuingiza pato dogo ,unapenda? .Haya mahitaji ya kifedha ni sehemu ndogo kati ya ile kubwa iundayo mahitaji yetu  ya msingi.Yaani malazi,makazi,chakula na mavazi. Katika upande mmoja ukubwa wa mahitaji ya msingi umepanuka kiasi cha kuziba  macho yasione mipango rahisi ya kujikwamua.Kwani tuzibwapo na kipindi cha njaa,usingizi,baridi n.k .Huwa ni ngumu kufikiria mipingo ya muda mrefu au ya kudumu itakayotuepusha  na taabu hizo.Na upande wa pili ni wakati unapokuwa huru husurutishwi na chakula, malazi, makazi, mavazi.Katika hii saa ambapo hatujazibwa na mahitaji tunaweza kuweka malengo, kuoata ndoto, kufanya mipango na kupendekeza mbinu. Hizi harakati na mipangalio   zinavuma tokea ndani ya mioyo yetu zikipita vichwani na kutua akilini. Akili ndio makao makuu ya kila ndoto,mipango na mbinu tulizojiwekea.Kwa kuwa hii sehemu ya ubongo ni mhimu kwetu kama nahodha ndani ya  meli.Basi tunapaswa kuitunza, kuiboresha na kuitumia   kwa uangalifu. Ahsanteh kwa watu  waliotufunza kusoma na kuandika, kwani kwa kitendo chao tumetambua akili hutiwa mwanga. Akili hutolewa gizani. Akili hubadirika. Akili hupokea maarifa kulingana na mambo yanayoizunguka.Na ili tufikie mahitaji ya kifedha na ya msingi tunapaswa kuwa waalimu wa akili zetu, tukizifundisha kulingana na somo zuri linalojiandika katika kuta za familia , mitaa, jamii na maeneo mengine tunayoishi.  Zikiwemo kata, wilaya , mikoa ,nchi ,bara n.k.Bila kuchukua mazuri ya sehemu uliopo akili hizi tunazilisha sumu .Itakayoua 'future' zetu .
Thursday, November 5, 2015
Kuna msemo wa miaka mingi usemao apandaye haba atavuna haba. Maana yake inaendana sambamba na maisha ya vijana wawili waliotoka familia tofauti. Mmoja ni Paul mwenye miaka 20 aliyetoka familia duni ,  na mwingine ni Michael mwenye miaka 21 aliyetoka familia bora.  Hawa vijana kulikuwa na kitu kilichoondoa tofauti zao. Hiki kitu ilikuwa ni kiu ya mafanikio. Kila mmoja alitamani maisha mazuri. Kulikuwa hakuna njia ya kupata hayo maisha bila kuhusisha wazazi wao. Paul alimwendea baba ake aliyekuwa mfugaji na mkulima akiomba maelekezo namna gani ataweza kufanikiwa. Baba ake  alimwambia mwanaye jambo asiloweza kutegemea. Hili jambo halikufanana na lile Michael aliloambiwa na mzazi wake. Michael alipomsihi baba ake,ampatie siri ya kupata mali na fedha kama zilizopo nyumbani. Mzazi wake alimcheka sana kabla hajasema yafuatayo. ''mwanangu mimi sikupata chochote toka kwa baba angu, babu yangu alisema kitu kimoja ambacho nataka usikisahau maishani mwako, sisi tumebarikiwa katika lolote tutakaloanzisha, likiwa sahihi utakuwa tajiri kama mimi ama marehemu babu yako''  Baada ya mazungumzo hayo Michael alianza safari ya kutafta maisha . Tukirudi kwa  Paul tunamuona  akianza safari ya maisha huku neno la mzazi wake likiwa kichwani na kumrudia mara kwa mara . Mzazi wake alimwambia kuwa ''mifugo na mashamba alionayo alipewa na baba ake,''  akasisitiza kuwa baba ake alisema ''wao hawakuumbiwa mafanikio  mengine wataendeleza mashamba na mifugo kwa kizazi hadi kizazi ''Lakini Paul hakuwa mtu wa kukata tamaa. Aliondoka kwao akaanza  maisha katika biashara. Biashara  ya kwanza ikafeli,  akafanya ya pili ikafeli,  ya tatu ikafeli, ya nne ika feli, Kabla hajaanza biashara ya tano .Paul  mwenye miaka 26 sasa  .alikumbuka kauli ya mzazi wake ''wao hawakuumbiwa mafanikio  mengine wataendeleza mashamba na mifugo kwa kizazi hadi kizazi'' ndipo akafanya hiyo biashara ambayo nayo kwa bahati mbaya ilishindikana. Paul aliketi chini na kutafakari kisha akarudi kwao  kuwa mkulima na mfugaji kama babu yake ,Huku kijana mwenzake( Michael) anatoka kwao na mtaji aliotafta mwenyewe anaanza na biashara ya kwanza inampa hasara, ya pili inamtia hasara , ya tatu inamtia hasara , ya nne inamtia hasara, ya tano inamtia hasara ya sita inamtia hasara ya  saba inafeli , ya nane inakwama ya tisa ina inajifunga, Katika Biashara ya kumi , Michael akiwa na umri wa miaka 30 anakumbuka maneno ya mzazi wake ''sisi tumebarikiwa,  katika lolote tutakaloanzisha likiwa sahihi umekuwa tajiri kama mimi ama marehemu babu yako'' na alipojaribu hii biashara ya kumi ikamfilisi. Lakini Michael hakati tamaa na mwisho anakuja kufanikiwa katika biashara ya 20 akiwa na umri wa mika 40 .Na kuwa tajiri kushinda hata baba  na babu yake.Kwani;

1. Ule muda wote wa makosa ulimjengea uzoefu na ujuzi mkubwa katika nidhamu ya fedha, uchumi na biashara.

2.Imani yake haikutetereka kwa maana hakuamini kwenye kushindwa 


3.Alijua hata kama huna kitu una nafasi ya kupata kitu kama tu bidii ni shina la utaftaji wa hicho kitu

4.Alibaini kuwa bahati sio kuzaliwa katika familia bora ama duni bali ni mwenyewe kuandaa mazingira yatakayopokea fursa na kuigeuza iwe ajira au mradi
.
5.Alipata ufahamu kuwa kuendelea sio lazima uwezeshwe, ukopeshwe, utaftiwe bali maendeleo yanaanza kwa chochote ulichonacho ikiwemo  wazo, elimu, nguvu , juhudi, akili,imani na bidii

6.Paul alishindwa kwa kuwa dira yake ilizimwa na maneno ya mzazi


7.Alikomea maisha ya kawaida kwa kuwa kauli ya mzazi ilitawala uwezo na mipango yake.


8.Paul hakuwa na mfano wa kuiga katika maisha zaidi ya babu yake mfugaji.

9.Kosa kubwa kuliko yote alilofanya Paul ni kitendo cha kukata taamaa.


10.Mwisho ,kufanikiwa ama kutofanikiwa ni matokeo ya sisi wenyewe tunavyosikiliza na kufanyia kazi mawazo na maneno ya watu wengine.
 

Popular Posts