Wednesday, March 8, 2017
Mama ni mwanamke anayejali,anayejinyima ili mwanae apate.Anachukia kushiba wakati mwanaye ananjaa.Anachukia kupendeza wakati mwanaye hana nguo ,anachukia kulala wakati mwanaye analia.Anapenda mtoto apate mara mbili ya apatavyo yeye.Anapenda mwanaye anawili mara mbili ya yeye.Haweki chuki ya kudumu moyoni hata kama mwanaye anaitwa msaliti wa jamii au adui wa watu.Mara nyingi hupambana kurudisha  utii  na heshima ya mwanae .Asiwe seheme na  upande chachu wa maisha.Hutoa msaada kutoka kila idara ya uwezo wake.Amwone huyo mwanae juu.Hususani katika kutimiza ndoto na malengo. Tuliobahatika kusaidiwa na huyu mwanamke wa nguvu sio mimi na wewe tu.bali pia tunao wafuatao.
1.AMBWENE YESAYA(A.Y)
Image result for ambwene yesaya
Msanii mkubwa na nguzo kongwe katika sanaa.Ana platform thabiti inayosaidia hata wasanii wenzake kupata nafasi za kushirikiana na wasanii wa nje.Kama alivyomnganisha Diamond na Davido.Lakini ukarimu na mapenzi haya ni kitu kilichofunguliwa baraka na mama yake.Anasema mama ndiye aliyekuwa mtu wa kwanza kumpatia fedha kwa ajili ya kurekodi nyimbo ya kwanza.

2.JUMA (JUX) 
Image result for juma jux
Hakuna msanii anayevaa vizuri juu ya jux .Utasema koti, tshirt, jeans ,cheni vilidizainiwa maalumu kwa umbile lake.Akiwa masomoni Uchina wanafunzi aliokuwanao walihisi ni  mmarekani mweusi.Kitendo kilichomuamsha hisia  na kuanzisha bland ya African boy.Kando na mziki,utanashati na ujasiliamali.Jux anaheshimu mchango wa mama yake baada ya kufungua pazia la neema,akimpatia pesa kadhaa kwa ajili ya kurekodi nyimbo yake ya kwanza.

3.MICHAEL(BELLE 9)
Image result for belle 9 tanzania
Anathibitisha kuimba ni kipaji anaweza kuandika chochote kikawa wimbo mzuri.Hata kama  ni kudai deni,kubembeleza mwenza au habari za kutendwa,Ni mbunifu wa sauti na mteuzi fasaha wa maneno.Huchezea lugha na kutufikia kirahisi masikioni.Akitamka masogange utapenda ilihali huelewi anachomaanisha.Akisema ''nilipe nisepe'' utamlipa deni lake faster.Akitamka sumu ya penzi,utakuwa radhi kuilamba hata kama huna maziwa.Lakini naye kama A.Y naJUX,mama yake ndiye  mzazi wa mwanzoni na msaidizi wa karibu  kumpatia sapoti ya hali na mali kwenye mziki 

4.LIL SAMIL(MR BLUE)
Image result for MR BLUE TANZAnia
Mwanzoni mwa miaka ya 2000 watoto wengi Tanzania walishawishika kurap.Na walihisi pengine ni kazi rahisi kama sindano kupenyeza nyuzi za koti.Ushawishi huo ulitokana na umaaru wa kazi nzuri za hip hop zilizovuma enzi hizo.Miongoni mwa hao watoto waliofanikiwa kupenyeza na kumantain hadi leo ni Mr blue.Wengi walifanya lakini sio kama blue.Mimi pia nilitaka kuwa kama blue halikadhalika rafiki zangu hakuna aliyemuweza Anastyle yake ya kuflow akibana maneno kwa mikogo si ya nchi hii.Hasa pale anapotamka kwenye baadhi ya nyimbo''unacheza raga'' na ''basi mororo''.Lakini kiini cha safari hii ndefu ni matokeo ya mama mzazi wa msanii huyu(wenyezi amlaze mahala pema peponi) kwa kumsapoti mwanae toka alipofaulu mtihani wa darasa la saba.

5.NASIB ABDUL (DIAMOND PLUTNUMS)
Image result for diamond platnumz
Mwisho katika list yetu ni Diamond.Ambaye namwona kama balozi wa mziki wa Tanzania kwa namna flani.Kutoka tandale, kutumia jina la Z Anto kariakoo na kufanya official video ya nje na ogopa dj ya kenya.Kutoka kwa Wema Tanzania!,kufika kwa Zari uganda! hadi kwa Coldstar Nigeria.!.Kutoka kwa Mzee Ngurumo Bongo,Papaa Wemba Congo hadi kwaNelson Mandela South Afrika(their soul should rest in peace)Kutoka nchi ya Magufuli,nchi ya Mugabe mpaka nchi ya Trump na Neyo .Lakini kitu ambachohawezi kusahau ni muumba wake na namna ya kipekee kabisa mama  mzazi alivyouza kito cha thamani ili yeye afanikiwe kuingia studio.

Popular Posts