Tuesday, January 17, 2017
Waswahili husema ‘siku hazilingani’ ni kweli. Leo ukifurahi, kesho utaduwaa. Na richa ya juhudi kubwa inayopimwa na jasho zito , majanga hayaishi kutuandama. Wakati mwingine chozi la uchungu linapita  . Jicho linazibwa  usione  fursa hata moja mbele yako. Na ghafra ukishtuka umeshajikwaa kwenye kisiki cha umaskini. Hapo utajiuliza maisha yana maana kweli?Na hakutakuwa na jibu.Maana matatizo yanakuwasha  kuliko upupu.Shida zinashamili kama magugu.Sikio halisikii habari njema tena.Ukifungulia redio  ikutie moyo ,majonzi ndo kwanza yanakithiri.  Matangazo  ni ya nafasi za shule zaidi ya nafasi za ajira, ni ya vyuo zaidi ya mahala pa kazi. Katika juhudi za kuepuka huo mfadhaiko unageuza jicho mpaka kulia kwako ambako kuna ‘tv’.Ni kipindi cha habari , bila kuamini mboni zako unajionea viongozi wakitumbuliwa Ili hali mifumo ikiachwa.Hasa elimu. Kabla hujaongeza sauti ya luninga , simu yako inayokaribia kukata ‘charge’sababu ya shida za umeme ,inaita.Ni ndugu analalamika maisha magumu pesa hakuna..Mkopeshe japo "jero" . Bila mafanikio ya kumweleza jinsi ulivyopigika,simu yake inakata hana voucher.Kufumba na kufumbua,,umeme umekata na simu inazima kumbe hata bila ya voucher kuisha bado mawasiliano yangekata tu.Ukiwa kwenye joto kali baada ya umeme kukata unabakia kutazama sura yako kwenye  televisheni iliyozima. Punde mwenyekiti wa wapangaji anakumbusha ni zamu yako kulipa LUKU,mzunguko ushakufikia. Ungali bado katika hali hii ya sintofahamu baada ya simu kumaliza moto, redio kupoteza matumaini  tv kuzima na sasa kulipa LUKU.Anakuja baba mwenye nyumba kudai chake. Utatamani kusikia maneno ya wasanii hawa.
1.’’Acha kulia ni shida za dunia ebu tulia’’Jose chamillioni
2.’’Haya yote ni maisha ipo siku yatakwisha leo mmoja anangaika mambo yamebadilika’’P funk
3. ’’Kama unapata moja kwa nini usipate na mia,hiyo inawezekana kwa wote waliona nia’’Prof jay
4.’’usikubali wakakushinda,Kwani wao waweze wananini na sisi tushindwe tuna nini’’Juma nature
5. ’’Wakati wako ndio leo kutimiza malengo yako nakusihi anza sasa jishughurishe utapata’’Ben Paul.
6.’’Na ugumu wote wa maisha shida zote za  kutaabisha usikate tama usivunije moyo’’Kara Jeremiah

Monday, January 16, 2017

Kuna milango mitano ya watu kuwa matajiri wakubwa ambayo mabilionea duniani wanatokea:


1. WATAALAMU WANAOLIPWA VIZURI
Kundi la kwanza ni wanataaluma wanaolipwa vizuri (well paid professionals) kama wanasheria wazuri, madaktari bingwa na wahandisi. Wengi waliofanikiwa katika kundi hili wanajua jinsi ya kuweka akiba na kuwekeza akiba zao kwenye maeneo yenye marejesho mazuri. Mabilionea wanaotokea kundi hili ni asilimi 10 tu ya mabilionea wote.


Image result for stephen hawking
2. WAKURUGENZI WA MAKAMPUNI MAKUBWA
Kundi lingine la mabilionea ni wakurugenzi wanaolipwa vizuri na makampuni makubwa (well paid executives). Hawa ni asilimia 10 ya mabilionea wote pia. Mara nyingi hawa huwa wametoka na kampuni mbali na wamekua nayo wakipandishwa cheo baada ya cheo mpaka kufikia hatua ya juu. Mara nyingi, watu wachache katika kundi hili huwa na uwezo mkubwa wa kuzishikilia fedha zao na kutozifuja na hiyo huwafikisha kwenye ubilionea.

Image result for executives who are billionaires
3. MAAFISA MAUZO
Kundi la tatu ni maafisa mauzo au mameneja wa idara za mauzo. Hawa huwa ni takriban asilimia 5 ya mabilionea wote na kinachowafanya wawe mabilionea ni kwa sababu ya nafasi ya kupata kamisheni kutokana na mauzo wanayoyafanya. Wengi wao huwa ni waajiriwa wa makampuni ambayo wamekuwa wakifanya nayo kazi kwa muda mrefu na kuzifahamu vizuri na baadaye kuja kuwa na milango mingi ya mafanikio.
Image result for top salesman

4. WATU WENYE VIPAJI MAALUM
Kundi la nne ni watu wenye vipaji maalumu kama wanamichezo, wanamuziki, watunzi wa filamu na vitabu na kadhalika. Hawa ni wachache sana 1%, lakini huonekana wengi sana kwa sababu ya kelele zinazoendana na umaarufu wao. 

Image result
5. WAJASIRIAMALI
Hili ndiyo kundi kubwa kuliko mengine yote, asilimia 74% ya mabilionea wote ni wajasiriamali. Hii inamaanisha kuwa nafasi ya mtu yeyote kuwa bilionea ni kubwa zaidi kupitia ujasiriamali kuliko kitu kingine chochote. 
Image result for reginald mengi biography
Sunday, January 1, 2017
     Mwaka mpya n kitu kizuri kutokea,hatuna budi kusherekea.Ila lazima tujue tunasherekea nini?.Taasisi za dini zinatufundisha kushukuru kwa kila jambo,ni sawa.Ila tushukuru tukisherekea kwa kiasi.By the way kuna sababu nyingi za kusherekea.Ikiwemo kuwa mzima,kutimiza malengo n.k.Hapa sitaongelea kwa kina habari ya sherehe na kusherekea .Nipo kwa ajili ya kushare mawazo ya watu wengine juu ya mwaka mpya.Na hapa chini wanasema

1.     Mwaka mpya ni kama kitabu cha kurasa tupu kinachosubiri kuandikwa.Tunaweza kukiandika kwa kuanza leo kujiwekea malengo.
Image result for book with empty pages
2.     Mwaka huu maombi yako yasikike  ndoto zote zitimie,jasho lote lizae .
Image result for christian muslim prayer
3.     Mwaka huu jiamini tena na upate kila unachostahili
Related image
4.     Ingawa hakuna anayeweza kurudi nyuma atengeneze mwanzo mzuri,sote tuna nafasi ya kuanza sasa na kufanya mwisho mzuri.

5.     Mwanzo wa mwaka ni mwanzo wa kufanya kila unachokusudia.

6.     Mwanzo wa mwaka ni kama karatasi nzuri isiyo na kitu.inayosubiri wewe kuiambia dunia hadithi yako
Image result for empty page
7.     Tukubali,tukatae mwaka mpya utaleta changamoto mpya,lakini tupende ,tusipende utakuja na fursa nyingi pia.
Image result for opportunity
8.     Ishi chini ya mwenye ndoto na mtendaji,anayeamini na kutafakari, lakini zaidi ya yote ishi na yule anayeona uweza ndani yako hata kama wewe  hujioni.
Image result for best company to hang with

9.     Haimanishi unatoka wapi cha msingi ni unaelekea wapi
1o.     .Kunywa kiasi,pangilia,tafta marafiki,punguza unene,kuwa chanya na tumia pesa kwa uangalifu.
Image result for no drinking

Popular Posts