Tuesday, January 17, 2017
Waswahili husema ‘siku hazilingani’ ni kweli. Leo ukifurahi, kesho utaduwaa. Na richa ya juhudi kubwa inayopimwa na jasho zito , majanga hayaishi kutuandama. Wakati mwingine chozi la uchungu linapita  . Jicho linazibwa  usione  fursa hata moja mbele yako. Na ghafra ukishtuka umeshajikwaa kwenye kisiki cha umaskini. Hapo utajiuliza maisha yana maana kweli?Na hakutakuwa na jibu.Maana matatizo yanakuwasha  kuliko upupu.Shida zinashamili kama magugu.Sikio halisikii habari njema tena.Ukifungulia redio  ikutie moyo ,majonzi ndo kwanza yanakithiri.  Matangazo  ni ya nafasi za shule zaidi ya nafasi za ajira, ni ya vyuo zaidi ya mahala pa kazi. Katika juhudi za kuepuka huo mfadhaiko unageuza jicho mpaka kulia kwako ambako kuna ‘tv’.Ni kipindi cha habari , bila kuamini mboni zako unajionea viongozi wakitumbuliwa Ili hali mifumo ikiachwa.Hasa elimu. Kabla hujaongeza sauti ya luninga , simu yako inayokaribia kukata ‘charge’sababu ya shida za umeme ,inaita.Ni ndugu analalamika maisha magumu pesa hakuna..Mkopeshe japo "jero" . Bila mafanikio ya kumweleza jinsi ulivyopigika,simu yake inakata hana voucher.Kufumba na kufumbua,,umeme umekata na simu inazima kumbe hata bila ya voucher kuisha bado mawasiliano yangekata tu.Ukiwa kwenye joto kali baada ya umeme kukata unabakia kutazama sura yako kwenye  televisheni iliyozima. Punde mwenyekiti wa wapangaji anakumbusha ni zamu yako kulipa LUKU,mzunguko ushakufikia. Ungali bado katika hali hii ya sintofahamu baada ya simu kumaliza moto, redio kupoteza matumaini  tv kuzima na sasa kulipa LUKU.Anakuja baba mwenye nyumba kudai chake. Utatamani kusikia maneno ya wasanii hawa.
1.’’Acha kulia ni shida za dunia ebu tulia’’Jose chamillioni
2.’’Haya yote ni maisha ipo siku yatakwisha leo mmoja anangaika mambo yamebadilika’’P funk
3. ’’Kama unapata moja kwa nini usipate na mia,hiyo inawezekana kwa wote waliona nia’’Prof jay
4.’’usikubali wakakushinda,Kwani wao waweze wananini na sisi tushindwe tuna nini’’Juma nature
5. ’’Wakati wako ndio leo kutimiza malengo yako nakusihi anza sasa jishughurishe utapata’’Ben Paul.
6.’’Na ugumu wote wa maisha shida zote za  kutaabisha usikate tama usivunije moyo’’Kara Jeremiah

Monday, January 16, 2017

Kuna milango mitano ya watu kuwa matajiri wakubwa ambayo mabilionea duniani wanatokea:


1. WATAALAMU WANAOLIPWA VIZURI
Kundi la kwanza ni wanataaluma wanaolipwa vizuri (well paid professionals) kama wanasheria wazuri, madaktari bingwa na wahandisi. Wengi waliofanikiwa katika kundi hili wanajua jinsi ya kuweka akiba na kuwekeza akiba zao kwenye maeneo yenye marejesho mazuri. Mabilionea wanaotokea kundi hili ni asilimi 10 tu ya mabilionea wote.


Image result for stephen hawking
2. WAKURUGENZI WA MAKAMPUNI MAKUBWA
Kundi lingine la mabilionea ni wakurugenzi wanaolipwa vizuri na makampuni makubwa (well paid executives). Hawa ni asilimia 10 ya mabilionea wote pia. Mara nyingi hawa huwa wametoka na kampuni mbali na wamekua nayo wakipandishwa cheo baada ya cheo mpaka kufikia hatua ya juu. Mara nyingi, watu wachache katika kundi hili huwa na uwezo mkubwa wa kuzishikilia fedha zao na kutozifuja na hiyo huwafikisha kwenye ubilionea.

Image result for executives who are billionaires
3. MAAFISA MAUZO
Kundi la tatu ni maafisa mauzo au mameneja wa idara za mauzo. Hawa huwa ni takriban asilimia 5 ya mabilionea wote na kinachowafanya wawe mabilionea ni kwa sababu ya nafasi ya kupata kamisheni kutokana na mauzo wanayoyafanya. Wengi wao huwa ni waajiriwa wa makampuni ambayo wamekuwa wakifanya nayo kazi kwa muda mrefu na kuzifahamu vizuri na baadaye kuja kuwa na milango mingi ya mafanikio.
Image result for top salesman

4. WATU WENYE VIPAJI MAALUM
Kundi la nne ni watu wenye vipaji maalumu kama wanamichezo, wanamuziki, watunzi wa filamu na vitabu na kadhalika. Hawa ni wachache sana 1%, lakini huonekana wengi sana kwa sababu ya kelele zinazoendana na umaarufu wao. 

Image result
5. WAJASIRIAMALI
Hili ndiyo kundi kubwa kuliko mengine yote, asilimia 74% ya mabilionea wote ni wajasiriamali. Hii inamaanisha kuwa nafasi ya mtu yeyote kuwa bilionea ni kubwa zaidi kupitia ujasiriamali kuliko kitu kingine chochote. 
Image result for reginald mengi biography
Sunday, January 1, 2017
     Mwaka mpya n kitu kizuri kutokea,hatuna budi kusherekea.Ila lazima tujue tunasherekea nini?.Taasisi za dini zinatufundisha kushukuru kwa kila jambo,ni sawa.Ila tushukuru tukisherekea kwa kiasi.By the way kuna sababu nyingi za kusherekea.Ikiwemo kuwa mzima,kutimiza malengo n.k.Hapa sitaongelea kwa kina habari ya sherehe na kusherekea .Nipo kwa ajili ya kushare mawazo ya watu wengine juu ya mwaka mpya.Na hapa chini wanasema

1.     Mwaka mpya ni kama kitabu cha kurasa tupu kinachosubiri kuandikwa.Tunaweza kukiandika kwa kuanza leo kujiwekea malengo.
Image result for book with empty pages
2.     Mwaka huu maombi yako yasikike  ndoto zote zitimie,jasho lote lizae .
Image result for christian muslim prayer
3.     Mwaka huu jiamini tena na upate kila unachostahili
Related image
4.     Ingawa hakuna anayeweza kurudi nyuma atengeneze mwanzo mzuri,sote tuna nafasi ya kuanza sasa na kufanya mwisho mzuri.

5.     Mwanzo wa mwaka ni mwanzo wa kufanya kila unachokusudia.

6.     Mwanzo wa mwaka ni kama karatasi nzuri isiyo na kitu.inayosubiri wewe kuiambia dunia hadithi yako
Image result for empty page
7.     Tukubali,tukatae mwaka mpya utaleta changamoto mpya,lakini tupende ,tusipende utakuja na fursa nyingi pia.
Image result for opportunity
8.     Ishi chini ya mwenye ndoto na mtendaji,anayeamini na kutafakari, lakini zaidi ya yote ishi na yule anayeona uweza ndani yako hata kama wewe  hujioni.
Image result for best company to hang with

9.     Haimanishi unatoka wapi cha msingi ni unaelekea wapi
1o.     .Kunywa kiasi,pangilia,tafta marafiki,punguza unene,kuwa chanya na tumia pesa kwa uangalifu.
Image result for no drinking

Wednesday, December 21, 2016
Toka ulimwengu ugeuke kijiji.Habari husambaa haraka kuliko  moto wa petrol.Hauhitaji nguvu kufuatilia mitindo,teknolojia,siasa na michezo. Siku izi kila mmoja ni model,IT,photographer ,kiongozi,na mchambuzi.Kwa sababu taarifa  zinapatikana kila mahali.Kuanzia facebook ,Whats apps.Instagram na kwingineko.Ukaribu wa dunia na mitandao ya kijamii ni chachu ya uelevu..Utitiri wa vyanzo vya habari kupitia simu za mikononi  laptop na tablets zilizounganishwa na internet ni shina la  wasomi na kundi  la waelevu  tulionao.Kuendena na kasi ya mabadiliko yanayotokea ughaibuni kote inategemea unamiliki kifaa gani? Ukinunua tecno,huwawei,Samsung,iphone au ipad yenye 3G hakika wewe umeukata.Kwani internet ni mama wa habari ,aliyezaa mitandao ya kijamii .Inayokupatia kile unachotaka .Familia hii inakuwa kila siku kwa maana kunazaliwa mitandao mipya na followers wapya. Je unajua list ya social networks bora 2016?.
1.Facebook
Image result for facebook

2.Youtube
Image result for youtube

3.Reddit
Image result for reddit

4.Tweeter
Image result for twitter

5.Pinterest
Image result for pinterest

6.Instagram













7.Tumblr
Image result for tumblr logo
8.Linked In
Image result for linkedin

9.Yahoo Answers
Image result for yahoo answers
10.Yelp
Image result for yelp
Monday, December 12, 2016
Haya ni mazungumzo ya babu wa kisasa  na mjukuu .Mjukuu aliuliza swali kwa babu.''Babu kuishi ni nini?'' Babu akamjibu ''Kuishi ni  safari  baina ya  pande kuu mbili, upande wa kuzaliwa na upande wa kifo''.Mjukuu kwa mshangao akauliza tena''kuzaliwa na kifo?.Babu kwa hali ya utulivu akajibu,ndio mjukuu wangu.Kila mmoja imemlazimu kuzaliwa na kufa.Kuja na kuondoka.Mjukuu akadakia''kwa hiyo babu,nani anajua nitakufa lini?''Babu akasogeza kiti vyema na kumueleza mjukuu.'' Tofauti na mungu ni wachache wanaoweza kusema utakufa lini.Nao ni watabiri au watu waliopewa nguvu ya kuona hatima ya maisha yako''.''Kwani wewe huwezi?'' Mjukuu akang'ang'aniza huku akimukazia macho babu yake.Babu kwa kutambua tabia ya ung'ang'anizi wa mjukuu,alianza kwa kusema.''Chozi ni kimiminika cha matukio mawili.furaha na huzuni.Mtu analia machozi, huzuni ikimshika. Anaomboleza  kwa sababu uwepo wako ulimpa mengi ya kujifunza .Mfululizo wa uhai wako ni somo linalojiandika kila siku vichwani mwa watu….Wachache watasahau habari ya kifo chako ndani ya muda mfupi.Lakini wengi watasherekea na wewe muda wa uhai wako. Ukizaliwa wanadamu wanasherekea. Mama ,kaka na ''washikaji''  watakuenzi wakiweka siku maalumu kwa ajili yako , ‘’birthday’’. Kila mwaka ifikapo tarehe ya siku uliozaliwa ‘maswaiba’ watakuambia ‘’Happy birthday’’ ’’Happy born day’’ na maneno mengi ya lugha maridhawa.Ili wakonge mtima wako na chozi la furaha likutoke.Kana kwamba hiyo haitoshi.Wataenda mbali zaidi  wakiandika’’Uishi miaka buku( 1000.). Kuna jambo hawatalitambua ,nalo ni mwisho wa maisha yako. Nawe mjukuu wangu  utakufa baada tu ya kupita duara nne za kuishi.

DUARA LA KWANZA UTAKUWA NA  NGUVU UNA MUDA UNA IDEA HUNA PESA.
Wewe kama inge ukiingia duniani utakuwa na nguvu mikononi  na miguuni.Kwa nguvu ulizonazo. Itakuja siku utazunguka huku na huko.Muda  mwingi ukijaribu sehemu kubwa ya  mawazo yako.Ufanye nini uache nini.Mambo mengi yanakusibu.Karibu yote yanawezekana.Ila mchawi atakuwa mtaji.Tatizo litakuwa ni pesa. Kwa mazingira yako hiki kitakuwa kipindi  kuanzia kuzaliwa hadi umri wa miaka 29
Image result for no money

DUARA LA PILI UTAKUWA NA NGUVU  UNA PESA UNA IDEA HUNA MUDA
Kama vile simba jike, nguvu zako zitakuwa maradufu mwilini. Ukifanya shughuri ngumu kushinda hapo mwanzo.Kwa kila kazi ujira utaingia. Akaunti ya idea itasoma vizuri, utakuwa na utulivu kwenye jambo moja. Kwani muda wa majaribio ulishapita.Itafika kipindi utaitwa aidha Boss, mwalimu, dokta, mfanyabiashara n,k.Uwapo njiani kuelekea ofisini au kurudi nyumbani. Utaelewa maana halisi ya bango lililonyuma ya lori, daladala, hiace, bus au boda boda linalosomeka’’Tatizo ni muda’’Kwa sababu kipindi hiki utakuwa na wingi wa majukumu.Muda wako utakakuwa mfinyu.Utafanya kazi, zaidi ya kupumzika.Hapo utakuwa una umri wa miaka 30-39
Image result for no time
.
DUARA LA TATU UTAKUWA NA KIKOMO CHA NGUVU UNA MUDA UNA PESA HUNA IDEA.
Kuna nyakati zinakuja nguvu ya mwili itafika kikomo.Haitaongezeka kabisa.Utastafishwa kazi au utafikiria kustaafu mwenyewe.Utendaji wako utakuwa ule wa ‘’one step at a time’’Kazi nyingi hazitafanyinyika mara moja.Hakuna namna, utakabidhi vijana. Wenye nguvu zaidi yako.Muda mwingi utazunguka huku na kule.Kuanzia Milima mirefu ( Kilimanjaro, Evaristi) mbuga za wanyama (Serengeti ,Amazoni ) ,   majangwani  (Dubai,Cairo) hadi fukwe za bahari (Mombasa, Brazil).Wakati unakula jasho na meema ya ulimwengu.Fedha itakuwa inaongezeka kila kukicha.Na utabaini kuwa una kosa kitu.Nacho  ni kimoja tu.idea. una wingi wa pesa ,una  uchache wa idea.Utaanzisha mashindano ya kutafuta idea.Watu kadhaa wataulizwa ''kwa kiwango cha pesa flani unaweza kufanya nini?''.Hapa mjukuu utakuwa una umri kati ya miaka 40-70.

Image result for no idea

DUARA LA NNE UTAKUWA NA IDEA UNA PESA UNA MUDA HUNA NGUVU.

Baada ya mashindano na  matembezi ya huku na kule na kumuona huyu na yule..Jua litazama.Utakuwa ni mchovu.Kwani kichwa kitakuwa na mengi.Utapumzika na kisha kuchuuja idea ulizopata.Utaitwa mshauri wakampuni mwenye busara.   Atoae mawazo madogo, yanayotengeneza faida kubwa ya pesa.Watumishi wako wataamini wewe si wa kawaida  .Kwa namna unavyotatua shida ngumu na kuleta maslahi  kirahisi. .Jina lako litabebwa na heshima uliojenga.Nafasi yako italeta marafiki wapya.Makanisa, Misikiti ,Shule ,Vyama na taasisi nyingi zitakupenda. Hautosita kuzisaidia pale unapoweza.Wajukuu na watu watakupenda. Shida ni moja  tu,nguvu..Nguvu itapungua kila mwaka, utakuwa taratibu sana.Hautokuwa mtu wa safari za mara kwa mara.Siku za usoni utashindwa kufanya vidogo ulivyoweza mwanzoni. Hutofunga tai, viatu, vishikizo wala kuvaa mkanda..Hautoweza kujinywesha maji wala kujilisha chakula.Ukiona hizi dalili mjukuu wangu zinakupata,tambua mwisho wa uhai wako umefika.Hapa utakuwa na umri wa miaka 71 na kuendelea

Image result for tired black old man

Popular Posts