Monday, September 15, 2014
Kuna wakati sisi wananadamu hupoteza mwelekeo  kama boti ndogo inayopigwa na dhoruba kubwa baharini. Ni muda ambao maisha huturushia tope, mawe, miiba na kila aina ya shida, Katika wasaa huu ni kawaida mtu kubaki njia panda, aidha kuendelea ama kutoendelea na jambo fulani alilokusudia hapo mwanzo. Tunapochagua kuendelea, huwa tumecheza karata sahihi. Kwani  mafanikio ni hali inayoanzia chini na baadae kufika juu ya kilele cha maendeleo aliyojipangia mtu mmoja. Watu wengi tumewahi kufanikiwa kwa namna moja ama nyingine. Lakini kadiri tunavyopiga hatua moja mbele , vikwazo navyo hutuvuta kwa hatua mbili  nyuma. Bila shaka umewahi kuona filamu ya nchini Thailand inayoitwa Ong Bak?. Ndani ya sinema hii kadiri  starling anavyopiga maadui ndivyo wanavyozidi kuongezeka. Halikadhalika na maisha ya kawaida, hali huwa hivyo .Jinsi tunavyofanikiwa zaidi na  mambo  huwa mengi zaidi. Hata Nasib au Diamond Platnums, mwanamuziki anayefanya vizuri Afrika mashariki.Hivi sasa ana ziara nyingi za muziki, Kenya,Uganda,Rwanda,Burundi na Ulaya.Hali inayomfanya,ajifunze lugha za kigeni, aandae nyimbo nzuri, afanye mazoezi ya kutosha kuliko wakati hajaanza sanaa ya muziki. Hii inatokana na ukweli kuwa ,mafanikio ni safari moja ambayo huanzisha mambo mengine. Mbali na sanaa hata katika biashara , tajiri Bill Gates ambaye sio  mgeni  masikioni mwetu. Anakiri kuwepo kwa changamoto katika mafanikio licha ya kumiliki na kuendesha miradi mikubwa ulimwenguni. Mtu huyu aliyeanza uwekezaji   akiwa na umri wa miaka tisa  ,kapitia shida ya kimasomo hata safari yake ya elimu  ikayumba kiasi. Lakini leo hii   anatuuzia vifaa,program,computer,smartphones .Bidhaa zinazoundwa na kampuni yake iitwayo  Microsoft.Hivyo   wafanyabiashara ,wasanii na sisi tunakila sababu ya kutokata tamaa na kufanikiwa ili mwisho wa siku tutimize mahitaji  yafuatayo:

1
. 

                               

2.Usalama wa maisha

                                                                                         

3. upendo na mahusiano 

                                                              

.4.Uwezo na heshima.

                                                            

.5. Uhuru katika
















0 comments:

Popular Posts