Wednesday, July 15, 2015
Miaka ya nyuma ilikuwa ni miongoni mwa nyumba nzuri hiyo sehemu. Mmliki wake ni bwana tajiri ambaye kila mmoja alimtazama kwa msaada. Gari ilikuwa ni kivutio cha kila jicho. Ilikuwa ni kama ndoto iliyotimia pale mmliki alivyoongeza gari na nyumba katika idadi ya miliki zake
               Lakini leo mali zote ni chakavu na kwa mujibu wa asili ya vitu, kimoja lazima kichoke ili kingine kije. Nyumba izeeke ili  nyingine ijengwe, gari lichoke ili  jipya linunuliwe. Je unadhani ni vyema kwa mtu wa namna hii , anayeishi na kumiliki hili gari la kale kuitwa mwenda wa zimu hivi sasa, na apelekwe mirembe au sehemu nyingine ya vichaa?
             Sidhani, kwa sababu  hakuna jipya chini ya jua. Nguo yako ya thamani ni dekio kwa mwingine, Salio lako la bank ni kiasi ambacho  mwingine anatoa msaada bure. Mrembo au mtanashati ulinaye leo   kaachwa na mwenzako jana. Hata dada anayeitwa kahaba pale mtaani au kule hotelini siku moja alikuwa bikira. Sasa ya nini majivuno? Maisha ni mafupi kujisikia, kujiona dhidi ya mwenzako. ’’Tungali wakosefu, hakuna mkamilifu’’  . Anasema steve job. Hakuna kitakachotusaidia wala sipendi kuona watu wakijikweza nakujivunia mali, uzuri, akili, kiwango cha elimu, umaarufu na  miliki za dunia. Mungu  anasema ’’Pendaneni na muongeze marafiki’’
                Siku zote kumbuka yule unayemdharau wakati unaelekea  juu ndo yule utakaye mkuta wakati unashuka chini.  Hivyo usiwe ni kisababishi  cha matatizo kwa mwingine. Kama utakuwa kisababishi ,  utakuwa umejipalia kaa la matatizo mwenyewe, na hakika , hao uliowaletea shida watakuwa  sehemu ya matatizo yako siku moja.
                 Mwisho  usisahau kuwa hata matawi ya mgomba  kuna siku huitwa  majani makavu. Hivyo hupaswi kupumbazwa na mali za duniani. Kwani siku moja zitachakaa na kufa.

                Endapo muda utafika ukahisi kulia,  basi niite, siahidi kukufanya ucheke siku hiyo,  lakini tutalia sote. Siku moja ukitaka kukimbilia mbali, usiogope, niite. Nakuahidi nitakimbia pembeni yako. Lakini ikitokea ukaniita na usisikie jibu, huenda  nakuhitaji.  Kwa maana siku  itakuja mmoja wetu hatokuepo tena. Na itakuwa umeshachelewa kusema ‘I care’. Machozi yatakuto lakini   haisaidii, nimeshatangulia mbele za haki. 

0 comments:

Popular Posts