Wednesday, July 22, 2015
Nilipokuwa mtoto kuna kundi kubwa la marafiki walinizunguka. Mmoja wao alijulikana kwa jina la Pola. Mie na rafiki yangu pola tulishirikiana kwa ukaribu juu ya  mambo mawili.  Pola alipenda sinema za Anord Shwarzenegger , mimi  za Jack Chan.  Rafiki angu  asipokwenda kutazama sinema,  alipenda  kucheza mpira. Ambalo ni jambo la pili lililotunganisha . Pola akikusanya makaratasi, mimi nilifuma mpira . Ujamaa wetu uliwakasirisha watoto wengine. Wangefurahi kutuona tukitengana, huku Sinema na kandanda vikiwa kando na maisha yetu  kuliko   mbingu na ardhi.
                Baada ya kuandaa mipira . Ukitukosa uwanjani tupo juu ya miti tukifanya kile tulichoamini ni mazungumzo. Na watoto wengine walikiita kuwa ni mabishano.  Mada kuu ya maneno yetu ilikuwa ni sinema.  Pola alikuwa nimwingi wa furaha tukianza hizi mada. Bilashaka  sikuleta kilio mbele ya macho yake.  Kama yeye ambavyo hakuleta kero usoni mwangu.  Mazungumzo ghafla yalikata tuliposikia filimbi (priiii).  Kwa sababu ilikuwa ni saa ya kandanda, tuliteremka viwanjani tukiungana na watoto wengine wakiwemo maadui.  Kama marafiki wengi  wa utotoni , hatukucheza kandanda katika timu pinzani hata siku moja.  Daima tulikuwa wa timu moja. Kwa kipindi kile mechi hazikufika  mwisho  bila mtoto mmoja kuwa Mohamed ali,  akipiga    ngumi na mwingine  Van damme akipiga mateke. Waliopewa kipondo ni  wachezaji waliokuwa hawana kosa. Katikati ya tifutifu sikupendezwa kuona rafiki angu akipigwa , licha ya umri wa miaka 6 niliokuwa nao, niliamini ningelimtetea Pola (niliyemzidi mwaka mmoja) , kama kuku mdogo  anavyolinda kifaranga wake baada ya mwewe  kukaribia. Sijui nini humwingia pola , kwani wakati wa vurugu jamaa alitumia siraha kama Anord Shwarzenegger (kipenzi chake). Akianza kuwatupia mawe watoto waonevu . Na kuchapa fimbo  zisizo na mpangilio  . Vita ikifikia hapa Sikukimbia, niliwakimbiza,  sikuogopa niliwaogopesha kwa mbio na ujasiri kama Jackie Chan (kipenzi changu).
            Miaka ikaenda sote tukahitimu elimu ya msingi. Nikabahatika kuingia sekondari.  Akafanikiwa kufanya biashara . Miaka ikapita nikachaguliwa form six.  Akabahatika kuwa wakala wa vinywaji vya  kokakola. Miaka ikazidi kusonga. Nikajiunga na Chuo, Yeye akajiunga na miradi mikubwa . Nikasikia Pola kaoa na kufungua biashara  za Tv, DVD , CD na ving’amuzi. Muda ukapita , nikapata ajira ya ualimu, kitengo cha  michezo. Sijasikia chochote toka kwa rafiki yangu . Mtu tuliolindana wakati wa vita ,  leo muda wa amani tunatengana. Mtu aliyenifundisha umoja, ananiacha katika  utengano. Hua sikomei hapo kuwaza. Siku za likizo,  nikifuatilia tamthilia za kikorea ,kimarekani na Uingereza. Hujiuliza mswali yasiyo na majibu.  Tungekuwa na mawasiliano na Pola angempenda mastar kama jumong?, Angemfurahia Will Smith au Harry Potter?  Hakuna wa kujibu haya maswali miongoni mwetu .Sio mimi,wala wewe isipokuwa ni Pola tu.  Kabla na wewe hujampoteza rafiki ako kipenzi ,uliepitia nae hatua nyingi za ukuaji,mateso na raha,njaa na shibe,furaha na huzuni.Napenda ujifunze jinsi urafiki wetu ulivyovunjika.

1.sote tulikuwa busy

2.Mawasiliano yalikuwa magumu tukiamini itakuwa usumbufu mmoja kuwasiliana na mwingine

3.Kisha tulidhani mmoja kati yetu atakuwa wa kwanza  kumtamtafta mwenzake


4.Baada ya kipindi najiuliza kwa nini mimi tu ndo nianzishe mawasailiaano?

5.Hatukuonyeshana upendo tuliounyeshana  thamani zetu
6.Bila mawasiliano ni wazi kuwa kumbukumbu baina yetu ilizaliwa,ikakuwa na mwisho ikafa


7.Hatimaye  tukasauliana hadi leo

Wednesday, July 15, 2015
Miaka ya nyuma ilikuwa ni miongoni mwa nyumba nzuri hiyo sehemu. Mmliki wake ni bwana tajiri ambaye kila mmoja alimtazama kwa msaada. Gari ilikuwa ni kivutio cha kila jicho. Ilikuwa ni kama ndoto iliyotimia pale mmliki alivyoongeza gari na nyumba katika idadi ya miliki zake
               Lakini leo mali zote ni chakavu na kwa mujibu wa asili ya vitu, kimoja lazima kichoke ili kingine kije. Nyumba izeeke ili  nyingine ijengwe, gari lichoke ili  jipya linunuliwe. Je unadhani ni vyema kwa mtu wa namna hii , anayeishi na kumiliki hili gari la kale kuitwa mwenda wa zimu hivi sasa, na apelekwe mirembe au sehemu nyingine ya vichaa?
             Sidhani, kwa sababu  hakuna jipya chini ya jua. Nguo yako ya thamani ni dekio kwa mwingine, Salio lako la bank ni kiasi ambacho  mwingine anatoa msaada bure. Mrembo au mtanashati ulinaye leo   kaachwa na mwenzako jana. Hata dada anayeitwa kahaba pale mtaani au kule hotelini siku moja alikuwa bikira. Sasa ya nini majivuno? Maisha ni mafupi kujisikia, kujiona dhidi ya mwenzako. ’’Tungali wakosefu, hakuna mkamilifu’’  . Anasema steve job. Hakuna kitakachotusaidia wala sipendi kuona watu wakijikweza nakujivunia mali, uzuri, akili, kiwango cha elimu, umaarufu na  miliki za dunia. Mungu  anasema ’’Pendaneni na muongeze marafiki’’
                Siku zote kumbuka yule unayemdharau wakati unaelekea  juu ndo yule utakaye mkuta wakati unashuka chini.  Hivyo usiwe ni kisababishi  cha matatizo kwa mwingine. Kama utakuwa kisababishi ,  utakuwa umejipalia kaa la matatizo mwenyewe, na hakika , hao uliowaletea shida watakuwa  sehemu ya matatizo yako siku moja.
                 Mwisho  usisahau kuwa hata matawi ya mgomba  kuna siku huitwa  majani makavu. Hivyo hupaswi kupumbazwa na mali za duniani. Kwani siku moja zitachakaa na kufa.

                Endapo muda utafika ukahisi kulia,  basi niite, siahidi kukufanya ucheke siku hiyo,  lakini tutalia sote. Siku moja ukitaka kukimbilia mbali, usiogope, niite. Nakuahidi nitakimbia pembeni yako. Lakini ikitokea ukaniita na usisikie jibu, huenda  nakuhitaji.  Kwa maana siku  itakuja mmoja wetu hatokuepo tena. Na itakuwa umeshachelewa kusema ‘I care’. Machozi yatakuto lakini   haisaidii, nimeshatangulia mbele za haki. 
Tuesday, July 7, 2015
Mabadiliko ni kama maji huweza kuchukua umbo la sura yeyote. Na huweza kufuata uelekeo mmoja au zaidi. Ukitazama  sura ya teknolojia iliopo leo utabaini hii sio taswira iliokuepo jana, yaani miaka 20 iliyopita. Mageuzi haya yanatokea huku wagunduzi kuntu wakiwa ni miongoni mwa watu adimu katika hiki kipindi. Richa ya kukosekana kwa wagunduzi nguri wakiwemo; Isack Newton, Pythogrus, Edson Thomas,  kati ya miaka  1995 hadi 2015 . Kuna upepo wa mabadiliko unaoletwa na waboreshaji wanaofuata misingi ya hao wagunduzi kuntu. Wagunduzi dhahiri, wangunduzi halisi , wagunduzi waliovuma miaka yote.  Ndani ya hiki kipindi cha miongo miwili ( miaka 20 ).  Kuna wabunifu wanaochipukia na kumiminika kama utitiri.  Hawa ndio shina linaloshikilia urahisi wa maisha na urahisi wa mawasiliano katika dunia ya leo. Hali inayopelekea mambo yaliokuwa hayawezekani miaka 20 iliyopita kufanikiwa. Na hapa ni baadhi ya hayo mambo

1.IMO,SKYPE












Kitendo cha kuonana ana kwa ana baina ya watu wawili walio katika sehemu tofauti za mchi , ilikuwa ni kitendawili katika niaka ya 90.  Ahsanteh kwa teknolojia ya imo na skype kwa kuleta nyuso na sauti za watu karibu.  Wapendanao waliokuwa wametenganishwa na umbali,  masomo,  kazi na majukumu  ,sasa wanafursa ya kusalimiana na kutazamana kwa ukaribu kama pua na mdomo.

2.WHATSAPP
Ilikuwa ni rahisi  kwa mganga wa kienyeji wakati ule. Kuendesha majadiliano na watu anaowaona yeye tu , kama hiyo haitoshi aliweza kusema kitakachojiri  duniani kabla ya mimi na wewe kutambua lolote.Baada ya simu kuingia kila mtu kapatiwa uwezo huo. Tena kama ina whats app ndio mtajadiliana hadithi zote kuanzia; siasa , katiba, tamaduni , uongozi, ajira, michezo, burudani ,utabiri wa hali ya hewa,kubet n.k .Vyanzo vya hizi habari kwa mwaka 2015 sio tena ‘mafundi’ au waganga wa kienyeji  pekee bali ni rafiki zako,wanafunzi wenzako,wafanyakazi na jamaa uliohifadhi namba zao katika simu ya kiganjani mwako. Kwa kutumiana jumbe za sauti,picha na video  Whats app hukupa maarifa pamoja  na taarifa za hayo matukio mbalimbali


3.YOUTUBE
 1995,Televisheni ilikuwa ni kila kitu juu ya masuala ya video. Kuona ‘kichupa’ au video mpya ya msanii unayempenda ilikupasa utege jicho kwa luninga. Ukikosa tukio kubwa katika taarifa ya habari ulitakiwa kuwa mvumilivu hadi taarifa irudiwe, vinginevyo ungoje  kipindi maalumu au mwisho wa wiki. Hali sio hiyo tena miaka ya kuanzia 2005, na Shukrani za kipekee ziendee  youtube kwa kutupa uhondo wa video tulizokosa, tuzitakazo katika muda wowote, mahali popote na kwa mtu yeyote.  matukio makubwayaliokupita au uliyoyakosa katika tv utayapa hapa.

4.SHAZAM
Unakumbuka enzi hizo ukisikia mziki mzuri redioni, unatamani mtangazaji ataje jina la huo wimbo?. Ama unapita mahala kuna mdundo wa nyibo za ughaibuni,zinakugusa moyoni lakini hujui msanii wala jina la wimbo? Hii shida sasa imefika mwisho.Mwaka 2015 Kazi imerahisishwa sana .  Ni vyepesi zaidi ya kumsukuma mlevi. Kwa kutumia shazam unaelekeza tu simu au komputa karibu na mdundo wa nyimbo,  na ndani ya sekunde umeshapata jina la msanii na nyimbo 
.
5.GOOGLE EARTH

Zamani ilikuwa ni ngumu kufika pointi moja  bila kuwa na mwenyeji, bila kuuliza ama kupanda chombo cha usafiri. 2015 unaweza kutembea dunia nzima bila kukwea pipa, kuchukuwa treni, kupita na meli wala kupanda basi. Ikiwa una google earth na mji una ramani mtandaoni  , utaelekezwa  njia za kupita kwa mguu, kwa gari hadi sehemu za kuvinjari, hotel, supermarket, beach  na kona za afya ;  hospitali, zahanati, na maduka ya madawa baridi. Google hawatoi tu ramani bali pia vituo mhimu unavyotaka kujua
 .
6.FACEBOOK
Karibu kila mmoja ana damu ya uandishi. kubali!, kataa!. Kwa maana anafurahi kushirikisha jamii dhidi ya mafanikio  ,mipango, ndoto,  huku akitia moyo marafiki na kuomba msaada wa maombi kwa ndugu hata pongezi kuto kwa jamaa . Mmoja yupo huru kutoa mawazo na hisia zake mbele ya wengine. Hii sehemu ya maisha ya mtu mmoja dhidi ya wengine hufanyika kwa maandishi yanayoambatanishwa na picha nzuri ya mhusika. Kama ishara ya kujuza jamii nini kinachoendelea upande wake. Endapo hujui ninachojaribu kuelezea hapa,  nakusihi jiunge na facebook, ukashuhudie jinsi uhuru wa kujieleza ‘freedom of expression’ inavyotendewa haki. Ikiwa una kumbukumbu nzuri, pengine umebahatika kuishi na wezee katika miaka ya 90. Utaona  bibi na babu zetu hawakufaidi dhana nzima ya uhuru wa mawasiliano.Ukilinganisha na FACEBOOK

7.TWITTER
Nakumbuka nilisoma kitabu kimoja zamani kidogo, ambacho kilielezea namna wafalme walivyokuwa wakituma jumbe ulimenguni.Kitendo kilifanya na mtu mwenye mbio sana aliagizwa kupeleka nyaraka katika himaya nyingine , na hiyo himaya  iliteua mjumbe wao mwenye kasi sana mpaka falme ya tatu .Ambayo pia ilieneza habari katika falme ya nne. Mtindo uliendelea  mpaka falme ya sita ,saba hadi  ya mwisho.Na baada ya miaka habari ilienea ulimenguni kote. Stori ya hiki kitabu chenye maisha ya zamani, kinafunua muongozo wa teknolojia ya twitter . Kitu ambacho twitter hufanya japo ni ni ndani ya sekunde,au dakika tu. Ni kueneza habari kwa haraka, Hivyo miomgoni mwa matumizi mengi ya tweeter,  dunia nzima hujua nini kimejiri. Kwa kuendeleza habari husika iwe ni Alshabab, Sunami, mapinduzi, ongezeko la joto n.k  .Ndani ya masaa taarifa itakuwa imefika uchina, Marekani, uingereza, Brazil, Australia na Tanzania . Dunia nzima hupelekewa taarifa kwa kufanya swala endeleve linaloitwa ‘retweete’

8.INSTAGRAM
Wakati sote tunaamini bank ni nyumba ya pesa, ghala ni nyumba ya mazao na msitu ni sehemu ya miti.  Basi instagram ni nyumba au sehemu ya picha. Zamani kuona picha ya msanii, mtu maarufu au kiongozi mkubwa ilikuwa nadra,  mpaka utafte  gazeti au kutembelea maneo ya kazi zao. Ahsanteh Instagram kutuletea pozi, dizaini, mbwembwe na matukio mengi ya watu hawa katika mfumo wa picha.

9.EBAY, AMAZON, KUPATANA



Unakumbuka wakati unauza bidhaa na hakuna mteja? .Unataka kununua mali hakuna hakuna muuzaji?. Ilikuwa ni zama ya miaka ya 90. Kuanzia mwaka 2015 Ebay, Amazoni, Kupatana.com ( Tanzania )  inatoa uhuru wa kuuza na kununua bidhaa yoyote mtandaoni. Hapa utapata nyumba, mavazi,  usafiri, vitabu, mashamba n.k

10.HULKSHARE, SOUND CLOUD

Sauti ina thamani yake na ili hii haiba idhihirike haina budi kukusanywa pamoja katika mfumo flani. Miaka ya 90,   miziki ilitunzwa vyema katika santuri, kanda , cd na baadae miaka ya 2000 , zikaingia flash. Lakini ukisahau mbinu hizi . Hulkshare na sound clound ni mapinduzi makubwa miongoni mwa mengi katika kutunza, kusikiliza na kupakuwa au ku ’download’ sauti, nyimbo, midundo, mziki unayoipenda.


Popular Posts