Saturday, June 25, 2016
Wakati wengine wakisema ujuzi ni aina ya  kazi au shughuri yenye kufanyika vizuri baada ya  elimu au mafunzo maalumu.Wahenga wanasema  ujuzi hauzeeki.Kwa maana  ni  uwezo unaopatikana kwa mtu hasa akiwa amepita hatua ya  kupokea  maelekezo, na kufanya matendo mengi.Dhana ya ujuzi imekuwa ya kikazi au ki uwezo kulingana na mfumo  anaoaksi mtu..Ukiwa ni  mtumishi wa ofisi rasmi ujuzi wako itakuwa ni utoaji wa huduma inayokubalika hapo kazini kwako.Na endapo umejiajiri au kuajiriwa sekta zisizo rasmi ,ujuzi ni ule uwezo wa kutoa matokeo mazuri ya  chochote  chema unachofanya.Kwa muda mwingi njozi kubwa na fikira pana zimekuwa kama  baba na mama wa ujuzi  katika mazingira yetu.Kujua zaidi kuhusu hilo fuatilia haya maneno 10

1.Kama mmea ustawivyo kwa mbolea na sio jua kali ndivyo Ujuzi umtajirishavyo mtu na sio maneno matupu

2.Ni vyema kila mmoja akawa na kila ujuzi na asiutumie,kuliko kutokuwa na huo ujuzi na ukataka uutumie


3.Kuna sheria za kufuata ili ubahatike,na kila jambo haliundi bahati,kwa waelevu wanatambua ujuzi ni njia mathubuti ya kuwa mtu mwenye bahati


4.Kumpatia mwanao ujuzi ni bora kuliko kumpatia vipande elfumoja vya madini ya dhahabu

5.Elimu huja kwa kujifunza ila ujuzi huja kwa uzoefu.


6.Elimu pekee sio ujuzi, bali ikizidishwa mara elfukumi ndio itakuwa ujuzi

7.Marudio ni mama wa ujuzi

8.Ujuzi ni mshikamano wa  uzoefu,akili na upenzi wa jambo vikiwa pamoja

9.Ujuzi na kujiamini ni jeshi lisilopigwa wala kushindwa


10.Kama huna ujuzi  ipo siku  inakuja kipaji chako kitakwama,kwani ujuzi  ni dhana ya matendo,bidii na shauku ya kutaka uwe bora kila kukicha,

Friday, June 17, 2016
Vitu vingine vinashangaza aisee! Jana unakula visheti vya mama HasaniTandale gengeni.Leo unapata dina ya chief cooker wa hotel ya nyota tano ufaransa!.Kweli mchawi wa giza ni mwanga na adhabu ya umasikini ni utajiri.Kumbe kila mtu ni mwandishi wa sheria za maisha yake!!.Ni uchaguzi binafsi aidha katiba yako itambulike kwa rasmu za umaskini au za utajiri.Nikiangalia mbali naona kijana anayeomba nafasi majukwaani.Namuona anasimama stejini akiwa na uwoga,hawezi kushika  mic.Ni kwa sababu ni mara ya kwanza kufanya  jambo hili.Na sasa nikivuta pumzi na kupepesa macho kwa suprise!!.Namwona kijana yule yule akiwa na nguvu mikononi.Hata mic haitetemeki ni vile inajua imekamatwa na gwiji.Gwiji anasimama na mic akiihamisha kutoka mkono mmoja hadi mwingine,Akikituna nayo jukwa la mkoa mmoja hadi mwingine.Na baada ya kukodoa macho vizuri namwona gwiji yule  akiwa na magwiji wa kimataifa.Wanaotoka mashariki na maghribi mwa Afrika.Magharibi na mashariki mwa dunia.Gwiji anatokea kupendwa .Anapata wapenzi ambao miongoni mwao wanamzalia mtoto.Vyombo vya habari na mitandao inamfuatilia kila hatua anayopitia.Kila kazi anayofanya.Kila safari anayokwenda. Hadi ile ya ufaransa kwa chief cooker wa hotel ya nyota tano.Mhhhhh .Kwa vile kila mmoja amegeuzia mjadala kwa gwiji huyu inanilazimu nimjue jina lake.Kumbe anaitwa Diamond Plutnums.ha ha haa.Nimechoka kbs,Wakati nikidhani namtambua vya kutosha nashangazwa na kelele za sentensi 8 nyingine ambazo hata wewe pengine huzijui kuhusu huyu Diamond Plutnnums.

1.NIDHAMU:Diamondi anatabia ya ukweli,haweki maigizo na uongo ili aonekane ni bora.Meneja wakeBabu Tale anathibitisha hili kwa kusema kuwa''Sitaki kumsifia Dioamond ni mtu ambaye hana nidhamu ya kuigiza, kwa hiyo hawa wengine(wasnii kutoka wcb) lazima wafuate tabia za kaka yao,



2.KUJITOLEA:Anapenda kutenda wema kwa watu .Yupo tayari yeye akose  madensa wake wapate.Katika kipindi cha EFM Radio,kinachoitwa uhondo dancer wa Diamondi Mose Iyobo alisikika akisema haya.’’Kuna vitu vingine (Diamond platinum)anafanya kwa kujitolea lakini kwetu sisi inabidi atulipe’’


3.MAHUSIANO:Hana tabia ya kuchunguza simu ya mpenzi wake.Katika kipindi na Millard Ayo TV Diamond alifunguka’’Nakumbuka nilishashikaga simu ya demu wangu zamani ikanicost tangia hapo nikakoma kushika simu za mwanamke na mpaka leo siwezi kushika hata kama inaita.’’

4.CHAKULA:Hapendelei vyakula vya kwenye ndege.Akiwa nchini  ni mdau wa wali maini ndizi mbivu.Uingereza ugali nyama ya kukaanga.Nigeria egusi ,fufu,South Africa chicken tikker ,pizza
5.IMANI:Upande wa kuamini Platnums anamtanguliza Mungu mbele‘’Katika maisha ukimwomba mwenyezi  mungu na ukaweka nia thabiti na ukijutuma vinawezekana’’anasema

6.MAFANIKIO:Yeye katika swala la kupata, anaheshimu vilivyo kuwekeza katika muda,. Diamond anasema‘’Kwenye mafanikio unapata muda mfupi sana wa kupumzika’’

7.MITANDAO:Anakubali jinsi unavyotumia social networks  vyema ndivyo  unavyonufaika . .Na hapa anasema ''Ukitumia mitandao kwa njia nzuri unaweza kufika mbali.



8.KAZI:Katika ufanyaji wa shughuri mbalimbali daimondi anadira kuu moja,kazi inapaswa iwe na kiwango ama ubora wa kutosha kwani hii ni sababu ya wewe kutambulika.Katka sentence ya maneno nane amesema ''Ubora wa kazi yako ndio unakufanya uwe staa’’
Friday, June 10, 2016

Kati ya movie za kuvutia na zilizonibadilisha fikra, ni hii movie maarufu ya JUMONG.
Movie hii maarufu wengi waliiangalia na kufurahia mapigano ila mimi nilifanikiwa kujifunza yafuatayo na yakanibadili:
1. 👨🏻Baba yake na Jumong, Haemosu, alikuwa na Kusudi la kutimiza lakini hakufanikiwa kulitimiza.
Funzo: Wazazi wetu wengi hawajatimiza malengo na kusudi zao maishani, hivyo tusiogope, tuamue tu kutimiza kusudi zetu. 

2. 👨🏻Jumong hakulifahamu kusudi lake hadi pale alipokutana na misukosuko kutoka katika familia yake.
Funzo: Misukosuko ina nafasi kubwa kutubadili chanya.

3. 👨🏻Kipaji cha Jumong cha kupiga mishale na kuongoza kilimsaidia kufikia kusudi lake kubwa la kuanzisha taifa kubwa.
Funzo: Kipaji ulichonacho kina nafasi kubwa kukufanikisha maishani ukikijua na kukitumia. 

4. 👨🏻Jumong alifanikiwa kwa kujenga timu ya marafiki 👫👬wachache na kuwafanya wawe hodari na waaminifu kwake na kutambua kusudi kubwa alilonalo.
FUNZO: Chagua vizuri aina ya marafiki wa kuwa nao na kutokuwa nao. Hawa wana nafasi kubwa ya kukufanya ufanikiwe au usifanikiwe maishani. 

5. 👨🏻Jumong alikuwa ana mtazamo chanya katika kila jambo.
Funzo: Hata jambo liwe gumu vipi, bado kuna tumaini na unaweza kufanikiwa.
 
6. 👨🏻Jumong alijifunza wapi wazazi wake walikosea na akaamua kupatia 
Funzo: Jifunze kwa waliokutangulia kwani huwezi kuishi miaka ya kutosha na hadi kugundua makosa yote duniani. 
7. 🤔Pamoja na misukosuko mbalimbali aliyoipata Jumong, bado aliweza kufikia Kusudi lake kwa kuwa tu alikuwa na udhubutu na uamuzi sahihi kufuata ndoto yake.
Funzo: Fuata ndoto yako, jiamini na utafanikiwa sana.
Tuesday, June 7, 2016
Bahati ni ndoa ya vitu viwili: maandalizi  na fursa.Fursa ni msingi wajambo moja,nafasi .Nafasi ni mahusiano ya mambo matatu;nia uwezo na utekelezaji..Palikuepo na mtu mmoja alie amini katika bahati,fursa,nafasi, na utekelezaji .Huyo  mmoja alikuwa kiongozi.Uongozi wake ulijaa utani.Hata moja ya kauli yake pendwa akiwa na raia wake ilikuwa ni hii.''Ndugu wana nchi msidharau vitu vidodo,vitu vidogo vinaumiza,kama mnabisha jaribuni kukalia sindano'' .Halaiki ilikufa kwa mbavu baada ya huu utani.Ukitaka kuamini vitu vidogo ni muhimu vinaendesha dunia,na ukivithamini utafurahia ,hautaumia ungana nami kwenye hizi stori zifuatazo

1.MUHAMMAD ALI
Hakuwahi kujiona kama mpiga ngumi,au bingwa wa makonde kimataifa.Mpaka pale alikumbwa na mkasa mdogo sana.Mohamedi Ali akiwa kijana mdogo miaka kama kumi na kitu ivi.Aliibiwa baiskel anayoipenda .Na akaripoti kwa askari kuwa akimpata mwizi atampiga.Askari alimwambia atamwajibishaje mwizi yule wakati hana uwezo wa kupigana.Basi ikabidi askari amfundishe Mohamedi Ali kuchapa masungwi.Baada ya kuiva hakumtafta mwizi ila akaingia kwenye mashindano ya ngumi 

.
2.MOHAMMED DEWIJ
Safari yake ki siasa ilianza baada ya kuona tukio dogo mkoani mwake Singida.Anasimulia''Nimetoka(Singida mjini) km 6 nakutana na mzee mmoja,kulikuwa kuna maji ya njano chini ,alikuwa na ndoo na sinia,amechuchumaa akiteka maji nakutia ndani ya chombo.Nikamsalimia mzee Shikamoo,unafanya nini hayo maji,akasema haya maji ndio tunakunywa sisi.Sikumwamini hadi pale nimefika  kwake na kuona watoto wakinywa maji yale yale ,mzee akanisihi MO,kwa nini usigombee ubunge?''Sauti ikamgusa Bwana MO.MO akagombea ubunge.MO  akachimba  visima .Wananchi wa Singida  wakanufaika kwa huduma ya maji.

3.JUX
Licha ya kupenda kun'gaa  na  mziki ,Juma jux hakuwahi kufikiri kama ni mwimbaji.Jux alikuwa anafanya hip hop kama vijana wengi wa mtaani. Nini kilimbadilisha? Baada ya Jux kumsindikiza msanii mkubwa studio.anatokewa na jambo dogo linaloleta hamu ya uimbaji..Na hapa  jux mwenyewe anasimulia .''Tulienda studio na Cyril,Cyril alitakiwa kufanya collabo na Makamua .Makamua alikuwa msanii mkubwa.Basi(Cyril) akampigia Makamua,Makamua akadai atakuja, tulichoma sana mahindi pale(tulikaa sana).Kuanzia kama saa moja mpaka saa tano tano.Maneke( producer wa muziki) akawa kaweka ile Beat.Ile beat imewekwa mie nikawa kama naimba tu unajua mzuka wa studio.Maneke akasikia naimba,akasema ebu imba tena,nikaimba.Akanambia mbona unaweza kuimba kwa nini unachana(kurap).Saa izo naogopa kinoma naogopa ile mic sana,sio nilikuwa naogopa kuimba,nilikuwa naogopa kusikiliza nyimbo  yangu mwenyewe kwenye redio,nilikuwa naona aibu sana.Akasema(Maneke) unaweza kuimba jaribu.Nakumbuka ndo mara ya kwanza naingia booth kurekodi''
Thursday, June 2, 2016
''Asiyesoma kitabu kizuri hana tofauti na asiyesoma kabisa''maneno ya Mark Twain.Usomaji kwa jamii nyingi unatazamwa kama adhabu.Ukizingatia wengi tulifundishwa kusoma kwa mabavu.Kushindwa kutamka sentensi moja kwa usahihi ilikulazimu kuchapwa na mwalimu.Ukikosea neno jingine unakufokewa na mzazi,kaka,dada .Inatafsiri kuwa  nje na sababu nyingine zinazofanya tuchukie vitabu,kichapo tulichopewa bado  kinarejesha mawazo  ya adhabu tuliopata enzi za shule na nyumbani. Hali inayotuweka kando na maandishi ya vitabuni.Ukipata muda chonga bongo yako kwa vitabu hivi

1.lONG WALK  TO FREEEDOM-NELSON MANDELA

2.RICH DAD POOR DAD-ROBERT KIYOSAKI

3.FAMOUS PEOPLE 'SFAMOUS SPEECH

4.HOW TO MOVE FROM POVERT TO SUCCESS-SHIGONGO JAMES

5.THINK BIG -BEN CARSON

6.UJAMAA-JULIUS NYERERE

7.DUNIA UWANJA WA FUJO-KEZILAHABI

8.JULIUS NYERERE AHSANTEH SANA-ROBERT MGABE


Popular Posts