Sunday, March 16, 2014
Kukua kwa nyanja ya teknolojia duniani imeendana bega kwa bega na kukua kwa matumizi yake  barani afrika. Kwa mapinduzi hayo matatizo makuu ya hili bara sasa yanaelezeka kirahisi kuliko hapo awali. Hapa siongelei tu vita, umaskini,  vifoo na magonjwa kama matatizo  yanayokumba bara hili,  bali pia ukabila, rushwa na mengineyo, kama vizuizi vinavyofunga milango ya kuelekea katika uwanja wa maendeleo. Teknolojia inayojaribu kwa ukaribu kuondoa vizuizi hivyo, imetoa fursa kwa mitandao ya kijamii, blog,  muziki, picha, na filamu kufikisha habari kwa uharaka zaidi. Filamu ndio teknolojia ambayo ni kiini cha maada yangu kwa leo. Hivi sasa makampuni makubwa yanayojihusisha na masuala ya filamu ulimwenguni, Hollywood pictures,  HBO films, Lion Gate Entertainment n.k,  yanawekeza Afrika. Uwekezaji huo unafuatia fursa ya uchumi iliyopo katika bara hili. Mtandao wa Wikipedia unasema '' Afrika ni bara lenye utajiri wa rasili mali lakini wakazi wake ni maskini '' Huu ukweli wa tatizo hili na mengine yaliotajwa hapo juu unadhihirishwa na filamu kumi zifuatazo.
1.SOMETIMES IN APRIL
2.THE DEADLY VOYAGE
3.SARAFINA
4.HOTEL RWANDA
5.ROOTS
6.NERIA
7.THE GODS MUST BE CRAZY
8.THE WHITE MAASAI

9.JERUSALEM
                                      
10.BLOOD DIAMOND

0 comments:

Popular Posts