Tuesday, March 6, 2018
Baada ya kuangalia mafanikio ya watu.Ilifika  kipindi nikasema''Martin huu ni wasaa wako''.Nikapumzika Kusoma vitabu vya ujasiliamali ,kutazama movie za insparation na kuzungumzia ndoto za kupata mali.Nikajisemea''kwa nini nisiache maneno na kuweka kila ninachokijua katika vitendo?''Ukiachilia mbali swala la kuomba baraka na kudra za mwenyezi mungu,Mtoa ridhiki.Nilianza na vitendo katika hatua mbili tatu.Hatua ya kwanza nilitafta mtaji,pili nikatafta mradi,tatu nikatafuta sehemu ya kuweka  na mwisho msimamizi .Ndani ya miezi sita ya uendeshaji nimefanikiwa kujifunza vitu vya msingi vitano.

1.KUWA MAKINI NA MKOPO
Image result for LOAN
Pesa ya kukopa ni hatari ,kabla ya kuchukua kiasi tasilimu kutoka kwa mtu au taasisi.Andaa sehemu uliyoifanyia utafti wa kina .Kisha wekeza pesa ya mkopo.Niliongozana na rafiki zangu  wanne, sote tukachukua kiwango sawa cha pesa ila baada ya hii miezi sita.Ni mmoja tu kati ya wanee aliyefanikiwa na mkopo.

2.WEKA KANDO MATUMIZI YAKO NA PESA YA BIASHARA
Image result for business and family
Pili nimejifunza kuwa mradi wa biashara ,kama ununuzi na uzaaji wa bidhaa za rejareja unahitaji uvumilivu sana.Biashara hii inapenda uwekezaji wa muda mrefu .Kila pesa ya mauzo iandikwe na kuachwa hapo ofisini.Kitendo cha kuamisha faida ,kitendo cha kuchanganya mapato na matumizi binafsi au ya familia ni sumu kwa ukuaji wa mradi wako.Miezi itaenda ,mwaka utakata biashara yako ingali vilenvile.

3.USIMWAMINI MTU KATIKA PESA AU BIASHARA 
Image result for never trust anyone
Karibu kila mwenye pesa nyingi aidha  aliwahi kudhurumiwa,kutapeliwa ama kuibiwa.Kwa wasiofahamu huwaona wenye miradi kama mabahiri,wachoyo wasiosaidia.Ila toka niingizwe mkenge na vijana tuliokuwapamoja.Imani kwa kila ninayeshirikiana naye kwenye biashara imetoweka.Kila anayetaka mkopo, kuazima kiasi kikubwa cha pesa namuona ni wale wale tu.

4.BIASHARA NI MAISHA NA TABIA YAKO
Image result for creating yourself
Biashara siyo kazi au ajira.Biashara ni tabia ya mtu ni  mfumo wako wa maisha.Wengi wanaofeli kwenye hatua ndogo kama hii yangu.Walifanya kosa ambalo nimekumbana nalo mara nyingi.Binafsi nilikuwa na tabia ya huruma halikadhalika kuamini watu.Nikawa mkopeshaji mzuri tena asiyeweka hata rekodi saaa nyingine.Nilipendenda kupunguza bei kupia hata ile niliyomumulia.Baada ya mambo kuanza ugumu hasara kukithiri,Mwenyewe nilibadili mfumo wa maisha na hii tabia  mpaka biashara nayo ikaanza kubadilika,

5,KUWA MBUNIFU NA JITUME KULIKO ULIVYOWAHI KUJITUMA
Image result for work hard and smart
Kila unachotaka kukiona kesho ndani ya biashara yako,kianzishe sasa.Usikubali kulala kabla hujafanya jukumu ulilojiwekea.Mimi nilikuwa na ndoto kubwa  katika biashara,Sikuwahi fikiri kama nitachukua muda mwingi kukuza biashara kwanza kabla ya kunufaika.Ndani ya miezi sita nahangaika na kuweka muonekano wa ofisi usadifu dira yangu,Najifunza mbinun kadhaa za kuleta wateja wapya kila mwezi.Pia najifunza uwezo walionao wapinzani wangu dhidiya udhaifu wangu.Mwisho nikitaza vizuri najiona nasogea nilipokusudia jana.


Thursday, April 13, 2017
Kuishi ni sayansi inayotegemea majaribio mengi.Kinachoshindikana leo kirudiwe tena kesho.Huko ndo kuishi.Usifanya kosa na kukata tama .Kufanya hivyo ni kujichimbia kaburi lako mwenyewe.Ukikosa tone la maji sasa jipe moyo kuna bahari inakusubiri mbele.Rudia hicho kitu,hizo hatua hiyo shughuri naamini utaifikia bahari yako.Ukiteleza leo kamwe usifunge kichwa nakuamini unabahati mbaya.Una mkosi una ‘’gundu’’.Lah hasha huna hizo bahati mbaya isipokuwa Kuna kitu maisha yanakufunza.Yanasema jiandae muda wako unawadia,rekebisha kasoro hizi chache uwe mkomavu baadae.Tunawatu wengi kama mifano ambao walikata tama katika umri kama wako na leo wanavilio vya kudumu.Hawana namna nyingine ila isipokuwa wanaomba muda urudi nyuma wasahihishe makosa.Makosa yaliyozaliwa na chaguzi za kukata tamaa.Walipokutana na  punje moja ya mchanga waliogopa kusonga mbele.Wakizani ni lazima mbele ya safari  kuna jangwa kubwa likiwasubiri.Lah hasha.Kuishi hakuko hivyo.Kuishi ni sayansi,kuishi ni majaribio, kabla ya hitimisho fanya upembuzi wa kutosha.Mimi na wewe tungali tuna muda,tungali tuna afya,tungali tuna akili,tungali tuna pumzi.Tukiunganisha vyote hivi hakika safari yetu haitavunjika na zaidi sana tutakutana ana kwa ana na bahari iliyosheheni lulu.Lulu Isiyo ndogo kwa vipimo,wala ndogo kwa kimo.Hii itakuwa sawa sawa na mapenzi yetu.Italingana na ndoto zetu,itafanana na juhudi zetu.Lulu hii haitakuwa na upendeleo.Itatii kiu kadri ya kila mmoja alivyothubutu ,kadri ya kila mmoja alivyoitafta.

Punje ya  mchanga anaweza kuwa rafiki yako,ndugu yako,maamuzi yako au jambo lolote linalokufanya usisogee mbele.

Jangwa ni wazo pingamizi uoga ,wasiwasi,hisia lemavu kuwa siku za usoni hutofanikiwa na hicho kitu unachokifanya

Kuchimba kaburi lako ni kudidimiza uwezo binafsi uliojaaliwa na mwenyezi,ni kuweka kikomo cha kila elimu ulioipata hapa duniani.

Tone la maji ni pamoja na  fursa,bahati,nafasi,kazi au chochote ambacho kinamuinua mutu toka katika dhiki aliyonayo mpaka fahari na anasa anazozingoja

Bahari yako ni fahari,anasa,furaha,matarajio Yaani Kikomo kikubwa cha Starehe(K.K.S)na kila kitu ambacho ni kinyume na shida unazopitia.


 Gundu ni hali na hisia ya kutokuwa na bahati ni bayana ya nadharia zinazohusishwa na mikosi kutokubalika,kutoendelea daima. 
Wednesday, March 8, 2017
Mama ni mwanamke anayejali,anayejinyima ili mwanae apate.Anachukia kushiba wakati mwanaye ananjaa.Anachukia kupendeza wakati mwanaye hana nguo ,anachukia kulala wakati mwanaye analia.Anapenda mtoto apate mara mbili ya apatavyo yeye.Anapenda mwanaye anawili mara mbili ya yeye.Haweki chuki ya kudumu moyoni hata kama mwanaye anaitwa msaliti wa jamii au adui wa watu.Mara nyingi hupambana kurudisha  utii  na heshima ya mwanae .Asiwe seheme na  upande chachu wa maisha.Hutoa msaada kutoka kila idara ya uwezo wake.Amwone huyo mwanae juu.Hususani katika kutimiza ndoto na malengo. Tuliobahatika kusaidiwa na huyu mwanamke wa nguvu sio mimi na wewe tu.bali pia tunao wafuatao.
1.AMBWENE YESAYA(A.Y)
Image result for ambwene yesaya
Msanii mkubwa na nguzo kongwe katika sanaa.Ana platform thabiti inayosaidia hata wasanii wenzake kupata nafasi za kushirikiana na wasanii wa nje.Kama alivyomnganisha Diamond na Davido.Lakini ukarimu na mapenzi haya ni kitu kilichofunguliwa baraka na mama yake.Anasema mama ndiye aliyekuwa mtu wa kwanza kumpatia fedha kwa ajili ya kurekodi nyimbo ya kwanza.

2.JUMA (JUX) 
Image result for juma jux
Hakuna msanii anayevaa vizuri juu ya jux .Utasema koti, tshirt, jeans ,cheni vilidizainiwa maalumu kwa umbile lake.Akiwa masomoni Uchina wanafunzi aliokuwanao walihisi ni  mmarekani mweusi.Kitendo kilichomuamsha hisia  na kuanzisha bland ya African boy.Kando na mziki,utanashati na ujasiliamali.Jux anaheshimu mchango wa mama yake baada ya kufungua pazia la neema,akimpatia pesa kadhaa kwa ajili ya kurekodi nyimbo yake ya kwanza.

3.MICHAEL(BELLE 9)
Image result for belle 9 tanzania
Anathibitisha kuimba ni kipaji anaweza kuandika chochote kikawa wimbo mzuri.Hata kama  ni kudai deni,kubembeleza mwenza au habari za kutendwa,Ni mbunifu wa sauti na mteuzi fasaha wa maneno.Huchezea lugha na kutufikia kirahisi masikioni.Akitamka masogange utapenda ilihali huelewi anachomaanisha.Akisema ''nilipe nisepe'' utamlipa deni lake faster.Akitamka sumu ya penzi,utakuwa radhi kuilamba hata kama huna maziwa.Lakini naye kama A.Y naJUX,mama yake ndiye  mzazi wa mwanzoni na msaidizi wa karibu  kumpatia sapoti ya hali na mali kwenye mziki 

4.LIL SAMIL(MR BLUE)
Image result for MR BLUE TANZAnia
Mwanzoni mwa miaka ya 2000 watoto wengi Tanzania walishawishika kurap.Na walihisi pengine ni kazi rahisi kama sindano kupenyeza nyuzi za koti.Ushawishi huo ulitokana na umaaru wa kazi nzuri za hip hop zilizovuma enzi hizo.Miongoni mwa hao watoto waliofanikiwa kupenyeza na kumantain hadi leo ni Mr blue.Wengi walifanya lakini sio kama blue.Mimi pia nilitaka kuwa kama blue halikadhalika rafiki zangu hakuna aliyemuweza Anastyle yake ya kuflow akibana maneno kwa mikogo si ya nchi hii.Hasa pale anapotamka kwenye baadhi ya nyimbo''unacheza raga'' na ''basi mororo''.Lakini kiini cha safari hii ndefu ni matokeo ya mama mzazi wa msanii huyu(wenyezi amlaze mahala pema peponi) kwa kumsapoti mwanae toka alipofaulu mtihani wa darasa la saba.

5.NASIB ABDUL (DIAMOND PLUTNUMS)
Image result for diamond platnumz
Mwisho katika list yetu ni Diamond.Ambaye namwona kama balozi wa mziki wa Tanzania kwa namna flani.Kutoka tandale, kutumia jina la Z Anto kariakoo na kufanya official video ya nje na ogopa dj ya kenya.Kutoka kwa Wema Tanzania!,kufika kwa Zari uganda! hadi kwa Coldstar Nigeria.!.Kutoka kwa Mzee Ngurumo Bongo,Papaa Wemba Congo hadi kwaNelson Mandela South Afrika(their soul should rest in peace)Kutoka nchi ya Magufuli,nchi ya Mugabe mpaka nchi ya Trump na Neyo .Lakini kitu ambachohawezi kusahau ni muumba wake na namna ya kipekee kabisa mama  mzazi alivyouza kito cha thamani ili yeye afanikiwe kuingia studio.
Tuesday, January 17, 2017
Waswahili husema ‘siku hazilingani’ ni kweli. Leo ukifurahi, kesho utaduwaa. Na richa ya juhudi kubwa inayopimwa na jasho zito , majanga hayaishi kutuandama. Wakati mwingine chozi la uchungu linapita  . Jicho linazibwa  usione  fursa hata moja mbele yako. Na ghafra ukishtuka umeshajikwaa kwenye kisiki cha umaskini. Hapo utajiuliza maisha yana maana kweli?Na hakutakuwa na jibu.Maana matatizo yanakuwasha  kuliko upupu.Shida zinashamili kama magugu.Sikio halisikii habari njema tena.Ukifungulia redio  ikutie moyo ,majonzi ndo kwanza yanakithiri.  Matangazo  ni ya nafasi za shule zaidi ya nafasi za ajira, ni ya vyuo zaidi ya mahala pa kazi. Katika juhudi za kuepuka huo mfadhaiko unageuza jicho mpaka kulia kwako ambako kuna ‘tv’.Ni kipindi cha habari , bila kuamini mboni zako unajionea viongozi wakitumbuliwa Ili hali mifumo ikiachwa.Hasa elimu. Kabla hujaongeza sauti ya luninga , simu yako inayokaribia kukata ‘charge’sababu ya shida za umeme ,inaita.Ni ndugu analalamika maisha magumu pesa hakuna..Mkopeshe japo "jero" . Bila mafanikio ya kumweleza jinsi ulivyopigika,simu yake inakata hana voucher.Kufumba na kufumbua,,umeme umekata na simu inazima kumbe hata bila ya voucher kuisha bado mawasiliano yangekata tu.Ukiwa kwenye joto kali baada ya umeme kukata unabakia kutazama sura yako kwenye  televisheni iliyozima. Punde mwenyekiti wa wapangaji anakumbusha ni zamu yako kulipa LUKU,mzunguko ushakufikia. Ungali bado katika hali hii ya sintofahamu baada ya simu kumaliza moto, redio kupoteza matumaini  tv kuzima na sasa kulipa LUKU.Anakuja baba mwenye nyumba kudai chake. Utatamani kusikia maneno ya wasanii hawa.
1.’’Acha kulia ni shida za dunia ebu tulia’’Jose chamillioni
2.’’Haya yote ni maisha ipo siku yatakwisha leo mmoja anangaika mambo yamebadilika’’P funk
3. ’’Kama unapata moja kwa nini usipate na mia,hiyo inawezekana kwa wote waliona nia’’Prof jay
4.’’usikubali wakakushinda,Kwani wao waweze wananini na sisi tushindwe tuna nini’’Juma nature
5. ’’Wakati wako ndio leo kutimiza malengo yako nakusihi anza sasa jishughurishe utapata’’Ben Paul.
6.’’Na ugumu wote wa maisha shida zote za  kutaabisha usikate tama usivunije moyo’’Kara Jeremiah

Monday, January 16, 2017

Kuna milango mitano ya watu kuwa matajiri wakubwa ambayo mabilionea duniani wanatokea:


1. WATAALAMU WANAOLIPWA VIZURI
Kundi la kwanza ni wanataaluma wanaolipwa vizuri (well paid professionals) kama wanasheria wazuri, madaktari bingwa na wahandisi. Wengi waliofanikiwa katika kundi hili wanajua jinsi ya kuweka akiba na kuwekeza akiba zao kwenye maeneo yenye marejesho mazuri. Mabilionea wanaotokea kundi hili ni asilimi 10 tu ya mabilionea wote.


Image result for stephen hawking
2. WAKURUGENZI WA MAKAMPUNI MAKUBWA
Kundi lingine la mabilionea ni wakurugenzi wanaolipwa vizuri na makampuni makubwa (well paid executives). Hawa ni asilimia 10 ya mabilionea wote pia. Mara nyingi hawa huwa wametoka na kampuni mbali na wamekua nayo wakipandishwa cheo baada ya cheo mpaka kufikia hatua ya juu. Mara nyingi, watu wachache katika kundi hili huwa na uwezo mkubwa wa kuzishikilia fedha zao na kutozifuja na hiyo huwafikisha kwenye ubilionea.

Image result for executives who are billionaires
3. MAAFISA MAUZO
Kundi la tatu ni maafisa mauzo au mameneja wa idara za mauzo. Hawa huwa ni takriban asilimia 5 ya mabilionea wote na kinachowafanya wawe mabilionea ni kwa sababu ya nafasi ya kupata kamisheni kutokana na mauzo wanayoyafanya. Wengi wao huwa ni waajiriwa wa makampuni ambayo wamekuwa wakifanya nayo kazi kwa muda mrefu na kuzifahamu vizuri na baadaye kuja kuwa na milango mingi ya mafanikio.
Image result for top salesman

4. WATU WENYE VIPAJI MAALUM
Kundi la nne ni watu wenye vipaji maalumu kama wanamichezo, wanamuziki, watunzi wa filamu na vitabu na kadhalika. Hawa ni wachache sana 1%, lakini huonekana wengi sana kwa sababu ya kelele zinazoendana na umaarufu wao. 

Image result
5. WAJASIRIAMALI
Hili ndiyo kundi kubwa kuliko mengine yote, asilimia 74% ya mabilionea wote ni wajasiriamali. Hii inamaanisha kuwa nafasi ya mtu yeyote kuwa bilionea ni kubwa zaidi kupitia ujasiriamali kuliko kitu kingine chochote. 
Image result for reginald mengi biography

Popular Posts