Saturday, June 25, 2016
Wakati wengine wakisema ujuzi ni aina ya  kazi au shughuri yenye kufanyika vizuri baada ya  elimu au mafunzo maalumu.Wahenga wanasema  ujuzi hauzeeki.Kwa maana  ni  uwezo unaopatikana kwa mtu hasa akiwa amepita hatua ya  kupokea  maelekezo, na kufanya matendo mengi.Dhana ya ujuzi imekuwa ya kikazi au ki uwezo kulingana na mfumo  anaoaksi mtu..Ukiwa ni  mtumishi wa ofisi rasmi ujuzi wako itakuwa ni utoaji wa huduma inayokubalika hapo kazini kwako.Na endapo umejiajiri au kuajiriwa sekta zisizo rasmi ,ujuzi ni ule uwezo wa kutoa matokeo mazuri ya  chochote  chema unachofanya.Kwa muda mwingi njozi kubwa na fikira pana zimekuwa kama  baba na mama wa ujuzi  katika mazingira yetu.Kujua zaidi kuhusu hilo fuatilia haya maneno 10

1.Kama mmea ustawivyo kwa mbolea na sio jua kali ndivyo Ujuzi umtajirishavyo mtu na sio maneno matupu

2.Ni vyema kila mmoja akawa na kila ujuzi na asiutumie,kuliko kutokuwa na huo ujuzi na ukataka uutumie


3.Kuna sheria za kufuata ili ubahatike,na kila jambo haliundi bahati,kwa waelevu wanatambua ujuzi ni njia mathubuti ya kuwa mtu mwenye bahati


4.Kumpatia mwanao ujuzi ni bora kuliko kumpatia vipande elfumoja vya madini ya dhahabu

5.Elimu huja kwa kujifunza ila ujuzi huja kwa uzoefu.


6.Elimu pekee sio ujuzi, bali ikizidishwa mara elfukumi ndio itakuwa ujuzi

7.Marudio ni mama wa ujuzi

8.Ujuzi ni mshikamano wa  uzoefu,akili na upenzi wa jambo vikiwa pamoja

9.Ujuzi na kujiamini ni jeshi lisilopigwa wala kushindwa


10.Kama huna ujuzi  ipo siku  inakuja kipaji chako kitakwama,kwani ujuzi  ni dhana ya matendo,bidii na shauku ya kutaka uwe bora kila kukicha,

0 comments:

Popular Posts