Saturday, December 28, 2013


Kompyuta ni nini?, iligunduliwa wapi?, muda gani na nani?. Ni maswali rahisi kuuliza na magumu kujibu.Ugumu unatokana na ukweli kwamba,kompyuta ni chombo cha umeme chenye kufikia, kuchakata, kuonyesha na kutunza habari (data) mbalimbali, kinachoundwa na sehemu nyingi, huku karibu kila sehemu ikiwa na mgunduzi wake anayejitegemea.Bill Gate ,Zuse na Steve Job ni mifano tu ya majina machache yajulikanayo kati ya mengi yalioleta mapinduzi juu ya chombo hiki cha digitali . Urahisi wa kuuliza maswali pia, unasukumwa sana na mchango mkubwa wa hiki kifaa cha umeme, ambacho kiligundulika Marekani mwanzoni mwa miaka ya 1930,ambapo mpaka sasa kimesaidia katika maeneo kadha wa kadha. Sio tu majumbani, mashuleni, maofisini, viwandani lakini pia hata maeneo muhimu ya huduma za kiafya kama  zahanati. Mpaka kufikia maendeleo yanayoonekana leo; kuchapa kazi, kusikiliza muziki, kutazama filamu, kufuatilia habari , kutuma na kupokea maombi ya kazi, elimu kwa njia ya mtanadao (internet) nk , chombo hiki kimepitia kizazi zaidi ya kimoja. Na vifuatavyo ni vizazi vikuu vinee  vya kompyuta.
1.kizazi cha kwanza(1946-1958)





2.kizazi cha pili(1959-1964)




3.kizazi cha tatu(1965-1970)



4.kizazi cha nne(1971mpaka sasa)


Popular Posts