Tuesday, June 7, 2016
Bahati ni ndoa ya vitu viwili: maandalizi  na fursa.Fursa ni msingi wajambo moja,nafasi .Nafasi ni mahusiano ya mambo matatu;nia uwezo na utekelezaji..Palikuepo na mtu mmoja alie amini katika bahati,fursa,nafasi, na utekelezaji .Huyo  mmoja alikuwa kiongozi.Uongozi wake ulijaa utani.Hata moja ya kauli yake pendwa akiwa na raia wake ilikuwa ni hii.''Ndugu wana nchi msidharau vitu vidodo,vitu vidogo vinaumiza,kama mnabisha jaribuni kukalia sindano'' .Halaiki ilikufa kwa mbavu baada ya huu utani.Ukitaka kuamini vitu vidogo ni muhimu vinaendesha dunia,na ukivithamini utafurahia ,hautaumia ungana nami kwenye hizi stori zifuatazo

1.MUHAMMAD ALI
Hakuwahi kujiona kama mpiga ngumi,au bingwa wa makonde kimataifa.Mpaka pale alikumbwa na mkasa mdogo sana.Mohamedi Ali akiwa kijana mdogo miaka kama kumi na kitu ivi.Aliibiwa baiskel anayoipenda .Na akaripoti kwa askari kuwa akimpata mwizi atampiga.Askari alimwambia atamwajibishaje mwizi yule wakati hana uwezo wa kupigana.Basi ikabidi askari amfundishe Mohamedi Ali kuchapa masungwi.Baada ya kuiva hakumtafta mwizi ila akaingia kwenye mashindano ya ngumi 

.
2.MOHAMMED DEWIJ
Safari yake ki siasa ilianza baada ya kuona tukio dogo mkoani mwake Singida.Anasimulia''Nimetoka(Singida mjini) km 6 nakutana na mzee mmoja,kulikuwa kuna maji ya njano chini ,alikuwa na ndoo na sinia,amechuchumaa akiteka maji nakutia ndani ya chombo.Nikamsalimia mzee Shikamoo,unafanya nini hayo maji,akasema haya maji ndio tunakunywa sisi.Sikumwamini hadi pale nimefika  kwake na kuona watoto wakinywa maji yale yale ,mzee akanisihi MO,kwa nini usigombee ubunge?''Sauti ikamgusa Bwana MO.MO akagombea ubunge.MO  akachimba  visima .Wananchi wa Singida  wakanufaika kwa huduma ya maji.

3.JUX
Licha ya kupenda kun'gaa  na  mziki ,Juma jux hakuwahi kufikiri kama ni mwimbaji.Jux alikuwa anafanya hip hop kama vijana wengi wa mtaani. Nini kilimbadilisha? Baada ya Jux kumsindikiza msanii mkubwa studio.anatokewa na jambo dogo linaloleta hamu ya uimbaji..Na hapa  jux mwenyewe anasimulia .''Tulienda studio na Cyril,Cyril alitakiwa kufanya collabo na Makamua .Makamua alikuwa msanii mkubwa.Basi(Cyril) akampigia Makamua,Makamua akadai atakuja, tulichoma sana mahindi pale(tulikaa sana).Kuanzia kama saa moja mpaka saa tano tano.Maneke( producer wa muziki) akawa kaweka ile Beat.Ile beat imewekwa mie nikawa kama naimba tu unajua mzuka wa studio.Maneke akasikia naimba,akasema ebu imba tena,nikaimba.Akanambia mbona unaweza kuimba kwa nini unachana(kurap).Saa izo naogopa kinoma naogopa ile mic sana,sio nilikuwa naogopa kuimba,nilikuwa naogopa kusikiliza nyimbo  yangu mwenyewe kwenye redio,nilikuwa naona aibu sana.Akasema(Maneke) unaweza kuimba jaribu.Nakumbuka ndo mara ya kwanza naingia booth kurekodi''

0 comments:

Popular Posts