Monday, January 4, 2016

Huku mwaka 2015 unamalizika.Shangwe za kukaribisha mwaka mwingine zinamiminika.Wengi  tukiwa ni washangiliaji ,tunasahau kuuliza swali alililojiuliza,rais wetu katika sherehe za uhuru,kwa nini tunasherekea?.Kutoka kwenye swali tutanweza kupata jibu kwa kutumia watu wachache kwa namna moja ama nyingine wanastahili kusherekea .Wale ambao neema iliwangukia ,walichosema kilitimia,walichofanya kilifanikiwa hata mengi waliokusudia yalionekana.Kitu kibaya kuhusu idada ya watu hawa ni kuwa japo wengi walifanikiwa tutatazama  wachache tu wasiopungua 10.Lakini Jambo zuri ,hawa sio wageni ni wale tuliozoea kuwaona kwenye michezo, dini, burudani, siasa, biashara, elimu, filamu na  sekta nyinginezo. Athari za hawa wachachehazi kuvuma kwenye tv, redio, magazeti, internet tu. Bali hata wewe walikuhusu kiganjani mwako pale ulipounga bundle ili usipitwe na habari zao.Maisha yao,mafanikio yao  na harakati zao.Unataka kuwafahamukwa undani ?, tazama mfululizo ujao.

10.JOHN JOSEPH POMBE MAGUFULI.
Ni mmoja wa watu waliopewa majina mengi mwaka 2015.Tingatinga,mzee wa msimamo,mchapa kazi,jembe n.k. Majina yote yalifutia ubora wake katika wizara  alizokwisha shika ikiwemo ya ujenzi,uvuvi,ardhi. kisha kuchukua fomu ya kugombea uraisi wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania.Jasho likamvuja kwani hakuwa peke ake katika kinyang’anyiro ni watu makumi walichuana.Hatimaye katika chama chake akatoka yeye .Hali iliomkutanisha na wapinzani wapya toka vyama vingine.Hapakuwa na njia fupi ya maisha kwa Bwana Magufuli.Zaidi ya kutia mafuta kwenye gari,weka funguo na kuzunguka nchi nzima kuwakumbusha watanzania kwa nini  yeye anafaa kuchukua ridhaa ya kuwaongoza.Mnamo Octoba 25,2015 alipaki gari na kungoja wananchi wafanye yao. Tahere 5 November 2015 mizunguko na hapa kazi tu zikazaa matunda akahapishwa kama rais wa awamu ya tano ya jumhuri wa mungano wa Tanzania.

9.Edward Lowassa.
Mwaka umekuwa wa neema kwa kile kinachosemekana kama kavunja record ya ushawishi kwa umma.Dhidi yamtazamo wao juu ya vyama pinzani, awali vyama pinzani havikuwa na nguvu kubwa kama alioleta  bwana huyu.Kwa mara ya kwanza kanda ya ziwa walipiga deki rami .Kaskazini walichora ngozi rangi ya chama chake,magharibi walipunga mikono hewani kama feni,kusini walifurika viwanjani haijawahi tokea.Vitendo hivi vilifuatia ishara ya mabadiliko na  kutokata tamaa.Alioioonyesha mgombea huyu.Kwani baada ya kutoridhishwa na mchakato wa kusaka wagaombea katika chama tawala.Alisimama wima katika chama pinzani na hivyo akafanikiwa kuimarisha ngombe ya upinzani  kuliko ilivyowahi kuwa hapo mwanzo.Kwa kuongezaa idadi ya wabunge kutoka upinzani na kufungua pazia jipya la ushindani wa kisiasa.Jina lake halitosahaulika katika historia za  hili taifa.

8.Diamond Platnums
Kama mafanikio yangekuwa yanapimwa na wingi wa majina.Diamond Plutnums  angekuwa trionea.Ukiachilia mbali jina la Naseeb  Abdul anajiita Chibwa, Dangote,rais wa wasafi,Mr ngololo,baba tifa,na sasa anajifananisha na mfalme wa chi kavu katika wanyama kwa kujiita ‘simba’.Yote tisa kumi huyu kijana kagusa mafanikio ya maana 2015.Baada ya kuingia  mgogoro wa  mashabiki (  team diamond vs team  kiba )Kijana wa majina mengi alipata muda mgumu kama sio uchungu wa mafanikiao.hali iliyomfanya atuache tumeshika vichwa kwa mshangao alipofanya kazi na wasanii wakubwa akiwemo,Neyo,Usher,A.K.A,Mafikizolo,Mr fleva.Wengi wao wakiwa ni wa afrika magharibi  afrika ya kusini na Marekani. Mwaka ukapendeza zaidi alivyotwaa tuzo ya Best Africa Act, BestWorld wide act,Best collaboration,Video bora ya mwaka n.k.Huku hizi tuzo zikiwa ni za ndani ya Tanzania,ndani ya afrika na Nje ya afrika.Dangote ama simba kama anavyojiita kakunja mkeka kwa kufungua studio inayosimamia kazi za wasanii wengine .Akiwemo Hermonize anaetamba na kibao cha Aiyola.Kama haitoshi ndani ya mwaka huo huo alipata binti yake wa kwanza waliomuita TIFA.

7.Alikiba
Huku akiwa ni baba wa watoto watatu; wa kike wawili na wa kiume mmoja.Alikiba amevuna zaidi ya alichokipanda mwaka 2015.Kufuatia kibao kimoja kuleta tuzo tano .Ambazo ni za ubora  katika uimbaji,utumbuizaji na utungaji. Sio jambo la kitoto eti.Baada ya kuachia single ya Mwana.Kiba alizimisha kelele zote redioni na ile iliyobaki ni mwana dar es salaam.Kumaanisha ilistahili kuwa nyimbo bora ya mwaka  graduation za vijijini hadi mijini,zilitumia ‘mwana’ kama nyimbo kuu katika sherehe zao.Ni kazi hii ilipelekea kuzuka  kwa ugomvi wa team mtandaoni .Baadhi ya watu waliamini king kiba yupo juu zaidi ya Diamond na wengine hawakuamini hiyvo.Unajua nini kilichofuata?Hii nyimbo bora ya afro pop ilimfanya Ali kiba aachie kibao kingine matata alichokiita ‘cheketua’ ndani ya masaa 10 tu kilipata zaidi  ya viewers 42,000 youtube.Jambo ambalo halijawahi kutokea.Mbali na hayo bidii yake imemuweka mjini kwa kupata show nyingi akizipiga kwa mfumo wa live band na kawaida  kisha  akanehemeka tena alivyoungana  na nguli wenzake wa muziki(NEYO) kwenye kipindi cha coke studio.

6.MOHAMMED  DEWJI

Sio mgeni  kwa wapenzi wa kandanda na wafanyabiashara ,kufanya ujasiliamali kumemleta mlangoni mwa familia zetu.Mwaka  2015 Ulikuwa wa fanaka, baada ya kuwa tajiri wa 1500 duniani.akaingia  miongoni mwa matajiri 30 Africa  na wa kwanza  Tanzania .Akimtangulia milionea Rostam Aziz,Said Salim Bakheresa, Murji na Mengi.Mo ni kijana kwa muonekano lakini mzee kwa busara .Anauza, anazalisha na kusambaza bidhaa na huduma zake.Huduma na bidhaa kama vile unga,mafuta,pembejeo na usafirishaji ni mwanya unaomfanya kijana huyu awe bilionea namba moja nchini anayefuatiwa na Rostam.Kujihusisha na kilimo,fedha,mawasiliano pamoja na usimamizi mzuri wa kampuni yao inayoitwa METL.Ilikuwa juhudi nzuri baada ya jarida la masuala ya biashara na ujasiliamali,Forbes.kumtunuku mtanzania huyu heshima ya mtu wa mwaka’’person of the year’’

0 comments:

Popular Posts