Waliotembelea
Tafuta
Labels
- afya (10)
- akili (1)
- filamu (4)
- filamu.video (1)
- kipaji (6)
- kompyuta (2)
- kujifunza (17)
- kuona (1)
- maneno (6)
- matokeo (1)
- mazoezi (2)
- mbinu (1)
- michezo (5)
- mitandao ya kijamii (1)
- mwaka (1)
- mziki (1)
- ndoto (2)
- njia (1)
- nukuu (6)
- picha (12)
- picture (10)
- sikiliza (1)
- social ntworks (1)
- tafiti (5)
- teknolojia (5)
- tukio (7)
- usahaulifu (1)
- usingizi (1)
- video (4)
- wasanii (4)
Saturday, February 27, 2016
Kila wakati wengi wetu katika maisha, ni watu wa kujiwekea malengo. Mara nyingi huwa tunaweka malengo haya, kwani kwa kujiwekea malengo hayo ndiyo hutuongeza na kutuhakikishia kule tunakotaka kufika kimafanikio. Kwa kujua hili, karibu kila mtu msaka maendeleo, kwake malengo huwa ni kitu cha lazima sio cha kuuliza tena.
Lakini hata hivyo, pamoja na kujiwekea malengo mazuri, kwa bahati mbaya sana tena wengi wetu huwa bado hatuyafikii malengo hayo. Hapo ndipo maswali mengi sana ya kwanini huanza kuibuka vichwani kwetu? Kama mambo ni hivyo usikate tamaa, Kwa kufatilia makala haya utajifunza juu ya mambo muhimu yatakayokusaidia kufikia malengo yako.
1. Yajue malengo yako vizuri.
Huwezi kufanikiwa kama huyajui malengo yako vizuri. Ni lazima malengo yako yawe ya wazi kwako. Ikiwezekana yaandike vizuri kwenye karatasi nayaweke sehemu inayoonekana. Kwa mafano kama lengo lako ni kufanya biashara ya ‘stationary’ liandike lengo hilo mahali na lionekane. Kama pia lengo lako ni kufungua duka weka wazi lengo lako kwa kuliandika.
Watu wengi mara nyingi wanashindwa kufikia malengo yao kwa sababu malengo yao yanakuwa sio wazi sana. Siku zote mawazo yetu ya ndani hutusaidia kufikia malengo yetu, kama malengo hayo yana eleweka. Kinyume cha hapo, utakaa sana kusubiri malengo yatimie lakini wapi. Hivyo siri ya kufikia mafanikio jitahidi kuweka malengo yako wazi.
![]() |
| HAKUNA CHA KUKUZUIA KWENYE MAFANIKIO UKIAMUA. |
2. Jitoe kikamilifu.
Siri ya mafanikio ni kujitoa kikimalifu kwa kile unachokifanya. Hata malengo yako ambayo umeshajiwekea na yako wazi ili kuweza kuyafikia ni lazima ufanye juu chini kujitoa kikamilifu na wala sio nusunusu. Ikiwa utakuwa unayaendea malengo yako, huku ukiwa hujaamua kujitoa kikamilifu tambua ikatokea umeshindwa usishangae hapo kwa hilo.
Kwa kuwa unanajua malengo yako nini, kama kuna kazi unatakiwa kuifanya ifanye kweli kwa nguvu zako zote bila kuchoka. Weka juhudi na maarifa yako yote na kuhakikisha unajitoa kweli. mafanikio yako hayatakuja kirahisi eti kwa kufanya kazi kilegevu. Jitoe kwa kupiga kazi kwelikweli mpaka kieleweke.
3. Kamilisha majukumu yako kila siku.
Unaweza ukawa unayajua malengo yako na umejitoa kikamilifu, lakini huwezi kuyafikia malengo yako kama kila wakti unakuwa hukamilishi zile kazi zinazotakiwa kukusaidi kuyafikia malengo yako. Hapa sasa ndipo unapotakiwa kujilazimisha na kuhakikisha kila jukumu ulilonalo unalikamilisha kwa siku husika.
Kwa mfano kama wewe ni mfnyabiashra ulitakiwa kupga mahesabu Fulani ya kukusidia, fanya hivyo bila kuacha. Halikadhalika akama wewe ni mwandishi na umejipangia kuandika kurasa mbili kwa siku, pia fanya hivyo bila kuacha wala kuahirisha. Kwa kukamilisha majukumu yako kila siku itakusaidia kufikia malengo yako kuliko ambavyo ungefanya mambo nusunusu.
4. Yagawanye malengo yako.
Malengo yoyote ulinayo yanaweza kufikika. Haijalishi malengo hayo ni makubwa kivipi lakini uwezo wa kuyafanikisha upo, ikiwa tu lakini utafuata hatua za kuyakamilisha malengo hayo. Pengine unajiuliza kivipi au nitawezaje kuyakamilisha malengo yangu makubwa? Ni rahisi tu na hata wewe unaweza.
Kulielewa hilo vizuri ngoja nikupe kisa kimoja moja ambacho kinaelezea siku moja fisi mkubwa alimkuta fisi mdogo akimla tembo. Fisi Yule alivyoona vile alicheka sana na kumuuliza utamaliza lini? Fisi Yule mdogo alimwambia nitamla kidogo kidogo mpaka ataisha. Kwa kutumia mfano huo hivyo, ndivyo unavyotakiwa na wewe kufanya kwa malengo yako makubwa. Unajiona una malengo mkubwa yagawe vipande vipande mpaka uyafikie..
5. Tafuta msaada.
Ni rahisi kuyafikia malengo yako, kama utatafuta msaada wa kukusaidia kuyafikia malengo hayo. Acha kung’ang’ania kukamilisha malengo hayo ukiwa peke yake. Yaangalie malengo yako yana husu nini kisha baada ya hapo jiulize je, ni mtu gani au watu gani ambao wanaweza kunisaidia kukamilisha malengo haya.
Kwa kujua watu ambao watakusaidia kukamilisha malengo yako itakusaidia sana kushirikiana nao kwa ukamilifu na kwa ubora wa hali ya juu hadi kufikia mafanikio yako. Tambua na elewa sio kwa sababu malengo ni yako, hivyo unatakiwa kuyakamilisha mwenyewe, hapana. Tafuta kile unachokosa, kisha omba msaada.
6. Kuwa chanya wakati wote.
Kuna wakati tunapokuwa tunajiwekea malengo huwa tunakutana na changamoto nyingi sana ambazo zinatukatisha tamaa. Sasa hali hii inapokutokea ni vyema ukajitahidi ukawa chanya wakati wote. Acha kukataa wala kujiona hufai, endelea kusonga mbele kati kati ya changamoto hizo ulizonazo wewe.
Kuwa chanya wakati unatafuta mafanikio inalipa sana. Tuchukulie kwa mfano unafanya biashara halafu ukapata hasara, hapo unafanyaje? Utaacha au itakuaje? Jibu ni kuendelea na safari ya mafanikio kwa kutambua kwamba hiyo nayo ni hatua ya mafanikio pia. Ndiyo maana tunasema ni muhimu na lazima kuwa chanya ili kuyafikia mafanikio yako.
7. Kuwa tayari kuyapitia malengo yako kila wakati.
Pamoja na kwamba umejwekea malengo vizuri, umejitoa kabisa kwenye malengo hayo, lakini hutakiwi kusahau kabisa kuyapitia malengo yako. Ni muhimu kuyapitia tena na tena malengo kwa kutambua wapi ulipofikia, nini kinachokukwamisha na ufanye nini ili uweze kusogea hapo ulipo kwa kasi zaidi.
Watu wengi wenye mafanikio wanayapitia malengo yao. Wanapita malengo yao asubuhi, wanapitia malengo yao mchana, wanapitia malengo yao jioni. Picha kamili ya malengo yao inakuwa ipo kichwani mwao tayari. Hiki ndicho kitu ambacho unatakiwa ukifanye hata wewe. Pitia malengo yako kila wakati ili yaumbieke vizuri na itakusaidia kuyakamilisha.
8. Jifunze kufurahia mafanikio kila hatua unayopitia.
Pamoja na kujiwekea malengo yetu makubwa, lakini kumbuka kuna yale malengo yetu madogo madogo ambayo huwa tunayashinda. Inapotokea umefanisha jambo fulani, hata kama kwako ni dogo ni vyema ukajifunza kulifurahia. Furahia mafanikio yako siku hadi siku kwa jinsi unavyoyapata. Hiyo itakupa nguvu ya kufanikisha mambo mengine.
Kama kweli una nia njema ya kufikia mafanikio makubwa, basi hayo mambo ni ya msingi sana katika kukusaidia kufikia malengo yako makubwa uliyojiwekea. Jukumu lako kubwa ni kuhakikisha unayaweka kwenye vitendo mambo hayo. Na kwa kufanya hivyo basi utaweza kufikia malengo yako na kutakuwa hakuna wa kukuzuia.
Nikutakie siku njema na endelea kujifunza kupitia DIRA YA MAFANIKIO kila wakati. Usikose kuwaalika wengine waweze kujifunza kupitia makala tunazozitoa hapa.
Ni wako rafiki katika kusaka mafanikio ya kweli,
Imani Ngwangwalu,
Simu; 0713 04 80 35,
E-mail, dirayamafanikio@gmail.com
Siku zote maisha ya mwanadamu yanaaongozwa na miiko au kanuni. Ni miiko hiyohiyo ambayo ilianza toka zamani lakini ambayo lengo lake kubwa lilikuwa ni kutuelekeza mambo yapi tufanye na mambo yapi tusiyafanye katika maisha ili tufanikiwe. Wale waliofuta miiko hiyo ni kweli walifanikiwa, na wale walioikiuka walishindwa katika maisha yao kwa naman fulani.
Kwa bahati mbaya au nzuri miiko au kanuni hizo zinafanya kazi katika maisha yetu mpaka sasa. Wengi huwa hawajui katika hili, lakini upo umuhimu mkubwa sana wa kuijua na kuifuata hiyo miiko au kanuni na kuamua kuachana na mambo ambayo yanawezayakawa kizuizi kwetu cha mafanikio. Katika makala hii tutaangalia mambo ambayo ni lazima tuyaache ili tufanikiwe.
Yafuatayo Ni Mambo Unayotakiwa Kuyaacha katika Maisha Yako.
1. Acha kuruhusu makosa madogo madogo, hatimaye yakawa makosa makubwa na yakakuzuia kufanikiwa .
2. Acha kukimbia changamoto zinazokukabili, pambana nazo mpaka ufanikiwe na kufikia mafanikio makubwa katika maisha yako.
3. Acha kusahau kule ulikotokea. Yapo mambo ya kujifunza kutokana na kule tulikotoka.
4. Acha siku zote kujijengea tabia ya kulalamika. Kama utaebndelea kufanya hivyo utashindwa katika mambo yako mengi sana .
5. Acha kamini kuwa utashindwa kwa kile unachokifanya. Kila mara na kila wakati amini wewe ni mshindi wa maisha yako.
6. Acha kuruhusu pesa ikakutawala. Matokeo yake itawale pesa na hiyo itakusaidia kufikia uhuru wa kipesa.
7. Acha Kurusu hofu ikakutawala maisha yako. Kwa kadri utakavyozidi kuwa na hofu ndivyo ambavyo maisha yako yatazidi kuwa mgumu. Hiyo yote ni kwa sababu utashindwa kufanya mambo yako kwa sababu ya hofu ulizonazo.
8. Acha kuanzisha biashara, huku ukiwa unategemea bahati ndiyo ufanikie. Ondoa mawazo ya bahati na fanya biashara yako kwa kujimini, utafanikiwa.
9. Acha kujijengea tabia ya kufurahia, hasa ple mambo yaw engine yaopkuwa mabaya. Badala yake wape moyo na kuwafariji.
10. Acha kuogopa kusonga mbele, hata kama kuna wakati unahisi kama vile unakwama. Wewe endelea kukazana na kusonga mbele na mwisho wa siku utafanikiwa.....
Makala kwa msaada wa mwungwanablogspot.com
Kwa bahati mbaya au nzuri miiko au kanuni hizo zinafanya kazi katika maisha yetu mpaka sasa. Wengi huwa hawajui katika hili, lakini upo umuhimu mkubwa sana wa kuijua na kuifuata hiyo miiko au kanuni na kuamua kuachana na mambo ambayo yanawezayakawa kizuizi kwetu cha mafanikio. Katika makala hii tutaangalia mambo ambayo ni lazima tuyaache ili tufanikiwe.
Yafuatayo Ni Mambo Unayotakiwa Kuyaacha katika Maisha Yako.
1. Acha kuruhusu makosa madogo madogo, hatimaye yakawa makosa makubwa na yakakuzuia kufanikiwa .
2. Acha kukimbia changamoto zinazokukabili, pambana nazo mpaka ufanikiwe na kufikia mafanikio makubwa katika maisha yako.
3. Acha kusahau kule ulikotokea. Yapo mambo ya kujifunza kutokana na kule tulikotoka.
4. Acha siku zote kujijengea tabia ya kulalamika. Kama utaebndelea kufanya hivyo utashindwa katika mambo yako mengi sana .
5. Acha kamini kuwa utashindwa kwa kile unachokifanya. Kila mara na kila wakati amini wewe ni mshindi wa maisha yako.
6. Acha kuruhusu pesa ikakutawala. Matokeo yake itawale pesa na hiyo itakusaidia kufikia uhuru wa kipesa.
7. Acha Kurusu hofu ikakutawala maisha yako. Kwa kadri utakavyozidi kuwa na hofu ndivyo ambavyo maisha yako yatazidi kuwa mgumu. Hiyo yote ni kwa sababu utashindwa kufanya mambo yako kwa sababu ya hofu ulizonazo.
8. Acha kuanzisha biashara, huku ukiwa unategemea bahati ndiyo ufanikie. Ondoa mawazo ya bahati na fanya biashara yako kwa kujimini, utafanikiwa.
9. Acha kujijengea tabia ya kufurahia, hasa ple mambo yaw engine yaopkuwa mabaya. Badala yake wape moyo na kuwafariji.
10. Acha kuogopa kusonga mbele, hata kama kuna wakati unahisi kama vile unakwama. Wewe endelea kukazana na kusonga mbele na mwisho wa siku utafanikiwa.....
Makala kwa msaada wa mwungwanablogspot.com
Wednesday, January 27, 2016
2.Millard Afrael Ayo.

Mwandishi wa habari , aliowahi kupewa tuzo ya mtangazaji bora wa
kiume anayependwa(2014), mwaka mmoja mbele, 2015, taaluma ya habari inamfanya atabasamu
kwa kufanikisha ufunguzi wa Kituo
binafsi cha redio alichokiita TZA.Ndani ya mwaka huo tabasamu inaendelea kushamiri
baada ya Millard Ayo. Com Kutunukiwa tuzo ya Website/blog inayopendwa Tanzania.
Katika tuzo za watu zilizofanyika Hyatt Legency, Dar es salaam. Ushindi huo
unakuja kwa kuziacha tovuti nyingine
kama; issamichuzi.blogspot.com, jamii forum. Com, dj chokamusic. Com. 2015 pia ilistawisha
mbegu za tabasamu jingine pale huyu mtu wa nguvu anayesihi watu wakae karibu na
speaker za redio, kuanzisha
Application(Millard Ayo app) inayopatikana Google play na play store.App
Inayosaidia wapenzi wa Habari anazotoa wasipitwe na chochote kile. Lakini tujiulize, Millard Afrael Ayo ni mtu
wa namna gani?...Huyu ni miongoni mwa Watanzania wabunifu, anaejua kutumia muda, wazo, pesa, na watu kwa dhamira ya kutimiza ndoto zake. Ndani ya
muda wa miaka 11 (toka 2004 alipoanza kazi ya utangazaji had 2015 mwaka wa
neema) Millard katoka ngazi ya ufukara mpaka Ile ya maisha bora. Wakati miaka
11 sio muda kidogo kwa hayo mabadiliko makubwa aliofanya. Huo muda umezaa
mawazo na mipango yakinifu ikiwemo; kufanya kazi na vituo bora vya matangazo
Tanzania (redio one /itv, clouds fm ) .Muda umezaa fikra za kuboresha
production, show na matangazo ya hewani yatakayofanyika chini ya Radio
yake.TZA. Mpango ambao ni moja ya malengo
matano ya siri, anayosema" muda ukiwa tayari nitaweka wazi
" Kuhusu pesa je?, Ujue sio rahisi
kila mtu kutunza sh. mia na hatimae siku moja utimize kiasi cha million moja.
Uwezo wa namna hii unapatikana ndani ya kingo za nafsi chache zilizokusudia
kweli . Millard Ayo anasemaje "kwa malimbikizo ya mshahara
amepata nguvu ya kununua vifaa vyote vya TZA. "kununua camera na mic za
kisasa zinazotumika na Millard Ayo TV. Matumizi ambayo sio tu yanaimarisha
anachokipenda (kazi) bali pia humsogeza karibu na watu. Mpaka mwaka 2015
Millard Ayo ni kipenzi cha watu. Anayeshika namba Tatu (3)Kwa kuwa mtanzania
maarufu aliyefikisha idadi ya followers
million moja na zaidi huko mitandaoni(instagram)
. Huku namba moja ikishikwa na Mwanamuziki Abdul Nasib maarufu "Diamond
Plutnumz" Namba mbili inakamatwa na aliyekuwa mwandani wake Diamond na
miss Tanzania 2007, Wema Abraham Sepetu. Watu ni kiungo kikuu cha mafanikio ya
Millard. Bila pongezi, maoni, chuki, upendo na ushirikiano wao, zile ndoto,
fedha, muda, na bidii pekee visingemfikisha hapo alipo leo. Kila lakheri
millard
Tuesday, January 12, 2016
5.Samia Suluhu Hassani.

Mwana mama aliyegawanya miaka 55 katika familia, elimu na siasa. Akiwa
anazaliwa visiwani Zanzibar mwaka 1960, Bi Samia anapata bahati ya mtende.Kuwa makamu Wa rais na mwanamke wa
kwanza kushika wazifa huo. Baada ya miaka 54 ya uhuru wa Tanzania .Hata hivyo
nafasi kama hiyo pamoja na vyeo vikubwa anavyovipata mwaka 2015 sio jambo geni
kwa Samia. Kwani baada ya kufanya kazi na N.g.os, Shirika la Chakula duniani na
ubunge , marais wawili kwa awamu tofauti waliwahi kumteua mara tatu mwanaharakati huyo kuwa waziri. Mwaka
2000 Rais wa Zanzibar,Amani Karume
alimteua Suluhu kuwa waziri wa Leba, jinsia na watoto ikifuatiwa na mwaka 2005
waziri wa utalii. Rais wa awamu ya nne, Dk Jakaya Mrisho Kikwete pia alimteua
awe waziri wa mambo ya muungano. Ukiwa unataka kujua nini kipo nyuma ya pazia,
Bi Suluhu hasiti kwa hilo, anatoa siri kwa maneno yasiozidi manne (4),kwamba
amefika hapo kutokana na’’ ueledi na umakini katika kila jambo analolifanya’’.Ni
kweli asemacho kwa sababu katikati ya miaka ya 80 (1986)Samia Hasani Suluhu
alihitimu elimu ya mambo ya utawala chuoni Mzumbe. Mwishoni mwa hiyo miaka ya
80 (1989) Aliongeza elimu yake katika moja ya chuo huko Pakistan na mwanzoni
mwa miaka ya 90(1991)Bi Suluhu alihitimu elimu nyingine ya uongozi Hyderabad,
India, na mapema mwaka 1994 alihitimu elimu ya mambo ya uchumi huko Uingereza katika chuo cha Manchester na
katika mwaka Wa neema, 2015, Samia alipata ujuzi mpya wa uchumi na maendeleo ya
jamii katika chuo cha kimarekani kinachoitwa Southern New Hampshire. Lakini
pamoja na yote hayo Bi Samia ni mke, na mama Wa watoto wanne. Tena anayelea na
kupenda familia yake vizuri.Kwa historia hii bi Samia ni miongoni mwa wanawake
maarufu na wenye ushawishi nchini.Kama Asha Rose Migiro, Janeth Magufuli, Anna
Mwighwira, Salima Kikwete nikitaja kwa uchache .
4.Mbwana Ally Samatta.
Wazungu wana msemo usemao "umri
ni namba" . Kwa maana idadi ya Miaka tuliyonayo sio kikwazo cha kutokuwa
watu tunaojikusudia kuwa. Hakika unaweza fanya chochote katika umri wowote.
Haya ndio maelezo yanayomvisha kilemba
bwana Samata. Mchezaji aliyezliwa 1992 na mwaka 2015 kugeuka
dhahabu pale alipo pewa tuzo ya ufungaji
bora wa ligi za mabingwa afrika. Ikifuatiwa na kuwania tuzo ya mchezaji bora Wa
afrika anayecheza ligi za ndani. Ni mswahili wa kwanza kuleta mchango kwa timu
akiiwezesha timu yake kutwaa kombe la
mabingwa wa afrika 2015 . Pengine unajiuliza Samata ni nani?. Huyu ni mtanzania
mwenye umri wa miaka 23 anayechezea timu ya mpira Wa miguu nchini Kongo
inayoitwaTP Mazembe . Mnamo mwaka 2011 Samata aliuzwa kwa dau nono la dola za
kimarekani mil 100(shilingi mil 150 za
kipind kile )na Simba Sport Club.Huku yeye
akipewa sh. Mil 50. Mpk mwaka wa neema, 2015, Mbwana Samatta tayari anamiliki
pesa, mali, majumba matano na magari ya kifahali manee;Range Rover yenye thamani ya mil 80 na
Chrysler crossfire ya mil 50. Tukisahau habari ya utajiri , Samata anamudu vyema
nafasi ya ushambuliaji akiwa uwanjani . Kwa mwaka 2015 tu ameifungia tp mazembe
goli saba, kitu kilichomfanya awindwe na ligi za ulaya kw tiketi ya timu za
ubelgiji .Kwa nafasi hiyo Samata ataingia kwenye orodha ya watanzania wachache waliowahi
kuchezea ligi za nje ya bara la Afrika.Tukikumbuka kuwa wachezaji wengine
waliofikia hiyo hatua ni pamoja na Haruna Moshi "Bobani", Athuman
Machupa waliokuwa Sweden, Renatus .Njohole, Uswizi, Mwinyi Kazimoto, Qatar .Henry Joseph,
Norway na Danny Mrwanda aliyekuwa Vietnam.Tunakutakia mafanikio mema Samata.
3..Amri Athuman 'King
majuto'.
Kama sio kipofu utakubali mwaka 2015 ulikuwa mzuri kwa gwiji wa
vimbwanga nchini, mzee king majuto. Kwani tumeshuhudia siku moja baada ya
kuachia filamu mpya ya Shikamoo Mzee . Tenda za pesa zilimfuata mzee wa watu.
Akifanya matangazo ya bidhaa tofauti tofauti zaid ya muigizaji mwingine. Hivyo kutawala sura za magazeti, vipindi vya
TV na redio . Ni miaka miwili imepita (2013-2015) tangu Majuto atangazwe kama
muigizaji aliyelipwa vizuri na kampun ya steps production. Akipokea kiasi cha
sh. Mil 20 kwa mwezi, kwenye mahojiano aliofanya na kipindi cha Amplifya
kinachorushwa na Miradi Ayo. Habari
inayoashiria kuwa, huenda na mwaka 2015, Majuto akawa mbele kwa kupiga mpunga
mnono. Kwa sababu muigizaji huyo wa comedy kanyakua tuzo ya mchekeshaji bora Wa
mwaka , pale viwanja vya Nyerere Dar es salaam.Akiwabwaga akina Jangala, Salma Jabu"Nisha" ambao ni wachekeshaji wazuri nchini. Ni zaidi ya
miaka 50 tangu Majuto aanze kufanya kazi
za uchekeshaji . Anasema "Mpaka sasa nimecheza movie zaidi ya 600 tokanimeanza kuigiza za kushirikishwa na zangu"Miongoni mwa filamu zilizomuweka sokoni ni Daladala, Mtu
mzima ovyo, Naenda kwa Mwanangu, Back from New York na Shikamoo Mzee. Mbali na
yote mvunja mbavu huyu ni baba Wa familia ya watoto tisa na amefanikiwa kujenga nyumba tatu, kuanzisha
shamba kubwa la kilimo .kusomesha wanae, kwenda Makka na kununua magari matano.
Kwa maendeleo haya ,mzee ni changamoto kubwa kwa wachekeshaji wanao chipukia na
wale wakongwe kama Onyango, Mzee Jangala, Senga , Pembe, Brother K, Nisha na
wengine.
Monday, January 4, 2016
Huku mwaka 2015 unamalizika.Shangwe za kukaribisha mwaka
mwingine zinamiminika.Wengi tukiwa ni
washangiliaji ,tunasahau kuuliza swali alililojiuliza,rais wetu katika sherehe
za uhuru,kwa nini tunasherekea?.Kutoka kwenye swali tutanweza kupata jibu kwa kutumia
watu wachache kwa namna moja ama nyingine wanastahili kusherekea .Wale ambao
neema iliwangukia ,walichosema kilitimia,walichofanya kilifanikiwa hata mengi
waliokusudia yalionekana.Kitu kibaya kuhusu idada ya watu hawa ni kuwa japo
wengi walifanikiwa tutatazama wachache
tu wasiopungua 10.Lakini Jambo zuri ,hawa sio wageni ni wale tuliozoea kuwaona
kwenye michezo, dini, burudani, siasa, biashara, elimu, filamu na sekta nyinginezo. Athari za hawa wachachehazi
kuvuma kwenye tv, redio, magazeti, internet tu. Bali hata wewe walikuhusu
kiganjani mwako pale ulipounga bundle ili usipitwe na habari zao.Maisha
yao,mafanikio yao na harakati zao.Unataka
kuwafahamukwa undani ?, tazama mfululizo ujao.
10.JOHN JOSEPH POMBE MAGUFULI.
Ni mmoja wa watu waliopewa majina mengi mwaka
2015.Tingatinga,mzee wa msimamo,mchapa kazi,jembe n.k. Majina yote yalifutia ubora
wake katika wizara alizokwisha shika ikiwemo
ya ujenzi,uvuvi,ardhi. kisha kuchukua fomu ya kugombea uraisi wa jamhuri ya
Muungano wa Tanzania.Jasho likamvuja kwani hakuwa peke ake katika kinyang’anyiro
ni watu makumi walichuana.Hatimaye katika chama chake akatoka yeye .Hali
iliomkutanisha na wapinzani wapya toka vyama vingine.Hapakuwa na njia fupi ya
maisha kwa Bwana Magufuli.Zaidi ya kutia mafuta kwenye gari,weka funguo na
kuzunguka nchi nzima kuwakumbusha watanzania kwa nini yeye anafaa kuchukua ridhaa ya
kuwaongoza.Mnamo Octoba 25,2015 alipaki gari na kungoja wananchi wafanye yao. Tahere
5 November 2015 mizunguko na hapa kazi tu zikazaa matunda akahapishwa kama rais wa awamu ya tano ya jumhuri wa mungano wa Tanzania.
9.Edward Lowassa.
Mwaka umekuwa wa neema kwa kile kinachosemekana kama kavunja
record ya ushawishi kwa umma.Dhidi yamtazamo wao juu ya vyama pinzani, awali
vyama pinzani havikuwa na nguvu kubwa kama alioleta bwana huyu.Kwa mara ya kwanza kanda ya ziwa
walipiga deki rami .Kaskazini walichora ngozi rangi ya chama chake,magharibi walipunga
mikono hewani kama feni,kusini walifurika viwanjani haijawahi tokea.Vitendo hivi
vilifuatia ishara ya mabadiliko na kutokata tamaa.Alioioonyesha mgombea huyu.Kwani
baada ya kutoridhishwa na mchakato wa kusaka wagaombea katika chama
tawala.Alisimama wima katika chama pinzani na hivyo akafanikiwa kuimarisha
ngombe ya upinzani kuliko ilivyowahi kuwa hapo mwanzo.Kwa kuongezaa idadi ya wabunge kutoka upinzani na kufungua pazia jipya la ushindani wa kisiasa.Jina lake
halitosahaulika katika historia za hili taifa.
8.Diamond Platnums
Kama mafanikio yangekuwa yanapimwa na wingi wa majina.Diamond
Plutnums angekuwa trionea.Ukiachilia
mbali jina la Naseeb Abdul anajiita Chibwa,
Dangote,rais wa wasafi,Mr ngololo,baba tifa,na sasa anajifananisha na mfalme wa
chi kavu katika wanyama kwa kujiita ‘simba’.Yote tisa kumi huyu kijana kagusa
mafanikio ya maana 2015.Baada ya kuingia mgogoro wa mashabiki ( team diamond vs team kiba )Kijana wa majina mengi alipata muda
mgumu kama sio uchungu wa mafanikiao.hali iliyomfanya atuache tumeshika vichwa kwa mshangao alipofanya kazi na wasanii wakubwa akiwemo,Neyo,Usher,A.K.A,Mafikizolo,Mr fleva.Wengi
wao wakiwa ni wa afrika magharibi afrika ya kusini na Marekani. Mwaka ukapendeza zaidi
alivyotwaa tuzo ya Best Africa Act, BestWorld wide act,Best collaboration,Video bora
ya mwaka n.k.Huku hizi tuzo zikiwa ni za ndani ya Tanzania,ndani ya afrika na Nje
ya afrika.Dangote ama simba kama anavyojiita kakunja mkeka kwa kufungua studio
inayosimamia kazi za wasanii wengine .Akiwemo Hermonize anaetamba na kibao cha
Aiyola.Kama haitoshi ndani ya mwaka huo huo alipata binti yake wa kwanza
waliomuita TIFA.
7.Alikiba
Huku akiwa ni baba wa watoto watatu; wa kike wawili na wa
kiume mmoja.Alikiba amevuna zaidi ya alichokipanda mwaka 2015.Kufuatia kibao
kimoja kuleta tuzo tano .Ambazo ni za ubora katika uimbaji,utumbuizaji
na utungaji. Sio jambo la kitoto eti.Baada ya kuachia single ya Mwana.Kiba alizimisha
kelele zote redioni na ile iliyobaki ni mwana dar es salaam.Kumaanisha ilistahili
kuwa nyimbo bora ya mwaka graduation za
vijijini hadi mijini,zilitumia ‘mwana’ kama nyimbo kuu katika sherehe zao.Ni
kazi hii ilipelekea kuzuka kwa ugomvi wa
team mtandaoni .Baadhi ya watu waliamini king kiba yupo juu zaidi ya Diamond na
wengine hawakuamini hiyvo.Unajua nini kilichofuata?Hii nyimbo bora ya afro pop
ilimfanya Ali kiba aachie kibao kingine matata alichokiita ‘cheketua’ ndani ya
masaa 10 tu kilipata zaidi ya viewers 42,000
youtube.Jambo ambalo halijawahi kutokea.Mbali na hayo bidii yake imemuweka
mjini kwa kupata show nyingi akizipiga kwa mfumo wa live band na kawaida kisha akanehemeka tena alivyoungana na nguli wenzake wa muziki(NEYO) kwenye
kipindi cha coke studio.
6.MOHAMMED DEWJI
Sio mgeni kwa wapenzi
wa kandanda na wafanyabiashara ,kufanya ujasiliamali kumemleta mlangoni mwa familia
zetu.Mwaka 2015 Ulikuwa wa fanaka, baada
ya kuwa tajiri wa 1500 duniani.akaingia miongoni mwa matajiri 30 Africa na wa kwanza Tanzania .Akimtangulia milionea Rostam Aziz,Said Salim Bakheresa,
Murji na Mengi.Mo ni kijana kwa muonekano lakini mzee kwa busara .Anauza, anazalisha
na kusambaza bidhaa na huduma zake.Huduma na bidhaa kama vile unga,mafuta,pembejeo
na usafirishaji ni mwanya unaomfanya kijana huyu awe bilionea namba moja
nchini anayefuatiwa na Rostam.Kujihusisha na kilimo,fedha,mawasiliano pamoja na usimamizi mzuri wa
kampuni yao inayoitwa METL.Ilikuwa juhudi nzuri baada ya jarida la masuala ya
biashara na ujasiliamali,Forbes.kumtunuku mtanzania huyu heshima ya mtu wa
mwaka’’person of the year’’
Nikiwa
mwanza mwaka 2004 nilikuwa mwanafunzi aliyependa somo la historia. Moja ya mada
niliyopenda ni colonialism. Mada ilinifunza , miongoni mwa athari walioleta
wakoloni ni kurudisha nyuma maendeleo ya
Tanzania. Huku maeneo ya kusini mwa nchi yakitajwa kuwa duni zaidi ya kwingine. Nikasoma pia Mtwara na
lindi ni mfano wa maeneo hayo. Lakini cha ajabu mwaka 2011 nikiwa mwaka wa
kwanza katika chuo kimoja cha hapa mtwara niliona mambo ni tofauti .Mtwara ya kipindi hiki inapiga hatua kuliko
picha niliojengewa na ile mada. Kuna ulinzi wa mali na usalama wa afya. Kuna
shule, vyuo na taasisi za elimu. Kuna viwanja vya michezo, vikundi vya sanaa na
mahala pa burudani.Kuna viwanja vya ndege,bandari na stand za bus. Kufikia
mwaka 2014, niliona Viwanda vya cement, vyombo vya habari, na rasli mali za
mafuta na gesi, huku fukwe za mtwara
mjini zikiwa na hotel nzuri na maandhari safi. Nakumbuka katika kufurahia mazingira haya nilikuwa napiga zoezi kila
alfajiri. Kisa kilichopelekea nipoteze simu.Pale uchovu uliponifanya nisahau hicho
chombo cha mawasiliano juu ya canteen ya chuo. Mungu ni mkubwa simu
ilipatikana siku kumi baadae.(Niliipata
vipi hiyo ni stori ya siku nyingine) na mwishoni mwa mwaka 2015 nikirudi chuoni kwa ajili ya kumsapoti mdogo wangu aliehitimu
chuo .Nilipata bahati kutembelea fukwe
tofauti tofauti. Msanga mkuu, Veta, makonde, bandari ya zamani . Ambapo
sikusita kuogelea baharini , wakati
nafanya hivyo mwenzangu ambaye ni mgeni hapa aliniuliza, ’’ni mambo gani ya
kuzingatia katika fukwe za mtwara?’’ Nikiwa majini nilianza kwa kumwambia . ’’Yapo
mengi ya kuzingatia ila nitaanza na haya’
’
’
1.URUMBA (wadudu).
Ukiwa unaogelea kuwa makini na wadudu walio na miiba iliyowazunguka mwili
mzima. Wakiwa katika rangi nyeusi na sura ya duara mara nyingi wadudu hawa
hujisogeza karibu na miamba . Na kwa kuwa miiba yake ni nchi moja na zaidi na
upana wa sindano ya mkono , ukimkanyaga mmoja mwiba unavunjikia mwilini mwako. Idadi
ya miiba iliyokuingia inasababisha
mwasho mkali, maumivu na baadae homa. Wenyeji wa pwani wanashauri
ukipatwa na tatizo hili(urumba) , mapema chukua
mafuta ya taa tia mahala miiba imeikuingia. Baada ya siku mbili mpaka
tatu utapona
.
2.ASKARI. Uwapo
katika fukwe za shangani, kama makonde na veta askari wa dolia ni wengi. Hivi
vikosi haviruhusu raia abaki maeneo haya muda wote. Ikifika saa 12 :30 jioni , watu
hufukuzwa. Saa 1 giza likiwa kubwa askari polisi hukamata watu . Raia hufikishwa
kituoni. Wakipewa adhabu ya kutotii sheria za fukwe.
3.MV
MAFANIKIO. Ni feli inayobeba magari ,mizigo na watu wanaotoka na kuelekea msanga mkuu.Baada
ya fukwe za veta na makonde kuwa na mashabiki wengi. Fukwe za kivuko cha Msanga
mkuu ndio imekuwa habari ya mjini miongoni mwa watu. Hakuna namna ya kuenjoy
pwani hii kama hujui utaratibu wa Mv mafanikio. Huanza asubu sana kukamilisha
safari yake. Muda wa mwisho ni jioni saa
12. Kabla ya kuondoka hupiga honii. Ukifika chomboni mkononi uwe na ticket . Kuna
nauli ya mtu, gari na mizigo mikubwa. Mpaka mwaka 2014 disemba nauli ya mtu
mzima ilikuwa ni sh. 300.
4.KUPWAA NA
KUJAA. Raha ya fukwe ipo machoni mwa mtazamaji. Hivyo ni msingi kutambua wewe
unapenda msimu wa bahari ikiwa ina maji au ikiwa haina. Kuna nyakati bahari hupwaa,
hapa ni muda maji yapo mbali sana na fukwe. Ukitazama utaona maadhari kama ya
jangwa, miamba vigumu kupata maji ya shingo wala ugoko. Na wakati imejaa huwa
ni wiki nzuri kwa waogeleaji. Ukitokea
pwani utaona fukwe zinatenganishwa na mawimbi ya amaji. Ukiyafuata yatakuanzia kweye
ugoko ,kiuno , shingo mpaka mwili mzima utabebwa .
5.SIKU KUU. Ni
siku njema kwa mambo mengi zikiwemo fukwe. Wakati wa chrismas, mwaka mpya, Idd n.k Fukwe za mtwara hufurika watu
zaidi ya mchanga. Siku kuu wanavyuo, watoto wa mjini, raia wa kawaida kutoka
kona zote za mtwara hujumuika hapa. Hizi siku mhimu huambatana na matukio mhimu
kama upigaji picha , biashara za vyakula na vinywaji. Huku mziki , nyama choma
na burudani zikiwa pale fukwe ya
makonde.
6.USAFIRI. Ni
mhimu kujua utatokaje eneo moja hadi jingine. Kama ilivyo lazima kujua
utafikaje ufukweni endapo upo nyumbani. sio vigumu , kama wewe unaishi mtwara
au ni mgeni nabado haumiliki chombo cha usafiri. Kwanza kuna usafiri wa aina
nne. Taxi,Bajaj,Bodaboda na baiskel. Pili kila usafiri una gharama yake. Wakati
taxi au gari za kukodi zikiongoza kwa gharama, bajaji na boda boda(pikipiki)
huwa ni nafuu ikitegemea na idadi yenu. Ukiwa ni mtu wa mzoezi baiskel zipo
unachotakiwa ni kukodi na kueleza unachukua kwa masaa mangapi. Mwisho kabisa
kwa wewe unaeishi mbali na hizi fukwe ni mhimu kutambua kuwa usafiri
unapatikana.
Subscribe to:
Posts
(Atom)
Popular Posts
-
Hekima huja sio tu kwa kuona matendo yasiyo na busara ndani yake. Bali hekima hujipambanua katika umbo la uelewa na ufahamu ,pale tu uwapo ...
-
Ibrahim na Neema huvutiwa sana na mitindo.Ndoto yao juu ya tasinia hii ilianza kwa kupenda haiba na unadhifu.Wakiwa ni vijana wasio na aj...
-
Katika moja ya kipindi cha luninga niliona mabishano baina ya watu watatu, hawa jamaa walitofautiana katika misamiati miwili. Msamiati wa...
-
Kwa mujibu wa mtandao mashuhuri duniani unaoeleza maada na mambo mbalimbali , Wikipedia the free encyclopedia . Kusoma ni mchakato wa ku...
-
Wakati mwili wa binadamu ni kama jumba ,akili huwa kama funguo ikusababishayo kufik ia kila chumba cha maamuzi. Maamuzi hufikiwa baada ya ...
-
Ni miongoni mwa maswali ya msingi sana hapa duniani ,mtu kuhoji,kudadisi na kujiuliza maisha ni nini?Kwa kuwa maisha yanagusa kila mwanad...
-
Wakati sauti hujaribu kudokeza baadhi ya tabia za ndani, mavazi hodokeza mawazo, fikra na hisia za mtu .Hii hutokana na muonekano unao...
-
Matokeo ya kidato cha nne ya mwaka 2013 yanatoka tar 21 februari 2014 , huku mabadiliko kadhaa yakijitokeza. Mabadiliko haya ni pamoja na...
-
Kupokea maarifa na elimu kutoka chanzo kimoja,mtu mmoja hadi hatua ya kutafasiriwa na akili ya mtu mwingine,haina budi kuja kwa njia ya kuji...
-
Kombe la dunia(2014) ilikua ni michuano ya kabumbu,ambayo ilianza tar 12 mwezi june na kuisha 13 july, huku ilikonga mioyo ya wanamichezo ...
