Wednesday, July 22, 2015
Nilipokuwa mtoto kuna kundi kubwa la marafiki walinizunguka. Mmoja wao alijulikana kwa jina la Pola. Mie na rafiki yangu pola tulishirikiana kwa ukaribu juu ya  mambo mawili.  Pola alipenda sinema za Anord Shwarzenegger , mimi  za Jack Chan.  Rafiki angu  asipokwenda kutazama sinema,  alipenda  kucheza mpira. Ambalo ni jambo la pili lililotunganisha . Pola akikusanya makaratasi, mimi nilifuma mpira . Ujamaa wetu uliwakasirisha watoto wengine. Wangefurahi kutuona tukitengana, huku Sinema na kandanda vikiwa kando na maisha yetu  kuliko   mbingu na ardhi.
                Baada ya kuandaa mipira . Ukitukosa uwanjani tupo juu ya miti tukifanya kile tulichoamini ni mazungumzo. Na watoto wengine walikiita kuwa ni mabishano.  Mada kuu ya maneno yetu ilikuwa ni sinema.  Pola alikuwa nimwingi wa furaha tukianza hizi mada. Bilashaka  sikuleta kilio mbele ya macho yake.  Kama yeye ambavyo hakuleta kero usoni mwangu.  Mazungumzo ghafla yalikata tuliposikia filimbi (priiii).  Kwa sababu ilikuwa ni saa ya kandanda, tuliteremka viwanjani tukiungana na watoto wengine wakiwemo maadui.  Kama marafiki wengi  wa utotoni , hatukucheza kandanda katika timu pinzani hata siku moja.  Daima tulikuwa wa timu moja. Kwa kipindi kile mechi hazikufika  mwisho  bila mtoto mmoja kuwa Mohamed ali,  akipiga    ngumi na mwingine  Van damme akipiga mateke. Waliopewa kipondo ni  wachezaji waliokuwa hawana kosa. Katikati ya tifutifu sikupendezwa kuona rafiki angu akipigwa , licha ya umri wa miaka 6 niliokuwa nao, niliamini ningelimtetea Pola (niliyemzidi mwaka mmoja) , kama kuku mdogo  anavyolinda kifaranga wake baada ya mwewe  kukaribia. Sijui nini humwingia pola , kwani wakati wa vurugu jamaa alitumia siraha kama Anord Shwarzenegger (kipenzi chake). Akianza kuwatupia mawe watoto waonevu . Na kuchapa fimbo  zisizo na mpangilio  . Vita ikifikia hapa Sikukimbia, niliwakimbiza,  sikuogopa niliwaogopesha kwa mbio na ujasiri kama Jackie Chan (kipenzi changu).
            Miaka ikaenda sote tukahitimu elimu ya msingi. Nikabahatika kuingia sekondari.  Akafanikiwa kufanya biashara . Miaka ikapita nikachaguliwa form six.  Akabahatika kuwa wakala wa vinywaji vya  kokakola. Miaka ikazidi kusonga. Nikajiunga na Chuo, Yeye akajiunga na miradi mikubwa . Nikasikia Pola kaoa na kufungua biashara  za Tv, DVD , CD na ving’amuzi. Muda ukapita , nikapata ajira ya ualimu, kitengo cha  michezo. Sijasikia chochote toka kwa rafiki yangu . Mtu tuliolindana wakati wa vita ,  leo muda wa amani tunatengana. Mtu aliyenifundisha umoja, ananiacha katika  utengano. Hua sikomei hapo kuwaza. Siku za likizo,  nikifuatilia tamthilia za kikorea ,kimarekani na Uingereza. Hujiuliza mswali yasiyo na majibu.  Tungekuwa na mawasiliano na Pola angempenda mastar kama jumong?, Angemfurahia Will Smith au Harry Potter?  Hakuna wa kujibu haya maswali miongoni mwetu .Sio mimi,wala wewe isipokuwa ni Pola tu.  Kabla na wewe hujampoteza rafiki ako kipenzi ,uliepitia nae hatua nyingi za ukuaji,mateso na raha,njaa na shibe,furaha na huzuni.Napenda ujifunze jinsi urafiki wetu ulivyovunjika.

1.sote tulikuwa busy

2.Mawasiliano yalikuwa magumu tukiamini itakuwa usumbufu mmoja kuwasiliana na mwingine

3.Kisha tulidhani mmoja kati yetu atakuwa wa kwanza  kumtamtafta mwenzake


4.Baada ya kipindi najiuliza kwa nini mimi tu ndo nianzishe mawasailiaano?

5.Hatukuonyeshana upendo tuliounyeshana  thamani zetu
6.Bila mawasiliano ni wazi kuwa kumbukumbu baina yetu ilizaliwa,ikakuwa na mwisho ikafa


7.Hatimaye  tukasauliana hadi leo

0 comments:

Popular Posts