Monday, December 8, 2014
Kwa muda mwingi wasanii wamekuwa wazungumzaji wakuu , wakisema visa na mikasa ya kila siku.Sauti zao hujadili makosa ya jamii, mafanikio ya jamii n.k. Wakati wakiongelea  makosa ambayo huambatanishwa na shughuri za kibinadamu zisizofanikiwa au kutekelezwa kwa kiwango stahiki. Pia wasanii huangaza mafanikio ya watu katika jamii kwa kutazama  jitihada za mwanaume au mwanamke zilizotoa matunda katika utaftaji wa maisha bora.Msaani mmoja anapofanikisha kuongea juu ya kushindwa na kufaulu kwa kugusia shida na raha lazima kazi yake ipendwe na jamii.Vile vile msanii anapoweza kutia moyo watu au  mtu aliyepoteza matumaini ya kuishi halikadhalika kazi yake hupendwa.  Na pale huyu msanii akifumbua fumbo  gumu kwa wananchi, mchango wake daima hausahauliki mapema. Katika jopo la la watu ambao ni kioo cha jamii ,hatuwezi kuwasahau wanamuziki. Kwa kuwa ni miongoni mwa wasanii muhimu katika jamii, ambao hugeuka waalimu na kutoa maarifa ya mambo yatukabiliyo kila mara. Hivyo nakusihi ufuatilie kile wasnii wa Afrika mashariki wanachosema   kuhusu maisha.

1.''maisha ni kama safari ni safari hakuna ajuaye kesho itakuaje''Jaquar


2.''Maisha ni sawa na kupiga mbizi,leo juu kesho chini,usinicheke kukosa.''Twanga pepeta.

3''Maisha ya mtaani ninanayo yaona sio sawa na ya shule niliyoyasoma''FID Q,na witness



4.'' Maisha ni fumbo fumbua,maisha ni bahati ,ifumbate  maisha ni mapigano,pigana'' Mwijuma Muumin

5.''Maisha ni kitendawili kigumu sana leo umepata kesho umekosa'' kimobitel

6.''maisha ni tendo lifanikishe,maisha ni huzuni ishinde,maisha ni mtihani faulu'' Mwijuma Muumin

7 .''Maisha ni safari nitafika msafiri kwa imani ya kuamnika sitofichwa kama siri''One the Incredible

8. ''maisha ni karata unaweza ukalamba dume,ukalamba garasha, ukalamba mzungu wa nne''Geez Mabovu



Tuesday, December 2, 2014
Mwezi novemba  mwaka 2014 nilifika mkoa fulani hapa Tanzania kwa ajili ya mahafali . Na kwa kuwa  matumizi ya simu za kisasa''smartphone'' ni makubwa  kwa kila mmoja ili nibidi ninunue simu ya dizaini hiyo ilahisishe mambao yangu. Hii ilikuwa ni simu ya tecno H6 iliyoweza kupiga picha za ubora mzuri kama zile za kamera ya kawaida. Ila mungu si Athumani asubuhi ya keshokutwa, siku mbili baadae,  niliamkia mazoezini kama ada yangu . Nikikimbia kando ya bahari ya hindi kwa muda wa nusu saa hali iliopelekea kuchoka sana kwani ni muda sijafanya joging. Hata jioni nikiwa katika mgahawa mmoja ,najivinjari kwa smartphone mkono wa kushoto na maji mkono wa kulia nikinywa taratibu kwa fundo la kizembe bado nilihisi uchovu wa mwili na akili uliotokana na zoezi la asubuhi. Baadae kidogo niliondoka eneo hilo la chuo kulipokuwa na mgahawa nakuelekea nje. Nikiwa nje nilitaka kuwajuza marafiki zangu kuwa nipo tayari mkoani hapo,  ndio ghafla nashishituka sina simu mfukoni wala mkononi. Japo akili ilikuwa imechoka ,  niliweza kumbuka kuwa , kabla ya kulipia maji kwa muhudumu niliacha simu mezani na sikuichukua wakati naondokka eneo hilo. Nikafanya jitihada za kumdadisi mhudumu hakuweza kufahamu lolote. Nikauliza watu waliokuwa karibu yangu wakitazama mechi ya West Brom na Arsenal Betting iliyochezwa siku hiyo ya jumamosi tarehe 29 novemba , nao pia walikana  kuiona smartphone yangu mpya iliyokuwa na siku tatu tu toka ninunue. Hatimaye nimeuliza mtandaoni na majibu yao yameshauri matumizi ya programm zifuatazo.


1. LOOKOUT. Hii ni moja ya programm inayomwezesha mmliki wa simu aina ya android kubaini mienendo ya simu iliyopotea. Huku ikitoa taarifa  mahala simu ilipo , Pia hii programu inapiga picha za siri bila mwizi au aliyechukua kutambua na kutuma moja kwa moja  kwa  anuani yako uliojisajilia katika hiyo programm.Ina uwezo wa kufunga ama kufuta habari binafsi zilizondani ya simu na endappo upo karibu na mtu mwenye simu yako programm inakuwezesha  kuruhusu simu itoe alarm na kumkamata mwizi.




2. LOOKOUT PLAN B. Tofauti ya programm hii na ya kwanza ni kuwa Lookout plan B hutumika na baadhi ya simu tu zinazotumia mifumo ya android. Na wakati programm zote katika hii list zinahitaji kuwekwa katika simu kabla haijaibiwa, Lookout plan b inaweza kuingizwa katika kifaa kilichopotea ama kuibiwa hata baada ya mwizi kutokomea Ni kwa njia ya mtandao Lookout Plan B huweza kufikia simu iliyopokonywa.



3. PREY. Kama zilivyo programm nyingine hii pia inapatikana Google play , yaani katika simu zitumiazo android . Au kwa urahisi sana zinajulikana kwa jina la '' simu za tachi' '(touch). Prey ni programm ambayo inauwezo wa kuonyesha mitandoo yote inayotumiwa na simu yako iliyopotea. Lakini hata kama kulikuwa na picha za muhimu hii ni prograam iayoweza kuzihifadhi katika account au anuani yako ya google.Zaid Prey huweza kutumika hata kutafta laptop na tablets zilizopotea.





4. FIND MY PHONE. Hii programm inatofautiana na nyingine kwa kuwa inawafaa watumiaji wa Iphone na vifaa vingine vinavyotengenezwa na  kampuni  ya Mac.Ambao ni wazalishaji wa ipod, ipad na simu zaIphone.  Habari nyeti za mtu alizoacha katika simu hupelekwa na  progrmm hii hadi uwanja wa icloud. ambako mmliki wa simu hufika kwa kufanya usajili mdogo. Hapa utajua simu yako iko wapi, nani anaitumia kwa kutazama picha zilizopigwa kwa usiri wakati mwizi akiitumia.
                                                                                     






5. ANDROID DEVICE MANAGER, Ni aina nzuri ya programm katika kurudisha simu kwa kuwa ina sifa kama programm nyingine ikiwemo ile ya kuwafaa watumiaji wa android, Pia ina mambo muhimu ya kuzingatia kama ; kupata simu iliyopotea .kwanza. inatakiwa iwe imeunganishwa na mtandao, pili,  iunganishwe na na programm hii kabla haijaibiwa,  tatu, simu itaonekana baada ya kuwa karibu na minara ya simu, huduma za wireless, bloothooth na mifumo mingine yenye kutuma mawasiliano katika satellite za google , nne, kuifikia simu iliyopotea unatakiwa kutumia simu tofauti, computer au kifaa kingine. Mwisho hii programm kama hizo zilizotajwa juu hupata simu ikiwa imewashwa na sio kuzimwa

.Kumbuka ni vyema kutoa taarifaya upotevu wa mali yako katika uongozi wa serikali kama polisi au ofisi ya kijiji kabla ya kufanya ufuatiliaji kwa kutumia programm hizi.

Saturday, November 8, 2014
Safari ya miguu 100 huanza na hatua moja. Ni kanuni  iliyodarizi safari nyingi za mafanikio. Kutana na safari ya aina hii  inayomhusu mwanafunzi Ben, anayetokea  familia  ya chini yenye mzazi mmoja, anayemudu milo mitatu kwa taabu. Ili watoto wa familia hii  washibe mama anapaswa kujinyima, akihangaika na kazi mbili , tatu au zaidi. Wakati wazazi wengine wameketi na kazi moja  inayowalipa vyema  , mama Ben hukatisha usingizi mnono ili kuanza mapema kazi   za kupiga deki, pasi, kufua  nguo, kuosha vyombo n.k . Mama huyu  huzunguka nyumba  za madokta, maprofesa na watu wengine wenye kipato cha juu ambako hufanya  kazi hizo za ndani . Hali inayomfanya kukimu familia  tu na  asifikirie kuponda raha ama kula bata wasemavyo vijana wa sasa. Hivyo hiyo fedha kidogo anyoipata hugharamia mlo, mavazi na elimu ya wanaye . Kwa hii nafasi mzazi huyu katimiza malengo mawili ; kumkabidhi elimu mtoto wake, na  yeye mwenyewe kumkabidhi mungu naisha yake. Kama kipepeo afuatavyo ua , mmea ufuatavyo jua  .Mwanae Ben anafuatilia elimu kwa umakini mkubwa.Lakini jitihada zinagonga mwamba baada ya kushika nafasi za mwisho darasani. Kitu kinachoibua chachu ya kujaribu tena kwanI Ben anajua fika hana urithi mwingine zaidi ya elimu. Na huo ndio unakua mwanzao wa Ben kukamata nafasi za  kwanza darasani, anafaulu kuingia chuo,na kuchukua masomo ya kitabibu. Hadi leo Ben ni Miongoni mwa madaktari bingwa anayefanya upasuaji wa   ubongo, ikulu ya ufahamu wa binadamu. Dr Ben Carson kafungua taasis ya kusaidia watu wasiojiweza maalufu kama Dr Ben Carson Foundation, kafanya upasuaji mgumu  wa kutenganisha mapacha walioungana vichwa , Dr Ben kapokea tunzo nyingi za heshima na ni muamerika muafrika wa kwanza  kufanya kazi katika kitengo nyeti  cha afya  kilichipo nchini Marekani akiwa na umri mdogo zaidi. Ben sasa ni baba na anafamilia anayoitunza na kuipenda  na sasa ana kula mlo  bora wa chakula cha aina yeyote anachotaka..Mpaka kufika hapo Ben anaorodhesha mambo sita yaliomfanya avune pakacha kubwa la mafanikio kiasi hicho.

1.Kutambua Kipaji. Kila mmoja ana uwezo wa asili katika  kazi,wajibu ama jambo fulani linalohitaji nguvu na akili. Mmoja huweza kuimba,mwinginekuongea, kuongoza,kufundisha n.k ,mmoja kufikiri,mwingine kutenda,kuhamasisha, kushawishi n.k. Huu uwezo binafsi(Kipaji) ukitambulika na kuendelezwa katika nyanja sahihi . Maisha ya kila mmoja wetu yatakuwa bora zaidi.katika Ualimu,uongozi,biashara,sheria,udaktari na kazi nyingine aipendayo.


2.Kuwa muaminifu.Ben,anaona uaminifu kama rangi inayo mtambulisha kila mmoja wetu zidi ya watu wamzungukao.Ukienda kinyume na kuwa raghai watu watakufahamu kwa  tabia hiyo ambayo madhara yake ni kujifungia milango mingi ya fursa zilizo mbele yako.Ila kwa kubakia muaminifu upendo wa jamii,familia na marafiki utaongezeka hata upatikanaji wa nafasi mbalimbali utaongezeka pia, kwa maana uaminifu hujenga  imani na matumaini mioyoni mwa watu wakuzungukao.



3.Jifunze kwa waliofanikiwa.Karibu kila ndoto tulizonazo kuna watu walizitimiza, hivyo ni vyema kujifunza kutokana na hao waliotutangulia kwa kuangalia walianza lini, waliweza vipi, kwa nini walishindwa na kutokata tamaa hata baada ya matatizo kuwa kabili..Kama una ndoto ya uongozi kuna viongozi bora duniani,nchini na mikoani.Kama ni ujasiliamali wapo wa kimataifa,kitaifa,wilaya hadi mtaani.Ukitaka kuwa hodari jifunze kwa mahodari ,na ukitaka kuwa mzuri jifunze toka kwa wazuri.


4.Kuongeza Elimu na maarifa. Unapokuwa na ujuzi, uelewa, na uzoefu lazima uhitajike na kuthaminika Elimu hiyo uliojifunza toka kizazi fulani, shule fulani, darasa fulani, mtaa fulani ina stahili kuongezwa mara kwa mara ili kupata ufanisi mkubwa.Hata kisu kitumikapo bila kunolewa hupoteza makali. . Kadri unavyokuwa na elimu zaidi ndo utakavyokuwa muhimu na wa thamani zaidi.


5.Kutumia Vitabu. Siri za maarifa makubwa zimefichwa katika vitabu vidogo.Utulivu wa fikra za wasomi zipo vitabuni. Mawazo endelevu ya wajuzi walio na busara yapo vitabuni. Hekima ya maelekezo rahisi juu ya mambo magumu  huhifadhiwa katika kurasa za vitabu.Kwa muujibu wa Carson,  usomaji wa maandishi kama vitabu ni maradufu kwa kujenga akili, maarifa na elimu katika kichwa zaidi ya kutazama tv au kusikiliza sauti. 




6.Kuwa na hofu ya mungu. Ben,anaamini kuwa hakuna kipaji,uaminifu, elimu, kujifunza, wala vitabu kama hukumtanguliza mungu mbele. Kwani kila kitu alichoumbiwa mwanadamu kililetwa mbele yake na mungu. Hivyo ni vyema kumuomba mungu akutangulie katika kila jambo unalofanya,na unalotarajia kufanya kwa maana yeye ndio mwenye utaratibu na ratiba ya hatma zetu.






Monday, September 15, 2014
Kuna wakati sisi wananadamu hupoteza mwelekeo  kama boti ndogo inayopigwa na dhoruba kubwa baharini. Ni muda ambao maisha huturushia tope, mawe, miiba na kila aina ya shida, Katika wasaa huu ni kawaida mtu kubaki njia panda, aidha kuendelea ama kutoendelea na jambo fulani alilokusudia hapo mwanzo. Tunapochagua kuendelea, huwa tumecheza karata sahihi. Kwani  mafanikio ni hali inayoanzia chini na baadae kufika juu ya kilele cha maendeleo aliyojipangia mtu mmoja. Watu wengi tumewahi kufanikiwa kwa namna moja ama nyingine. Lakini kadiri tunavyopiga hatua moja mbele , vikwazo navyo hutuvuta kwa hatua mbili  nyuma. Bila shaka umewahi kuona filamu ya nchini Thailand inayoitwa Ong Bak?. Ndani ya sinema hii kadiri  starling anavyopiga maadui ndivyo wanavyozidi kuongezeka. Halikadhalika na maisha ya kawaida, hali huwa hivyo .Jinsi tunavyofanikiwa zaidi na  mambo  huwa mengi zaidi. Hata Nasib au Diamond Platnums, mwanamuziki anayefanya vizuri Afrika mashariki.Hivi sasa ana ziara nyingi za muziki, Kenya,Uganda,Rwanda,Burundi na Ulaya.Hali inayomfanya,ajifunze lugha za kigeni, aandae nyimbo nzuri, afanye mazoezi ya kutosha kuliko wakati hajaanza sanaa ya muziki. Hii inatokana na ukweli kuwa ,mafanikio ni safari moja ambayo huanzisha mambo mengine. Mbali na sanaa hata katika biashara , tajiri Bill Gates ambaye sio  mgeni  masikioni mwetu. Anakiri kuwepo kwa changamoto katika mafanikio licha ya kumiliki na kuendesha miradi mikubwa ulimwenguni. Mtu huyu aliyeanza uwekezaji   akiwa na umri wa miaka tisa  ,kapitia shida ya kimasomo hata safari yake ya elimu  ikayumba kiasi. Lakini leo hii   anatuuzia vifaa,program,computer,smartphones .Bidhaa zinazoundwa na kampuni yake iitwayo  Microsoft.Hivyo   wafanyabiashara ,wasanii na sisi tunakila sababu ya kutokata tamaa na kufanikiwa ili mwisho wa siku tutimize mahitaji  yafuatayo:

1
. 

                               

2.Usalama wa maisha

                                                                                         

3. upendo na mahusiano 

                                                              

.4.Uwezo na heshima.

                                                            

.5. Uhuru katika
















Thursday, September 11, 2014
Ibrahim na Neema huvutiwa sana na mitindo.Ndoto yao juu ya tasinia hii ilianza kwa kupenda   haiba na unadhifu.Wakiwa ni vijana wasio na ajira hawakuweza kutafta mvuto kwa namna inayohusisha gharama kubwa.Hawakuweza kuingia  gym, hawakuwrza kumudu vifaa maluum vya bei mbaya. Hali iliyopelea mmoja kati yao kutafta mwalimu  wa mazoezi ya mwili kwa njia ya mkopo. Na mwingine kujisimamia katika mazoezi ya aina hiyo bila mwalimu kabisa. Neema alipata msaada mkubwa toka kwa huyu mwalimu wa mazoezi. Ibrahim halikadhalika  alifanikiwa kutokana na bidii aliyojiwekea katika mazoezi. Wawili hawa katu hawakukata tamaa ya mazoezi hata siku moja kwa kuwa walipenda michezo kuliko kitu kingine.Walipenda  kuwa wanamitindo kuliko kazi nyingine. Walivutiwa na uzuri kuliko sifa nyingine. Baada ya miezi mitatu kupita  huku zoezi ni kama dini na kitu cha muhimu kwao, mmoja wa vijana hawa anatokea kuwa kisura aliyevutia sana na mwingine ni mtanashati aliyependeza sana. Huku siri yao kubwa kufika hapo walipo ndani ya muda  kidogo, ikitokana na  juhudi katika mazoezi yafuatayo..

1,KURUKA KAMBA. Ni zoezi rahisi lisilochukua gharama kubwa.Zoezi hili linafanyika sehemu nyingi kwa sababu vifaa vyake ni rahisi kubeba na hupatikana kwa uepesi.Kwa kuwa linahusisha mikono,miguu,mgongo na viungo vingine vya mwili,huongeza stamina,nguvu na kukaza misuri ya mrukaji. Ni moja ya zoezi zuri katika kupunguza uzito wa mwili.

2.KUKIMBIA.Ni zoezi linalofanyika uwanjani,barabarani,mbugani na sehemu nyingi za uwazi mkubwa.Zoezi hili hupendeza pasipokuwa na jua kali hasa majira ya asubuhi na majira ya jioni..Ni moja ya zoezi zuri kwa mapafu na moyo.Kwani viungo hivi hurejesha msukumo wa damu na hewa  kuwa vyema,kiasi cha mkimbiaji kupata nguvu na pumzi ya kutosha katika mwili wake.

3.PUSH UP. Ni zoezi rahisi, linalochukua gharama ndogo sana na gharama hii ni muda pekee . Mbali na muda, push up hazihitaji uwanja  mpana zaidi ya chunba chako. Kwa kupiga push up ndani ya nyumba itakusaidia kukaza mwili sehemu ya juu. Ukianza na kupanuka  kifua, ikifuatiwa na kuimarisha mabega, mikono  mgongo na  tumbo. Ni zoezi zuri kwa ukakamavu

4.KUOGELEA . Ni mchezo ambao huvutia watu wengi, watoto kwa wakubwa wenye kipato na wasionacho. Lakini wakati karibu kila mmoja anafurahai mchezo huo, kuna faida nyingi mwili hupata  Kwanza ni mara mbili ya zoezi la kukimbia, na huimarisha misuli ya mwili kutokana na ukinzani wa maji. Pili huondoa mfadhaiko na msongo wa mawazo, tatu ni zoezi linalohusisha
miguu, mikono, mabega na viungo vya mwili karibu vyote na baadae mwili hujengeka na kukaa fiti.
5.KUENDESHA BAISKEL. Kwa kuendesha tu usafiri wa baiskel ni sehemu ya zoezi muhimu sana kwa afya . Miguu inapokazana kupita mpando na ama tambarare.  Mwili unashitua misuli inayosukuma nguvu zaidi . Zoezi hili linasaidia ubongo kwa kuwa makini na kunakiri chochote kinachoendelea. Unapofikia hatua ya kutoa jasho wakati wa zoezi hili , inasaidia kupunguza taka mwili na mafuta yasiotakiwa mwilini. Hatimaye mwendeshaji mwenye uzito mkubwa atakuwa anapunguza uzito endapo tu ataendesha baiskel mara kwa mara.
Sunday, August 24, 2014
Katika ukuaji wa mtu ndani ya jamii fulani, unashabihiwa na mambo zaidi ya manee , na ukuaji huo hautofautiani na ule wa mmea ndani ya msitu.Mmea hauchipui hadi kuwa hatua ya mti bila kuathiriwa na joto, mwanga, maji na udongo.  Usawa wa hivi viumbe hai ki makuzi unapatikana  baada ya mimea na watu kuzongwa  na athari za mazingira yanayozunguka viumbe vyote viwili . Haya mazingira mwisho wa siku ni sababu za unyoofu, uzuri, afya, stamina na maisha marefu ya  viumbe hao. Wakati mimea inakumbwa na athari zitokanazo na mazingira  kama hali ya hewa, rutuba, ardhi n.k .Binadamu anakabiliwa na  vipengele vitano vinavyoathiri maisha yake ambayo  ni ;familia, makundi,  shule, dini na vyombo vya habari. Vipera hivi   ni mizizi ya uelewa kwa binadamu , na huwa havifuatani kwa mtiririko na mpangilio maalum isipokuwa hutokea kulingana na muda pamoja na mahali mtoto anapoishi.
.1.Familia ni kitovu awali cha maarifa kwa binti ama kijana. Kupitia familia, watu hawa hujua dunia kwa mara ya kwanza katika hali mbili; ya kuishi na watu na jinsi  ya mapokezi . Ueredi unaosababishwa na vitendo vya kunakiri na kurudia wafanyavyo wazazi na ndugu wengine wanaowazunguka vijana .Marudio ni njia pekee kwa wanajamii wachanga kujaribu mienendo na maisha ya utu uzima. Kupitia mikono ya mama, baba,kaka ,dada , shangazi ,mjomba n.k , mtoto hukomaa kiakili na kimwili mpaka kujibu maswali mengi juu ya dunia.
2.Shule ni uwanja wa elimu unaofafanua mazingira, hali, historia,na maarifa  kuhusu mtoto anapotoka, alipo na atakapo kwenda. Mambo haya huwa katika masomo na  sehemu ndogo ndogo ambazo huitwa mada au topic .Kisha huandaliwa waelimishaji maalum ambao husimama baadala ya wazazi ili kufundisha  watoto hawa, ambacho ni kizazi kisichokuwa na maono pevu juu ya ulimwengu.Waelimishaji huitwa waalimu na na watoto  huitwa wanafunzi. Wakiwa shuleni huendelea kubadiri utafakali wa matukio, maada, watu na vitu kutokana na masomo mbalimbali wanayopata ndani ya taasisi hiyo.Hata wakiwa vijana, ambayo ni hatua kiasi ya ukomavu wa binadamu.Shule na taasisi nyingine za elimu  hupanuka kwa kujali umri na uhitaji ya huyu mwanajamii komavu.Kwa kumuelekeza afuate nini,aache nini,anapaswa kuifanyia nini jamii yake na kuafanua kwa kina taifa na dunia ni dhana zenye mantiki gani mbele ya uso wake.




..3.Makundi ni idadi ya wasichana ,wavulana na watu wengine wanaovutiwa  kuendesha jambo katika hali ya ushirikiano ,wingi na  umoja  . Kama msemo usemao'' onyesha rafiki zako nikueleze tabia yako''.Ndivyo makundi  huathiri ukuaji wa mtu mmoja. Katika makundi, marafiki wakikutana, watu wa rika moja wakionana, na  wenye umri unaoendana  wakijumuika, huathiriana mmoja baada ya mwingine hatimaye wote. Athari yake hujipambanua katika mazungumzo, hisia, ufahamu na mtazamo  wao.Hali inayotokea aidha wakiwa wanafahamu ama kutotambua mabadiriko hayo .Kama uzi wa mafuta unavyoshika moto kwa kasi, halikadhalika tabia ya mtoto mmoja hushika na kuenea kwa wenzake.Japo mara nyingi huwa ni jumla ya tabia za watoto ndani ya makundi zinazoathiri akili ya  mvula ama msichana mmoja.Endapo kundi sio jema mtoto hubomoka kwa kuwa na maadili mabaya na kundi likiwa bora kijana hujengeka kwa kuwa na tabia sitahiki .
4.Dini  ni kisima cha imani, chenye utamaduni na taratibu maalum kinachotoa mafunzo ya kiroho kuhusu mwenendo wa mtu na namna ya kukabiliana na ulimwengu  .Elimu ya kina hutolewa na watu maalum walioteuliwa kwa misingi na kanuni za dini na madhehebu tofauti tofauti.Huu  ni utaratibu ambao unashabaha ya kuwezesha  binadamu kupata mafunzo ya mambo yasionekana na yale ya kimwili.Wakati utaratibu wa kupata haya mafunzo hupitia kuabdu, kusali, ama kuswali ukiendelea. Dini huwa kama shule kwa kuwa na watu wa aina mbili, watu wanaofika ili kupata elimu  ambao huitwa waumini.Na wengine ni watu ambao hutoa hayo mafunzo, ambao pia hupewa majina kulingana na aina ya dini.Ndani ya dini mambo yasionekana ama kujificha huitwa  mambo ya kiroho. Huku yale ya onekanayo au  ya kimwili yakibakia kuwa ni kuvaa, kula, kunywa , kulala n.k. Hivyo waumini huenda katika madhehebu yao  ili kupokea maarifa juu ya mambo ya kawaida na yale ya kiroho.Muumini aendae kinyume na utaratibu uliopangwa huwa amefanya makosa ambayo hutambuliwa kama dhambi,ama maovu na kutakiwa kutofanya hayo makosa tena.Mwisho vijana waliokulia ndani ya dini huwa ni toauti na wale ambao hawakulelewa katika misingi hiyo.   
 




 5.Kipengele cha tano  ni vyombo vya habari , ambavyo huwa ni hatari na baraka kutegemea na  kijana na huduma za hivyo vyombo.Kijana atakuwa  katika  hatari inayotokana na vyombo kama redio, televisheni, magazeti, na mitandao (internet) pale atakapokosa misingi   endelevu ya kujisimamia.Ambayo inatokana na familia, ushauri mzuri wa makundi, elimu bora ya shule na mafunzo ya dini. Kwa maana vifaa hivi vya mawasiliano  huchukua  tamaduni, imani, lugha, sanaa, michezo na tanzu zote za maisha toka sehemu tofauti za dunia.Kama vile jamii za kisasa ,taifa lililoendelea, na mabara yenye hatua nzuri za kimaisha.Na kupereka katika jamii zinazoishi maisha ya kale na zama za nyuma.Vyomba vya habari hutoa picha za maendeleo toka ughaibuni kitu ambacho huwavutia  vijana wengi katika mataifa yanaendelea na kutaka kuwa kama hao wawaona katika sinema, magazeti,internet na mitandao mingine ya kijamii.Usishangea mavazi ya kileo,misemo ya kisasa,nyimbo ,mahusiano na miondoko ya vijana wa karne ya 21 .Hii ni sehemu yamapinduzi na athari zitokanazo na  vyombo vya habari tulivyonavyo chumbani,sebureni,mtaani na kwingine kote.
 

Popular Posts