Tuesday, July 7, 2015
Mabadiliko ni kama maji huweza kuchukua umbo la sura yeyote. Na huweza kufuata uelekeo mmoja au zaidi. Ukitazama  sura ya teknolojia iliopo leo utabaini hii sio taswira iliokuepo jana, yaani miaka 20 iliyopita. Mageuzi haya yanatokea huku wagunduzi kuntu wakiwa ni miongoni mwa watu adimu katika hiki kipindi. Richa ya kukosekana kwa wagunduzi nguri wakiwemo; Isack Newton, Pythogrus, Edson Thomas,  kati ya miaka  1995 hadi 2015 . Kuna upepo wa mabadiliko unaoletwa na waboreshaji wanaofuata misingi ya hao wagunduzi kuntu. Wagunduzi dhahiri, wangunduzi halisi , wagunduzi waliovuma miaka yote.  Ndani ya hiki kipindi cha miongo miwili ( miaka 20 ).  Kuna wabunifu wanaochipukia na kumiminika kama utitiri.  Hawa ndio shina linaloshikilia urahisi wa maisha na urahisi wa mawasiliano katika dunia ya leo. Hali inayopelekea mambo yaliokuwa hayawezekani miaka 20 iliyopita kufanikiwa. Na hapa ni baadhi ya hayo mambo

1.IMO,SKYPE












Kitendo cha kuonana ana kwa ana baina ya watu wawili walio katika sehemu tofauti za mchi , ilikuwa ni kitendawili katika niaka ya 90.  Ahsanteh kwa teknolojia ya imo na skype kwa kuleta nyuso na sauti za watu karibu.  Wapendanao waliokuwa wametenganishwa na umbali,  masomo,  kazi na majukumu  ,sasa wanafursa ya kusalimiana na kutazamana kwa ukaribu kama pua na mdomo.

2.WHATSAPP
Ilikuwa ni rahisi  kwa mganga wa kienyeji wakati ule. Kuendesha majadiliano na watu anaowaona yeye tu , kama hiyo haitoshi aliweza kusema kitakachojiri  duniani kabla ya mimi na wewe kutambua lolote.Baada ya simu kuingia kila mtu kapatiwa uwezo huo. Tena kama ina whats app ndio mtajadiliana hadithi zote kuanzia; siasa , katiba, tamaduni , uongozi, ajira, michezo, burudani ,utabiri wa hali ya hewa,kubet n.k .Vyanzo vya hizi habari kwa mwaka 2015 sio tena ‘mafundi’ au waganga wa kienyeji  pekee bali ni rafiki zako,wanafunzi wenzako,wafanyakazi na jamaa uliohifadhi namba zao katika simu ya kiganjani mwako. Kwa kutumiana jumbe za sauti,picha na video  Whats app hukupa maarifa pamoja  na taarifa za hayo matukio mbalimbali


3.YOUTUBE
 1995,Televisheni ilikuwa ni kila kitu juu ya masuala ya video. Kuona ‘kichupa’ au video mpya ya msanii unayempenda ilikupasa utege jicho kwa luninga. Ukikosa tukio kubwa katika taarifa ya habari ulitakiwa kuwa mvumilivu hadi taarifa irudiwe, vinginevyo ungoje  kipindi maalumu au mwisho wa wiki. Hali sio hiyo tena miaka ya kuanzia 2005, na Shukrani za kipekee ziendee  youtube kwa kutupa uhondo wa video tulizokosa, tuzitakazo katika muda wowote, mahali popote na kwa mtu yeyote.  matukio makubwayaliokupita au uliyoyakosa katika tv utayapa hapa.

4.SHAZAM
Unakumbuka enzi hizo ukisikia mziki mzuri redioni, unatamani mtangazaji ataje jina la huo wimbo?. Ama unapita mahala kuna mdundo wa nyibo za ughaibuni,zinakugusa moyoni lakini hujui msanii wala jina la wimbo? Hii shida sasa imefika mwisho.Mwaka 2015 Kazi imerahisishwa sana .  Ni vyepesi zaidi ya kumsukuma mlevi. Kwa kutumia shazam unaelekeza tu simu au komputa karibu na mdundo wa nyimbo,  na ndani ya sekunde umeshapata jina la msanii na nyimbo 
.
5.GOOGLE EARTH

Zamani ilikuwa ni ngumu kufika pointi moja  bila kuwa na mwenyeji, bila kuuliza ama kupanda chombo cha usafiri. 2015 unaweza kutembea dunia nzima bila kukwea pipa, kuchukuwa treni, kupita na meli wala kupanda basi. Ikiwa una google earth na mji una ramani mtandaoni  , utaelekezwa  njia za kupita kwa mguu, kwa gari hadi sehemu za kuvinjari, hotel, supermarket, beach  na kona za afya ;  hospitali, zahanati, na maduka ya madawa baridi. Google hawatoi tu ramani bali pia vituo mhimu unavyotaka kujua
 .
6.FACEBOOK
Karibu kila mmoja ana damu ya uandishi. kubali!, kataa!. Kwa maana anafurahi kushirikisha jamii dhidi ya mafanikio  ,mipango, ndoto,  huku akitia moyo marafiki na kuomba msaada wa maombi kwa ndugu hata pongezi kuto kwa jamaa . Mmoja yupo huru kutoa mawazo na hisia zake mbele ya wengine. Hii sehemu ya maisha ya mtu mmoja dhidi ya wengine hufanyika kwa maandishi yanayoambatanishwa na picha nzuri ya mhusika. Kama ishara ya kujuza jamii nini kinachoendelea upande wake. Endapo hujui ninachojaribu kuelezea hapa,  nakusihi jiunge na facebook, ukashuhudie jinsi uhuru wa kujieleza ‘freedom of expression’ inavyotendewa haki. Ikiwa una kumbukumbu nzuri, pengine umebahatika kuishi na wezee katika miaka ya 90. Utaona  bibi na babu zetu hawakufaidi dhana nzima ya uhuru wa mawasiliano.Ukilinganisha na FACEBOOK

7.TWITTER
Nakumbuka nilisoma kitabu kimoja zamani kidogo, ambacho kilielezea namna wafalme walivyokuwa wakituma jumbe ulimenguni.Kitendo kilifanya na mtu mwenye mbio sana aliagizwa kupeleka nyaraka katika himaya nyingine , na hiyo himaya  iliteua mjumbe wao mwenye kasi sana mpaka falme ya tatu .Ambayo pia ilieneza habari katika falme ya nne. Mtindo uliendelea  mpaka falme ya sita ,saba hadi  ya mwisho.Na baada ya miaka habari ilienea ulimenguni kote. Stori ya hiki kitabu chenye maisha ya zamani, kinafunua muongozo wa teknolojia ya twitter . Kitu ambacho twitter hufanya japo ni ni ndani ya sekunde,au dakika tu. Ni kueneza habari kwa haraka, Hivyo miomgoni mwa matumizi mengi ya tweeter,  dunia nzima hujua nini kimejiri. Kwa kuendeleza habari husika iwe ni Alshabab, Sunami, mapinduzi, ongezeko la joto n.k  .Ndani ya masaa taarifa itakuwa imefika uchina, Marekani, uingereza, Brazil, Australia na Tanzania . Dunia nzima hupelekewa taarifa kwa kufanya swala endeleve linaloitwa ‘retweete’

8.INSTAGRAM
Wakati sote tunaamini bank ni nyumba ya pesa, ghala ni nyumba ya mazao na msitu ni sehemu ya miti.  Basi instagram ni nyumba au sehemu ya picha. Zamani kuona picha ya msanii, mtu maarufu au kiongozi mkubwa ilikuwa nadra,  mpaka utafte  gazeti au kutembelea maneo ya kazi zao. Ahsanteh Instagram kutuletea pozi, dizaini, mbwembwe na matukio mengi ya watu hawa katika mfumo wa picha.

9.EBAY, AMAZON, KUPATANA



Unakumbuka wakati unauza bidhaa na hakuna mteja? .Unataka kununua mali hakuna hakuna muuzaji?. Ilikuwa ni zama ya miaka ya 90. Kuanzia mwaka 2015 Ebay, Amazoni, Kupatana.com ( Tanzania )  inatoa uhuru wa kuuza na kununua bidhaa yoyote mtandaoni. Hapa utapata nyumba, mavazi,  usafiri, vitabu, mashamba n.k

10.HULKSHARE, SOUND CLOUD

Sauti ina thamani yake na ili hii haiba idhihirike haina budi kukusanywa pamoja katika mfumo flani. Miaka ya 90,   miziki ilitunzwa vyema katika santuri, kanda , cd na baadae miaka ya 2000 , zikaingia flash. Lakini ukisahau mbinu hizi . Hulkshare na sound clound ni mapinduzi makubwa miongoni mwa mengi katika kutunza, kusikiliza na kupakuwa au ku ’download’ sauti, nyimbo, midundo, mziki unayoipenda.


Monday, June 15, 2015
A.Y au Ambwene Yessaya ni mwanamziki mkongwe anayetetemesha bongo fleva likija swala la mafanikio.Msanii huyu kajiwekea mizizi mirefu hadi nje ya mipaka ya Tanzania.Akianzia na kundi la East Coast Army ,A.Y anapata umarufu kwa uwezo wake wa kurap vizuri,na baadae anajitegemea huku akifanyakazi na wasanii wakubwa kama Sean Kingstone,Romeo,n,k. Na hapa anakuuliza ''Ni kitu gani huwafanya watu wawe na mafanikio?'' kisha anasema ''Leo namalizia kukupa siri 10 ambazo ukizizingatia utabadilika na kuwa mtu ambaye kila mmoja atakuwa akikuangalia kama mfano.''Ambwene Yessaya(2015).

1. siri ya kwanza:UNAVYOFIKIRIA NDIO KILA KITU
Siku zote kuwa na mawazo chanya. Fikiria mafanikio na sio kushindwa. Kuwa makini na mazingira hasi. Siri hii inafaa kuwa ya muhimu zaidi kwenye orodha ya mambo ntakayokuambia.Imani kuwa unaweza kuyafikia malengo yako inapaswa kuwa imara. Pindi unapojiambia mwenyewe kuwa ‘siwezi..’, basi hautaweza. Mambo chanya huwatokea watu chanya.

2. siri ya pili:KUWA MSTAHIMILIVE NA JITUME
Mafanikio ni kama marathon na sio mbio fupi. Kamwe usikate tamaa. Ukimuuliza kila mtu aliyefanikiwa leo au ukisoma historia za watu wenye uwezo mkubwa kifedha na maisha kwa jumla, utagundua kuwa walijituma sana hadi kufika hapo walipo.
Hakuna njia ya mkato katika kufikia kilele cha mafanikio. Lakini kama unafanya kitu ambacho unakipenda – basi sioni hata kama unaweza kukiita ni kazi!

3. siri ya tatu: KUWA TOFAUTI
Kama utafanya kitu kile kile kama wengine wanavyofanya, ni ngumu sana kuwa na mafanikio. Ni muhimu sana kupata kitu tofauti na kukomaa nacho.Hivi ndivyo itakuwa rahisi watu kukuona na wewe kupata unachotaka. Iwe ni fedha, uhusiano wenye maana, mtu tofauti huvutia wote.

4.  siri ya nne: ANZA SASA
Watu wengi hushindwa kuufikia uwezo wao wa juu kabisa kwasababu huwa hawaanzi kufanya kitu. Siku zote wamekuwa ni watu wa kujiandaa, kujipanga na kusubiri muda mzuri wa kuanza.Kama ningeendelea kusubiri hadi leo pengine nisingekuwa na mafanikio haya niliyonayo. Kama nisingechukua hatua za kusafiri na kwenda Kenya, Uganda na kwingineko, nisingekuwa msanii ninayejulikana kama hivi sasa.Kama nisingekuwa mjasiri na kuamua mwenyewe kubadilisha video zangu na kuzigharamikia, naamini nisingewapa moyo wasanii wenzangu wanaowekeza sasa kwenye kazi zao. Kujiongeza ni neno sahihi hapa! Kama unataka kujenga nyumba, ni ngumu kupata kwa mfano shilingi milioni 50 za hapo hapo ili uanze. Anza kwa hicho ulichonacho mkononi na utashangaa kuwa una nyumba tayari! Si unaujua ule usemi kuwa hata mbuyu ulianza kama mchicha? 
Je unasubiri kitu fulani kabla ya kuanza? Ni kitu gani kibaya sana kinaweza kutokea kama ukianza sasa? Kama wewe ni mtu ambaye umekuwa ukisubiri muda muafaka ufike, acha kusoma post hii na anza kufanya kile umekuwa ukitaka kufanya. Post hii itaendelea kuwepo hapa hapa ukirejea tena. Ha ha ha ha! Tukutane kwenye siri ya tano! 

5. siri ya tano:ISHI KWA KILE ULICHONACHO/UNACHOINGIZA
Watu wenye uwezo huepuka sana kutumia hovyo fedha zao. Lakini cha ajabu, miongoni mwa wengi wenye kipato cha chini huishi maisha yaliyo juu ya uwezo wao. Hutumia zaidi kuliko kile wanachoingiza na hivyo kujikuta na madeni mengi. Kama wewe ni mtu wa aina hii, punguza sasa ili kujiwekea akiba kwaajili yako na familia yako.

6.  siri ya sita:KUJIWEKEA TABIA NJEMA ZA KILA SIKU
Tabia njema ni msingi wa kutengeneza utajiri. Tofauti kati ya watu waliofanikiwa na wale ambao hawajafanikiwa ipo kwenye tabia zao za kila siku. Watu waliofanikiwa wana tabia njema ama ili kueleweka zaidi niyaite mazoea mengi mazuri kuliko yale mabaya.
Kama unaelewa kuwa tabia zako mbaya zinakukwamisha kuwa tajiri, utambuzi huo utakuwa ni hatua ya kwanza katika kuboresha mienendo yako.
Kwenye kitabu chake kiitwacho ‘Rich Habits - The Daily Success Habits of Wealthy Individuals’, Tom Corley anakupa ushauri wa kuchukua karatasi na kuorodhesha tabia zako mbaya kwenye column moja na kisha zibadilishe kila moja kwenye column nyingi kwaajili ya tabia njema. Mfano ni kama huu:
Tabia mbaya
Ninaangalia mno TV Sikumbuki majina ya watu
Ninajizuia mwenyewe hadi kuwa na saa moja tu ya kuangalia TV
Ninaandika majina ya watu na kuyakumbuka
Watu wengi waliofanikiwa huyazungumzia mafanikio yao kwa kuwaongelea watu fulani waliowasaidia kuwaongoza kufika hapo walipo. Washauri (mentor) wamepitia njia unayohangaika nayo sasa na wanaweza kukuongoza kufika uendako wa haraka zaidi kuliko kama ukienda mwenyewe.
Kama unataka kuwa na afya njema, utahitaji kwenda kwa mshauri ambaye tayari ana afya. Kama unataka kuwa tajiri, basi pia mtafute mtu ambaye ni tajiri akupe baadhi ya siri zake.

Tabia njema
Kisha kwa siku 30, fuata maelekezo ya kwenye orodha ya tabia zako njema. Utashangaa namna utakavyofanikiwa.

7. siri ya saba:USIOGOPE KUOMBA MSAADA
Watu waliofanikiwa hawana kasumba ya kufa na tai shingoni kama mjerumani. Walipokumbana na vikwazo walitafuta msaada wa hali na mali kwa wale waliokuwa na nafasi kuwazidi.
Kila mmoja na ule uthubutu wa kufanya mambo yake mwenyewe, ni nzuri katika upande mmoja lakini pia mbaya katika upande mwingine.
Kama kuna mtu unamfahamu ni mjuzi kwenye sekta fulani na unahisi anaweza kukusaidia katika mradi wako sio mbaya ukimshirikisha katika ushauri.

8. siri ya nane:NI MARUFUKU KUKATA TAMAA
Safari ya kuyafikia mafanikio sio rahisi hata kidogo. Kama unataka kuwa na maisha mazuri kwa njia halali, ni lazima utakutana na vikwazo vingi ambavyo kama hutokuwa jasiri, ni rahisi sana kuanguka.Usikate tamaa pale mambo yanapokuwa magumu. Watu waliofanikiwa huvumilia. Hubadilisha njia. Hujaribu kitu kipya. Husonga mbele. Wanaweza kubadilisha muelekeo lakini huendelea mbele.

9. siri ya tisa:TAFUTA USHAURI KWA WATU WALIOFANIKIWA
Watu wengi waliofanikiwa huyazungumzia mafanikio yao kwa kuwaongelea watu fulani waliowasaidia kuwaongoza kufika hapo walipo. Washauri (mentor) wamepitia njia unayohangaika nayo sasa na wanaweza kukuongoza kufika uendako wa haraka zaidi kuliko kama ukienda mwenyewe.Kama unataka kuwa na afya njema, utahitaji kwenda kwa mshauri ambaye tayari ana afya. Kama unataka kuwa tajiri, basi pia mtafute mtu ambaye ni tajiri akupe baadhi ya siri zake.



10.siri ya kumi:JIWEKEE AKIBA
Wahenga walisema akiba haiozi na haba na haba hujaza kibaba. Watu wengi hudhani kuwa ili uweze kuweka akiba ni lazima uwe na kipato cha juu. Nakubali kabisa kuwa wakati mwingine watu hujikuta tukishindwa kutunza chochote kwasababu majukumu ni mengi kuzidi kipato chetu, lakini hebu chukua mfano huu:
Wakati ulipokuwa ukiingiza 50,000 kwa wiki, kwanini uliweza kuishi kwa hicho unachokipata na maisha yalienda? Kisha ulipokuja kupata 100,000 kwa wiki maisha yalibadilika kwa muda lakini baadaye ukaja kuona tena kuwa hiyo nayo haitoshi! Fundisho hapo ni kuwa binadamu hatuwezi kuridhika kwa kile tunachokipata na kwamba tunaishi kwa kile kinachopatikana.
Kwahiyo kama unaingiza 50,000 kwa wiki, ukifanikiwa tu kuweka 5,000 kwa wiki, kwa mwaka mzima utakuwa umeweka akiba ya 260,000! Lakini pia utaweza kujibana na kuishi kwa 45,000 iliyobakia.
Wengi wenu hapa mnapata zaidi ya hapa hivyo kama mkiwa na desturi ya kujiwekea akiba, hutaamini kiasi cha fedha ambacho utakuwa umefikisha baada ya mwaka mmoja au miaka mitano kwa malengo marefu zaidi. Anza sasa kujiwekea akiba.
Watu wengi waliofanikiwa huyazungumzia mafanikio yao kwa kuwaongelea watu fulani waliowasaidia kuwaongoza kufika hapo walipo. Washauri (mentor) wamepitia njia unayohangaika nayo sasa na wanaweza kukuongoza kufika uendako wa haraka zaidi kuliko kama ukienda mwenyewe.
Kama unataka kuwa na afya njema, utahitaji kwenda kwa mshauri ambaye tayari ana afya. Kama unataka kuwa tajiri, basi pia mtafute mtu ambaye ni tajiri akupe baadhi ya siri zake.
Je! Siri hizi 10 nilizokupa zimekufundisha au kukuwekea kitu kichwani?





Ni kwa muda sasa katika jamii nyingi kumwona kijana kavaa headphone akisikiliza mziki. Swali tunalojiuliza. Ni je hawa vijana wanavutiwa na asali ipi katika hiyo burudani? Tena sio jambo la kushangaza kusikia mdundo mkubwa ndani ya vyumba vya wanachuo na makazi ya vijana hasa wale walio wapya katika ajira.Wakati mikito ya muziki haitenganishwi na masikio ya vijana wengi.Siku hizi kuna magari,kumbi za starehe,ambazo ni mahususi kwa kuweka wadau wa mziki pamoja.Kama wewe ni mpezi wa fukwe lazima utakua unazijua hiace na gari binafsi ambazo huja na mziki 'mnene'.Na kama umeingia night club au kupita mahala penye disco ni rahisi sana kubaini kundi la masharobalo wakiegeza mfano wa wasanii wa magharibi wanaofanya miondoko ya kufoka foka. Remmy Ongala kutoka Afrika aliwahi kuuliza mziki ni nini?Kujua zaidi mziki ni nini na kwa sababu gani  vijana wanapenda sana mziki soma tafiti hapa chini.

1.Kufanya kazi wakati kuna mziki inapelekea hali chanya na kuongeza uzarishaji


2.Mdundo na mkito hufanya akili ijiamini na kuwa na nguvu

3.Kusikiliza mziki mara kwa mara ni tiba ya ubongo dhidi ya uvimbe wa hilo eneo(brain tumor)

5.Sauti kubwa kwa baadhi ya wapenda mziki huwapa furaha 




6.Maneno na mapigo katika baadhi ya miziki hupunguza msongo wa mawazo


7.Mziki hukomaza hisia changa na ni dawa ya kujiamini

9.kiafya inasemekana mziki huchangia kuzalishwa kwa chembe hai , kinga ya mwili na hupunguza matatizo ya moyo



Sunday, June 14, 2015
Wahenga husema ukitaka kuruka juu sharti uagane na nyonga na mgaa gaa na upwa hali wali mkavu.Ivi ni nani anayeamini mwalimu anaweza kufika mbali awe raisi au kiongozi wa nchi? Wakati  ukweli unasadiki kuwa, nafasi hizo za juu huheshimika kwa sababu ni kitovu cha mamlaka makubwa na hukaliwa na  wachache .Kuna asilimia kubwa ya viongozi katika ikulu  chimbuko lao linatokana na kazi ya kufundisha watu darasani.Kitendo kinachowapa  msingi wa kusimama mbele ya halaiki wakizungumza na kuongoza  .Haya matunda ya ualimu ni kiiza machoni pa  watu wanaobeza taaluma hiyo kila kukicha.Kwa madai kuwa   ’ualimu ni kitanzi cha ajira ‘ na(walimu) hawaishiwi vitimbwi dhidi ya serikali .Ukizingatia katika moja ya sherehe za wafanyakazi hapa nchini, waalimu  wamewahi kutuma ujumbe kwa raisi uliovuta umakini wa mamilioni ya watanzania.Ujumbe ulibeba maneno mawili tu ,  yaliosomeka ’’shemeji unatuchaje’’lakini ‘message’ ilikuwa ‘sent and delivered’.hahahaha lazima ucheke.Ukiweka kando mzaha  huo na ubezaji, bilashaka tutakubaliana kuwa viongozi na waalimu wana mambo kadhaa yanayoendana,moja ikiwa ni  watu wanaofanya kazi  karibu na jamii , lakini pia wana fursa inayowaka  kama mwenge wa taifa unaosubiliwa kwa hamu ulete maendeleo ya nchi.Basi sikuchoshi tena na wafuatao ni   maraisi waliofikia hicho cheo ilihali wanajua dustor,chaki na rula zinakazi gani ubaoni  
 1.Baraka Obama.

2.Yoweri Museveni.

3.Robert  Gabriel Mugabe

4.bill Clinton

5.Kwame Nkrumah


6.John Evans Atta Mills

7.kenneth Kaunda


8.Benito Mussolin


9.julius Nyerere




Popular Posts