Thursday, November 12, 2015
Japokuwa kuna giza,mwanga,mwezi , jua , bado siku hazifanani.Kama hivyo ndivyo ni kitu gani hasa hufanana?.Siku zote wewe na mimi tumeumbiwa uhitaji.Kwa maana nyingine kila siku tunaongeza idadi ya vitu tunavyopenda,tunavyotaka. Vitu hivi vinaweza kutengwa  katika mipango na katika uchumi. Katika uchumi,mimi napenda  mshahara mkubwa.Bila shaka hupendi kuingiza pato dogo ,unapenda? .Haya mahitaji ya kifedha ni sehemu ndogo kati ya ile kubwa iundayo mahitaji yetu  ya msingi.Yaani malazi,makazi,chakula na mavazi. Katika upande mmoja ukubwa wa mahitaji ya msingi umepanuka kiasi cha kuziba  macho yasione mipango rahisi ya kujikwamua.Kwani tuzibwapo na kipindi cha njaa,usingizi,baridi n.k .Huwa ni ngumu kufikiria mipingo ya muda mrefu au ya kudumu itakayotuepusha  na taabu hizo.Na upande wa pili ni wakati unapokuwa huru husurutishwi na chakula, malazi, makazi, mavazi.Katika hii saa ambapo hatujazibwa na mahitaji tunaweza kuweka malengo, kuoata ndoto, kufanya mipango na kupendekeza mbinu. Hizi harakati na mipangalio   zinavuma tokea ndani ya mioyo yetu zikipita vichwani na kutua akilini. Akili ndio makao makuu ya kila ndoto,mipango na mbinu tulizojiwekea.Kwa kuwa hii sehemu ya ubongo ni mhimu kwetu kama nahodha ndani ya  meli.Basi tunapaswa kuitunza, kuiboresha na kuitumia   kwa uangalifu. Ahsanteh kwa watu  waliotufunza kusoma na kuandika, kwani kwa kitendo chao tumetambua akili hutiwa mwanga. Akili hutolewa gizani. Akili hubadirika. Akili hupokea maarifa kulingana na mambo yanayoizunguka.Na ili tufikie mahitaji ya kifedha na ya msingi tunapaswa kuwa waalimu wa akili zetu, tukizifundisha kulingana na somo zuri linalojiandika katika kuta za familia , mitaa, jamii na maeneo mengine tunayoishi.  Zikiwemo kata, wilaya , mikoa ,nchi ,bara n.k.Bila kuchukua mazuri ya sehemu uliopo akili hizi tunazilisha sumu .Itakayoua 'future' zetu .

0 comments:

Popular Posts